Habari za usiku huu wanajamvi? Poleni sana kwa mihangaiko ya siku nzima ya leo pia kwa wale wakazi wa Dar poleni sana kwa foleni ya siku ya leo. Hope baada ya kufika now tupo kwenye jukwaa letu pendwa.
Now back to the topic, hapa nilipo nina kisirani na kero ambayo hata imechangia kuharibu siku yangu tangu usiku wa jana, kisa mtoto wa ,marehemu kaka yetu. Ipo hivi; kaka yetu mkubwa alibahatika kuzaa akiwa shuleni miaka hiyo.
Huyo mtoto nimepishana naye kama miaka mitano so kwa kiasi Fulani nimekua naye kabisa kama mdogo wangu wa kunifuata maana mie die kitinda mimba katika familia yetu. Huyu mtoto amekuwa na tabia za ajabu sana tangu akiwa mdogo kama vile ubinafsi, matumizi mabaya ya fedha, uchonganishi, kiburi na mengineyo mengi ambayo hata kwa sasa ndio yamenipelekea naandika uzi huu.
Tumeanza kumlea tangu tangu akiwa na umri wa miaka mitatu baada ya wazazi wa mama yake kutuzilia hapo ndio ikawa hadi wazazi wake wanafariki katikati na mwishoni mwa miaka ya tisini. So hadi wazazi wetu nao pia wanafariki alikuwa ni mdogo sana ndio kwanza yupo form one wakati mie nipo form six. In short baada ya mie kumaliza chuo na kuanza kazi ikawa ni jukumu letu na dada yangu kumsomesha huyo mtoto ili nae apate msingi bora wa maisha ingawa alikuwa na usumbufu ila darasani hakuwa haba kwa kweli.
Nakumbuka mwaka juzi alichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kimoja hivi cha binafsi hapa nchini, kweli tulijipinda na kumpeleka. Akiwa huko vibweka havikuisha kabisa kwa kupiga vibomu vikubwa vikubwa huku na huku (kwangu na sister). Baada ya kushitukia hila zake dada alipendekeza mie kuwa ndie in charge bila ya kujua kuwa naingia kwenye shimo la moto nikakubali.
Akiwa chuo alipiga bomu moja kubwa sana akijumlishia na gharama za medical capitation, wakati huo bima anatumia kadi ya bima ya afya ya kwangu niliomkatia. Nijuavyo ni kuwa chuoni kama mtu una bima ya afya ya shirika Fulani unaweza usichangie hiyo medical capitation given kuwa umeweka taarifa zako bayana kuwa una bima gani na ni mwanachama hai
So baada ya hiko kibomu nikiwa pamoja dada yangu nilimpa taratibu za kufuata ili kuweza kuweka mambo yake sawa ili kupunguza gharama zisizokuwa za lazima kwangu na dada. Alionekana dhahiri kutoridhika na ile proposal yangu ila nikakomaa nae nikamwambia kuwa nampa siku tatu afanye follow up then when he is done anambie alipofikia kama kaweza au la. Basi ile kumwambia vile ndio ikawa kama nimekata undugu maana sikupata hata missed call kutoka kwake hadi wiki inaisha. Nikaona sasa isiwe taabu maana shida zake yeye anataka tena alete kiburi, so na mie nikawa jeuri nikakaa kimya.
Amini msiamini ilikuwa ni mwezi wa 9 mwaka jana alikaa kimyaaaa hadi mwezi wa 12 tarehe 31 aliponitumia message inasema hello papaa! Happy new year. Yo ma dad and am ya son. I always love you ila kama ni shida zangu nitajitahidi kutokukushirikisha Hiyo text nimecopy na kupaste kama alivyotuma nothing added or removed. Kwa kweli ilinikera na nikaona kama anajiona tayari kajipanga kimaisha, let him be. Niliendelea na ukimya wangu ili kuepusha shari na wala sikutaka kumwambia mtu.
Jana usiku wa saa nne nilimpigia dada simu kumjulia hali ndio hapo ikawa balaa sasa. Dada aliuliza mara ya mwisho ni lini ilikuwa kuongea na mwanao?
Nilimwambia kila kitu juu ya misbehavior za mtoto. Alichonambia ni kuwa mie nakuwa mjinga na katili. Akaendelea kuwa kama hapo ukiambiwa mwanao anaumwa je? Nikajibu kuwa kwa kuwa ana bima ya afya basi mie wala sitokuwa na wasi na kama akihitaji msaada kama kweli nitatoa msaada wangu kwa kadiri niwezavyo.
Basi hapo dada yangu aliwaka vibaya mno kuwa mie katili, mtoto wiki ya tatu hii anaumwa halafu mie natoa majibu mepesi what I told her ni kuwa je ningeota au ningejuaje kama yeye aliamua kukaa kimya.
Dada aliendelea kuwaka na kunivisha kila aina ya ubaya akimtetea mtoto. (sijui wana ajenda gani ya siri maana it seems wao wana mawasiliano ya karibu ambayo mie siyajui na sijui wanaongea nini).
Baada ya kuona vile dada anakuja juu nilikata simu kwa hasira. Hakuishia hapo, alituma message ikisema Ahsante umekuwa nashukuru, nakuacha kama ulivyosema ndugu zako ni hao wa mkeo ila
Hapo pia nilishindwa kuelewa mke wangu anaingilia wapi jamani? Yaani usiku wa jana ulikuwa mchungu, kazi hazikwenda leo na hata sasa nipo mood less.
Hapa nashindwa kuelewa kosa langu lipo wapi? Je mwisho wa haya yote ni nini? Huyu mtoto nimfanyaje? Naombeni ushauri na maoni yenu wadau na pia samahani kwa posti ndefu namna hii but I was trying to explain the situation exhaustively.
Karibuni.
Now back to the topic, hapa nilipo nina kisirani na kero ambayo hata imechangia kuharibu siku yangu tangu usiku wa jana, kisa mtoto wa ,marehemu kaka yetu. Ipo hivi; kaka yetu mkubwa alibahatika kuzaa akiwa shuleni miaka hiyo.
Huyo mtoto nimepishana naye kama miaka mitano so kwa kiasi Fulani nimekua naye kabisa kama mdogo wangu wa kunifuata maana mie die kitinda mimba katika familia yetu. Huyu mtoto amekuwa na tabia za ajabu sana tangu akiwa mdogo kama vile ubinafsi, matumizi mabaya ya fedha, uchonganishi, kiburi na mengineyo mengi ambayo hata kwa sasa ndio yamenipelekea naandika uzi huu.
Tumeanza kumlea tangu tangu akiwa na umri wa miaka mitatu baada ya wazazi wa mama yake kutuzilia hapo ndio ikawa hadi wazazi wake wanafariki katikati na mwishoni mwa miaka ya tisini. So hadi wazazi wetu nao pia wanafariki alikuwa ni mdogo sana ndio kwanza yupo form one wakati mie nipo form six. In short baada ya mie kumaliza chuo na kuanza kazi ikawa ni jukumu letu na dada yangu kumsomesha huyo mtoto ili nae apate msingi bora wa maisha ingawa alikuwa na usumbufu ila darasani hakuwa haba kwa kweli.
Nakumbuka mwaka juzi alichaguliwa kujiunga na chuo kikuu kimoja hivi cha binafsi hapa nchini, kweli tulijipinda na kumpeleka. Akiwa huko vibweka havikuisha kabisa kwa kupiga vibomu vikubwa vikubwa huku na huku (kwangu na sister). Baada ya kushitukia hila zake dada alipendekeza mie kuwa ndie in charge bila ya kujua kuwa naingia kwenye shimo la moto nikakubali.
Akiwa chuo alipiga bomu moja kubwa sana akijumlishia na gharama za medical capitation, wakati huo bima anatumia kadi ya bima ya afya ya kwangu niliomkatia. Nijuavyo ni kuwa chuoni kama mtu una bima ya afya ya shirika Fulani unaweza usichangie hiyo medical capitation given kuwa umeweka taarifa zako bayana kuwa una bima gani na ni mwanachama hai
So baada ya hiko kibomu nikiwa pamoja dada yangu nilimpa taratibu za kufuata ili kuweza kuweka mambo yake sawa ili kupunguza gharama zisizokuwa za lazima kwangu na dada. Alionekana dhahiri kutoridhika na ile proposal yangu ila nikakomaa nae nikamwambia kuwa nampa siku tatu afanye follow up then when he is done anambie alipofikia kama kaweza au la. Basi ile kumwambia vile ndio ikawa kama nimekata undugu maana sikupata hata missed call kutoka kwake hadi wiki inaisha. Nikaona sasa isiwe taabu maana shida zake yeye anataka tena alete kiburi, so na mie nikawa jeuri nikakaa kimya.
Amini msiamini ilikuwa ni mwezi wa 9 mwaka jana alikaa kimyaaaa hadi mwezi wa 12 tarehe 31 aliponitumia message inasema hello papaa! Happy new year. Yo ma dad and am ya son. I always love you ila kama ni shida zangu nitajitahidi kutokukushirikisha Hiyo text nimecopy na kupaste kama alivyotuma nothing added or removed. Kwa kweli ilinikera na nikaona kama anajiona tayari kajipanga kimaisha, let him be. Niliendelea na ukimya wangu ili kuepusha shari na wala sikutaka kumwambia mtu.
Jana usiku wa saa nne nilimpigia dada simu kumjulia hali ndio hapo ikawa balaa sasa. Dada aliuliza mara ya mwisho ni lini ilikuwa kuongea na mwanao?
Nilimwambia kila kitu juu ya misbehavior za mtoto. Alichonambia ni kuwa mie nakuwa mjinga na katili. Akaendelea kuwa kama hapo ukiambiwa mwanao anaumwa je? Nikajibu kuwa kwa kuwa ana bima ya afya basi mie wala sitokuwa na wasi na kama akihitaji msaada kama kweli nitatoa msaada wangu kwa kadiri niwezavyo.
Basi hapo dada yangu aliwaka vibaya mno kuwa mie katili, mtoto wiki ya tatu hii anaumwa halafu mie natoa majibu mepesi what I told her ni kuwa je ningeota au ningejuaje kama yeye aliamua kukaa kimya.
Dada aliendelea kuwaka na kunivisha kila aina ya ubaya akimtetea mtoto. (sijui wana ajenda gani ya siri maana it seems wao wana mawasiliano ya karibu ambayo mie siyajui na sijui wanaongea nini).
Baada ya kuona vile dada anakuja juu nilikata simu kwa hasira. Hakuishia hapo, alituma message ikisema Ahsante umekuwa nashukuru, nakuacha kama ulivyosema ndugu zako ni hao wa mkeo ila
Hapo pia nilishindwa kuelewa mke wangu anaingilia wapi jamani? Yaani usiku wa jana ulikuwa mchungu, kazi hazikwenda leo na hata sasa nipo mood less.
Hapa nashindwa kuelewa kosa langu lipo wapi? Je mwisho wa haya yote ni nini? Huyu mtoto nimfanyaje? Naombeni ushauri na maoni yenu wadau na pia samahani kwa posti ndefu namna hii but I was trying to explain the situation exhaustively.
Karibuni.