Huyu Pogba wetu ni hasara tu

Huyu Pogba wetu ni hasara tu

Hamna lolote, LVG alikuwa msanii tu kwanza hata timu ifanye vibaya yeye alikuwa hanyanyuki kwenye kiti chake, alibaki kuandika andika tu na ndio maana timu ilifika kubaya sana na ikafkia kipindi tukaomba kocha mkali asiyechekacheka na ndo tunaye sasa,kilichobaki ni tumuunge mkono tu.

Mkuu huyu Kocha pamoja na kumuunga mikono mpaka miguu bado matokeo yamekuwa sifuri ,au hakuna namna ya kufanya sub ?
 
Hakika tumesajili garasa tena garasa haswaaaaa yuko busy na mitindo ya nywele na mambo ambayo si ya msingi kwa club yetu alafu anadanganya kuhusu takwimu zake za mchezo kila siku anatuaminisha anaongeza idadi ya magoli wakati mashabiki tunaona kua hajafunga wala ku-assist sasa nimeamini club ilikurupuka ipo haja ya kutomuongezea mkataba uyu Pogba.
 
Ukweli ni kwamba Pogba mashabiki wengi hatukutak asajiliwe kwenye klabu yetu sema ndo vile figisu figisu nyingi tu wakatumia nguvu zao klabuni kumnunua viongozi wa klabu.Ila tuvumilie staili yake ya uchezaj tu maana hakuna namna sasa.
 
Wakulaumiwa ni Morinyo baada ya kushindwa kumpata mchezaji anayempenda akakurupuka na Pogba! Kumsajili mchezaji siku ya kufunga dirisha matokeo yake ndiyo haya. Kwanza mtamsajili mchezaji ambaye hakuwa kwenye mipango yetu. Halafu mchezaji kama huyu hujifanya yeye wa kiwango cha juu! Ck 2 tu utajua tu huu ni usajili wa bahati mbaya! Bahati mbaya ni bahati mbaya tu!
 
Mi niliomba huyu Pogba tumpe japo miaka miwili cz naamini baada ya miaka hiyo ataleta matunda yaliyotarajiwa. Si mnakumbuka jinsi alivyoikuta Man U ikiwa dhoofu ilhali baada ya uongozi mbaya wa LVG!? Na kwa kitendo cha mleta mada kutumia hela ya usajili wa Pogba kumponda Pogba ni wazi yeye mleta mada na wanaomuunga mkono wamejiandaa kuangukia pua baada ya msimu huu. Hamjiulizi ni kwa nini huyu Pogba ni maarufu sn kwa sasa hadi Forbes wanamwelewa sana na wanaamini haya ni mapito tu,na huyu pogba ana bright future!? Kwa imani yako mleta mada labda ungemtumia Fellaini, ila kwa huyu Pogba naamini wengi tunaamini huko mbeleni atatoa matunda mazuri. Watanzania wanajua,Forbes wanajua na dunia inajua!!
 
Makala fupi nzuri na yakufikirisha zaidi,tujiulize sisi mashabiki ni nani alimsajili pogba?ni shilling ngapi zilitumika? Na je tunauzoefu na usajili wa dirisha dogo?mana huyu kasajiliwa dirisha dogo masaa machache kabla usajili kufungwa !!!

Aiseee,dirisha dogo la usajiri linahusika hapa mkuu,katiba yetu ingekuwa kama ya marekani ingewezekana,huyu Pogba huyu akiendelea kusukuma gozi ataigharimu sana nchi yetu,bora apelekwe hata kwa mkopo huko Majimaji ya Songea akapate uzoefu halafu 2020 tukiona kiwango chake kimeongezeka ndio tunamsajiri rasmi
 
Kwa hiyo Pobga ni foward!!! Uchwara!!!

Mbona tunasikia Pogba anishi maisha mazuri tu huko alipo!! analindwa!! anasindikizwa kwa ving'ora akienda mazoezini!!
Lakini tatizo kubwa la Pogba anajua lugha ya Kifaransa pekee, lakini lugha ya wenyeji wake haifahamu!!!
Amakweli tumeramba garasa!!

Na ndio maana kwenye mazoezi tunasikia anatabia ya kujificha nyuma nyuma!!

Lakushangaza zaidi Pogba anatabia ya KUKURUPUKA alishawahi kwenda mazoezini bila viatu!!
Pogba angefaa asajiliwe na klabu za hata hapa bongo tu!! Simba Ss, Yanga Fc au CHATO FC!!
Pole kwa mashabiki wa Pogba!!

Walidhani TURUFU kumbe GARASA!!
 
Wanajamvi mtakumbuka wakati wa usajili tuliambiwa hii timu yetu sasa inasajili bonge la fowadi anayekuja kumaliza matatizo yote.

Hata kuingia kwake ktk timu alikuja na mbwembwe kibao, Mara kufanya mazoezi ya ghafla klabuni usiku au mchana akiwa na waandishi Wa habari ili mradi ajioneshe tuu kwa mashabiki kuwa anauwezo.

Cha kushangaza ligi ilipoanza ameanza kuja na Masharti kibao klabuni eti ili aonekane kuwa yeye ni mchezaji mzuri kuliko Wa timu pinzani tumtimizie mambo yafuatayo.

1. Mabeki wa timu pinzani wote wafungwe miguu na mikono wawapo uwanjani.

2. Timu yetu iwe inapewa penati kila mechi na marefa ili yeye awe mfungaji bora.

3. Timu pinzani zisiruhusiwe kuleta mashabiki uwanjani.

Sasa wenye Akili hapa klabuni tukaanza kuhoji huyu kweli ni fowadi au garasa?
Mbona fowadi tuliye muacha alikuwa anafunga magoli huku mabeki Wa timu pinzani wakicheza japo tulimuona kama kashuka kiwango?

Tena timu pinzani ziliruhusiwa kwenda kwa ndege helcopta au usafiri wowote kokote hapa nchini kuchukua mashabiki na kuwaleta uwanjani katika mashindano mbali mbali.

Uchumi Wa klabu umeshuka ghafla mashabiki hawana imani naye tena kabisa. Wanajiuliza fowadi gani hawezi cheza mechi za kimataifa anag'ang'ania mechi za mchangani tuu.

Huyu Pogba klabu imepata hasara kubwa Sana kwa kusajili mchezaji bila hata kuangalia uzoefu na historia yake hapa klabuni. Anazua hofu ubabe na kushabikia magoli ya mikono eti yawe halali kwa timu yake tuu.

Hahahaha
Yaani mnashangaza mnapotamka mnataka experience ya kuotea.
Ila mmeumizwa na jamaa kuchukua kiatu cha dhahabu na ukaptain juu
 
Wanajamvi mtakumbuka wakati wa usajili tuliambiwa hii timu yetu sasa inasajili bonge la fowadi anayekuja kumaliza matatizo yote.

Hata kuingia kwake ktk timu alikuja na mbwembwe kibao, Mara kufanya mazoezi ya ghafla klabuni usiku au mchana akiwa na waandishi Wa habari ili mradi ajioneshe tuu kwa mashabiki kuwa anauwezo.

Cha kushangaza ligi ilipoanza ameanza kuja na Masharti kibao klabuni eti ili aonekane kuwa yeye ni mchezaji mzuri kuliko Wa timu pinzani tumtimizie mambo yafuatayo.

1. Mabeki wa timu pinzani wote wafungwe miguu na mikono wawapo uwanjani.

2. Timu yetu iwe inapewa penati kila mechi na marefa ili yeye awe mfungaji bora.

3. Timu pinzani zisiruhusiwe kuleta mashabiki uwanjani.

Sasa wenye Akili hapa klabuni tukaanza kuhoji huyu kweli ni fowadi au garasa?
Mbona fowadi tuliye muacha alikuwa anafunga magoli huku mabeki Wa timu pinzani wakicheza japo tulimuona kama kashuka kiwango?

Tena timu pinzani ziliruhusiwa kwenda kwa ndege helcopta au usafiri wowote kokote hapa nchini kuchukua mashabiki na kuwaleta uwanjani katika mashindano mbali mbali.

Uchumi Wa klabu umeshuka ghafla mashabiki hawana imani naye tena kabisa. Wanajiuliza fowadi gani hawezi cheza mechi za kimataifa anag'ang'ania mechi za mchangani tuu.

Huyu Pogba klabu imepata hasara kubwa Sana kwa kusajili mchezaji bila hata kuangalia uzoefu na historia yake hapa klabuni. Anazua hofu ubabe na kushabikia magoli ya mikono eti yawe halali kwa timu yake tuu.
Hahahaaa u made my day, huyu pogba lol
 
Kweli POGBA amechokwa na wengi..!!
Sasa kocha si aache kumpanga kikosi cha kwanza?..Au mkataba hauruhusu?
Au waajiri wake wamtoe kwa mkopo..
Ila wapenzi wa hii timu anayocheza Pogba wananung'unika tu.. hakuna anayetoa sauti ikasikika,, wakienda uwanjani hata Pogba akicheza rafu wanamshangilia tu..
Hapo ndo nashindwa kuwaelewa hawa mashabiki kabisa.
 
Wa kulaumiwa ni kamati ya usajili
Tangu huko nyuma hakuonekana mfungaji , mkabaji wala mshambuliaji.
Mkizubaa timu inashuka daraja
 
Kweli Pogba ni hasara kama ndo yupo hivo.
Huu uzi umenifurahisha sana tena sana
 
Huwenda timu imerogwa, kila siku malanga na kutumbua wachezaji...haraf kocha ni mkali mno, hadi mafowadi wanashindwa kujipanga sawasawa, akitaka kufunga goli mpaka amwangalie kocha ili apate go ahead ya kufunga. Mashabiki tutakoma...
 
Back
Top Bottom