Huyu Pogba wetu ni hasara tu

Huyu Pogba wetu ni hasara tu

...kuna hadithi nyingi za wapiga dili zitapikwa bila kuiva wala kuliwa, lakini kuna watakaokula mbichi hizo, ila watatapika. Tanzania inayonufaisha wote inasonga mbele wakati wapenda dili zao wakizaa nao kwa dili zao.
 
Pogba sasa hivi ananadi manywele yake meupe huko kongwa na Chemba. Hivi kwa huu upuuzi wake tutapata faida naye?
 
Kwanini apewe miaka miwili wakati ana uzoefu wa ligi? Angekua ni chipukizi tungekuelewa. Lakini uyu alikua kwenye kikosi bora cha FIFA cha msimu uliopita na kacheza mechi nyingi sana za kwenye ligi.
Kamati ya usajili imetuangusha, Pogba hajapiga hata shuti moja kuelekea langoni.......
 
Pogba bado anatuaminisha kuwa yeye ndie mchezaji sahihi wa ile timu yetu na tusihofu tutapata ushindi tu,anasema huu ndio msimu wake wa kwanza toka asajiliwe,tumpe muda
 
Hujauelewa uzi mkuu..tuliza munkari usome vizuri

''Wanajamvi mtakumbuka wakati wa usajili tuliambiwa hii timu yetu sasa inasajili bonge la fowadi anayekuja kumaliza matatizo yote.''

ingekua lugha ya mamtoni nisingeelewa,,,,,
 
Nalaani vikali matumizi mabaya ya jina la mchezaji wangu.!
 
Pogba nasikia anajiapiza kuzinyoosha timu kwa kufunga magoli mengi huku kumbe anatoa kitu kidogo kwa makipa....kama vile 10m ili apewe magoli ya chee
 
Home Of Great Thinker

Jamaa umetumia akili za ziada kuleta huu ujumbe bila kuonekana mchochezi . Pogba nadhani msimu ujao wa League ataachwa au huenda akatolewa hata kwa mkopo timu za mchangani .
 
Pogba anauwa timu mchana kweupe
Lawama za nini wakati mmempa namba siyo yake? Yeye ni defender ninyi mnampanga kuwa striker. Wapi na wapi? Ndio maana mara nyingi akifika golini anapiga mipira nje
 
Back
Top Bottom