Huyu Pogba wetu ni hasara tu

Huyu Pogba wetu ni hasara tu

Wanajamvi mtakumbuka wakati wa usajili tuliambiwa hii timu yetu sasa inasajili bonge la fowadi anayekuja kumaliza matatizo yote.

Hata kuingia kwake ktk timu alikuja na mbwembwe kibao, Mara kufanya mazoezi ya ghafla klabuni usiku au mchana akiwa na waandishi Wa habari ili mradi ajioneshe tuu kwa mashabiki kuwa anauwezo.

Cha kushangaza ligi ilipoanza ameanza kuja na Masharti kibao klabuni eti ili aonekane kuwa yeye ni mchezaji mzuri kuliko Wa timu pinzani tumtimizie mambo yafuatayo.

1. Mabeki wa timu pinzani wote wafungwe miguu na mikono wawapo uwanjani.

2. Timu yetu iwe inapewa penati kila mechi na marefa ili yeye awe mfungaji bora.

3. Timu pinzani zisiruhusiwe kuleta mashabiki uwanjani.

Sasa wenye Akili hapa klabuni tukaanza kuhoji huyu kweli ni fowadi au garasa?
Mbona fowadi tuliye muacha alikuwa anafunga magoli huku mabeki Wa timu pinzani wakicheza japo tulimuona kama kashuka kiwango?

Tena timu pinzani ziliruhusiwa kwenda kwa ndege helcopta au usafiri wowote kokote hapa nchini kuchukua mashabiki na kuwaleta uwanjani katika mashindano mbali mbali.

Uchumi Wa klabu umeshuka ghafla mashabiki hawana imani naye tena kabisa. Wanajiuliza fowadi gani hawezi cheza mechi za kimataifa anag'ang'ania mechi za mchangani tuu.

Huyu Pogba klabu imepata hasara kubwa Sana kwa kusajili mchezaji bila hata kuangalia uzoefu na historia yake hapa klabuni. Anazua hofu ubabe na kushabikia magoli ya mikono eti yawe halali kwa timu yake tuu.
105220719-pogba-sport-large_trans++Kqm9Kg4Q49j1ShszehWsUKVuwW-Pkw5C8lYSsVZynrw.jpg
 
Naweza kufikiri haya siyo makosa ya POGBA, tumlaumu zaidi Aliyemkataa yule mchezaji wa zamani mwenye uzoefu na kumkimbilia POGBA. Mashabiki wote walisikika wakiimba wanaimani na yule mchezaji wa zamani lakini Mkataji aliona HAPANA...POGBA atatufaa tu.

Kila siku Pogba amekuwa na visasi vya ajabu ajabu, anatoa pasi akitaka, anakuondoa hata kwenye team akitaka. anapendekeza nani awe kipa nani au mlinzi wa kati...anachagua team. usipomsifia akifanya madudu uwanjani ujue una hatihati ya kutolewa kwa mkopo..

Kuna yule mchezaji toka jiji mashuhuri ameweza kudumu kwenye number baada ya kuonyesha ushabiki wa makosa ya POGBA uwanjani...

Kelele za mashabiki hazimzuii POGBA kucheza FYONGO... ngoja tusuburi dirisha dogo tumsajili mbadala wa POGBA toka team Pinzani...
 
duh!!!pogba anatuchomesha sana!yan team imepotean kabsa cjui tutumie mfumo gan ili aperfom vingnenevyo mpk mkataba wake unaisha timu itashuka daraja.
 
Pogba kwani si ndo kwanza ana msimu wa kwanza katika mkataba wa miaka mitano!!! Slow slow anatupia magoli ya kushtukiza. Japo inaonekana kama uhaba wa magoli kwa mashabiki umeanza kuwa tatizo kwake na kwa team. Mashabiki wanalia sana kwani toka kikosi kilichopita kilivyokuwa kinasuasua kwenye league nyakati za mwisho, afueni ilipatikana wakati wa mechi za majaribio akitupia magoli na pasi za mwisho matata sana. Ooh! Inawezekana kukosekana kwa first eleven ya uhakika ndo tatizo la Pogba ama yeye kama superstar wa team basi anataka kila mafanikio ya team uwanjani asemwe ni yeye. Nadhani Pogba anatakiwa kupata ushauri wa kimchezo toka kwa viungo nguli maana naona ma-legend kama Scholes na Giggs wamempa ushauri ila anaona yeye ndo yeye.

Labda kama alivyosema mwenyewe ngoja ainyooshe klabu.
Nadhani POGBA ana tatizo sio kama wachezaji wenzake waliowahi kununuliwa kwa bei kubwa. wenzake waliacha mbwembwe . lanini pogba bado anamajisifu na kujiona yeye ndio manyuuu, anabadili mikato na rangi za nywele.

ila najiuliza mbona haitaji ile rangi ya team yake? hivi huyu ni manyuu kweli? Kweli POGBA anatuharibia team,....
 
`bonge la fowadi` Pogba sio fowadi,,, nenda kwa Edo kumwembe akufundishe uchambuzi
Siku nyingine soma Kwanzaa uelewe ndio ujibu leo tupo na Paul pogba kule team coach sizonje hatari hatari
 
Pogba nasikia anajiapiza kuzinyoosha timu kwa kufunga magoli mengi huku kumbe anatoa kitu kidogo kwa makipa....kama vile 10m ili apewe magoli ya chee
ETI APIGE PENATI BILA KIPA KUWEPO!
 
Siku nyingine soma Kwanzaa uelewe ndio ujibu leo tupo na Paul pogba kule team coach sizonje hatari hatari
Qwi Qwi Qwi.... Huyu jamaa ni Div V kabisa!! Eti nenda kwa Edo Kumwembe akuelezee kuhusu Pogba wa Man U!!! Fasihi kidogo tu inamshinda?
 
Tatizo yeye ni ni kiungo....

Wakati huo anataka kuwa forward.....


Wakati huo anataka kuwa beki........

Sometime anataka awe Goalkeeper...
Mtu mmoja huyo huyo? Kwa mechi moja ama mechi anuwai?
 
HAMNA POGBA YUKO FRESH TU SEMA WABONGO TUNABEBEWA SANA AKILI ZETU NA TUNATUMIKA KWA KUDANGANYWA NA MAKOCHA WA TIMU PINZANI KAMA HATUKO TIMAMU. KWA KIFUPI MAKOCHA NA VIONGOZI WA TIMU PINZANI WAMESHINDWA KUFUNDISHA NA KUENDESHA SOKA LA UKWELI,WAMEBAKI KUFANYA POROJO TU WANAPOKUWA HUKO CNN,SKY NEWS,BBC NK! ILA POGBA KIWANGO BADO KIPO CHA KUELEWEKA TU. HALAFU YATUPASA TUMPE JAPO HATA MIAKA MIWILI HUYU POGBA!!
Na Baadae mtasema miaka miwili ni michache sana kama awali mlivyo sema Siku mia ni chache.
Pogba ameishiwa mbinu kila siku ni ugomvi na wachezaji wenzie. Na mbaya zaidi ni kwamba Kila akikutana Na washabiki anaomba Wamuombee hirizi yake ili iwe na nguvu zaidi!!
 
Nasikia pogba analalamika hakujua kama hii kazi ya uchezaji ni ngumu,ange-sign mkataba wa miaka miwili tu na siyo mitano
Kila Mtu Man U anatamani Van Persie asingeuzwa. Van Persie alikua mtu wa majeraha ila alikua akifunga Magoli na hasa magoli Muhimu.
 
Kama wanaompa taarifa wanamdanganya, akipita hapa anaweza kuona wahariri na wanahabari wanamsaidia aelewe hali ya kitaa. Mkulu aliwaomba wahariri na wanahabari waisadie serikali. Hiyo taarifa sikuitayarisha, nimeiwasilisha tu kama ilivyoripotiwa.

Ingawaje viongozi wanajitahidi kutushawishi kwamba uchumi unakua, unapaa lakini hali ya maisha ya kitaa inaonesha kama uchumi umepiga stop. Uchumi gani wa kukusanya mapato tu? (kuwakamua walalahoi). Haya sasa mambo ndio hayo, mfalme amevaa joho linalompendeza sana.
Mtoto ametokea kum-save mfalme ili asitembee bila nguo.

Kwa kweli waandishi na wanahabari wanatakiwa kwenda kitaa kuwahoji wananchi live!
Acha Uchochezi bana!! Sisi tunamzungumzia Pogba na Man U. Qwi Qwi Qwi...
 
Pogba wa KAUZU FC AU HUYU NINAYEMFAHAMU???

Isee Unataka Pogba apige Chenga uwanja mzima nini kwani anacheza mwenyewe?

Pogba-Herrera-Matta goal

Mtoto anaweza kuongoza mtihani kwa wastani wa 20% jiulize hilo darasa likoje?

POGBA halisi hana shida labda pogba wa Kauzu fc
Teh teh teh.... huu uzi umewapiga Chenga watu wengi sana, hasa wale wasomaji wa magazeti ya Ijumaa na kiu bila kuwasahau waangaliaji wa Bongo Muvie.
 
Pogba bana alivyo kuja alisema Man U ya Pogba itakua Man U ya magoli yaani atafunga magoli akiwa kwenye kona yoyote uwanjani. Sasa Msimu umeisha hatuoni magoli!! Mbaya zaidi mpambe wake anasema Pogba kashafunga Magoli 3800, sasa sijui alikua ajiyafunga akiwa mazoezinii au alikua akiyafungia bafuni!? Qwi Qwi Qwi
 
Ndo kwanza dakika ya 20 kipindi cha kwanza Pogba kakata moto.....pumzi ndogo route ndefu
 
ah pogbaaaaaa...
pogba nasikia amekuwa mnyang'anyi mtaani,eti mali za washabiki wake zote zinapaswa azimiliki yeye...
na ukitaka kumjua pogba vizuri mwambie hujui kucheza mpira...
hapo mechi utazisikia ukiwa gerezani...
pogbaaaaaaaaaaaaa...
akijibu hoja jiandae kushangaa kwamba ni msomi au kila.za wa mpira.


Hongera mkuu unatisha kwakweli
 
Back
Top Bottom