Mimi lawama zangu za kwanza ni kwa Fugason ambaye kwa ubabe wake hujifanya muamuzi wa masuala nyeti ya Nchi. Mara Katiba pendekezwa ya FIFA kaivuruga, mara kaingilia matokeo ya uchaguzi mkuu wa Scotland. Nasikia alimpigia sana chapuo huyu Pogba na kudiriki kuwatukana timu pinzani kuwa malof. Nahisi ndiye aliyeshinikiza asajiliwe pamoja na kwamba Morhinyo alikuwa anamtaka yule mwingine aliyekuwa rafiki wa mtawala Libya.
Hoja yangu kubwa ni kwamba sasa niwakati wa timu zote za Premier Leage kushinikiza FIFA ibadili taratibu zake hasa utaratibu mzima wa usajili, kuanzia kuandikisha mashabiki, hadi kusajili. Wadai kamati huru isiyoingiliwa. Lakini pia taratibu za kupata marefa na ma raise men ili kuhakikisha akina Pogba hawaingilii katika kutekeleza wajibu wao. Hivi sasa Poga ana uwezo wa kuteua refa, juzi akateua raise woman kaenda kuwa kinara wa ma raise men. Yaani hata Kocha wa Asernal akiwa na swali kwa kocha wa Man U, utaona raise woman ananyoosha kibendera kuwa hilo si swali. Katika mazingira kama haya usitegemee timu kama Man city, Chelsie, Liverpol Asernal zitaweza cheza mpira, achana na kufunga goli hata la mkono!
Kuhusu mapato, nasikia baada ya kukusanya madeni ya mauzo ya jezi zilizouzwa china na kwingineko kabla Pogba haja sajiliwa, sasa hivi hakuna mauzo mapya kabisa. Timu iko hoi, mashabiki hoi na raia woote wa England hoi.
Kibaya zaidi, Ikitokea mchezaji wa timu pinzani akaota ndoto kuwa kwa utendaji huu Pogba anaweza asimalize mkataba wake, sasa hivi anashauriwa akae kimya na ndoto yake. Akijaribu tu kumsimulia rafiki yake kuhusu ndoto hiyo, asahau kuonekana katika viwanja, ataishia Gwantanamo!, Kweli nawaambia!