mkuyuga na kiruma,
Mimi huwa msomaji mara nyngi na si aghalabu nikachangia mada na wala sikutaka kuchangia mada hii. Lakini ninaona waziwazi kuwa yanaletwa mabo ya kutugawa na anayefanya hivyo si Jizalendo bali ni huyu huyu Mkuyuga na kundi lake. Ninaona wale wanaotahadharisha udini ndio wao wao waliojaa udini na ukweli unaposemwa basi njia ya kukimbilia ni kudai udini na kutaadharisha watu eti tuwe macho na mtu fulani atatuchanganya, na hao wengine eti tunashangilia "tahadhari" hizi ambazo inaonekana wazi yeye yule anayezitowa ndiye anayenuka udini. Hatukugawanywa na upendeleo wa dhahiri wanaopewa baadhi ya taasisi za dini na kunyimwa nyingine tutagawanywa kwa hizi mada ambazo ni za kuweka vitu wazi na ambazo zinatakiwa zitowe ukweli, ziepuke dhana na kashfa zisizokuwa na ushahidi hata chembe.
Kwanini tuogope kusema ukweli. Mwalim Nyerere ni BABA WA TAIFA LA TANZANIA, hiyo ni hadhi aliyonayo ambayo anyang'anyiki kwa sababu zilzo wazi - alijitowa muanga na kutojali mshahara wa ualimu aliolipwa na wakoloni katika jitihada za kutukomboa. Alikuwa mwanaharakati kutetea wanyonge na pia kuikomboa Afrika na mimi ninamueshimu sana kwa hadhi aliyotuletea taifa letu. Aliplay his part pamoja na ufanisi na makosa.
Mzee Mwinyi naye vivyo hivyo aliplay part yake kadri awezavyo na katika kufanya hivyo alijaribu kurekebisha makosa ya Mwalim na kudumisha mazuri yake, na pia alifanya makosa yake. Bali kuna makosa ambayo ni magumu kuyarekebisha na inakuwa siuungwana kumpambikizia makosa hayo wakati tunajuwa chanzo chake alikuwa ni Mwalim Nyerere. Pia si uungwana kumkebei mmoja na kumsifu mwengine kwa misingi ambayo mtu anaijuwa mwenyewe. Hapa tunaangalia pande zote.
Sasa tuchambuwe haya malawama ambayo Mkuyuga anampambikiza nayo Mzee Mwinyi kijumlajumla bila ya ushahidi wala muelekeo:
1. Kuanguka kwa shillingi ya Tanzania:
Shillingi ya Tanzania ilianza kuanguka tangu miaka ya sabini na kufikia mwaka 1975 tayari ilikuwa ni sawa na senti 50 za kenya nakaribu Tsh 15 kwa US$1. Kutoka hapo ikachukuwa plunge za ajabu ukilinganisha na US$ mara 22, mara 35 mara 45, mara 60 na ikapiga mbio hadi shillingi 120 na ikawa inabebwa kwa makapu tayari ingawa makapu hayo yalibidi yafichwe sana. Mwaka 1984 Edward Sokoine akaleta jambajamba na makapu ya shillingi yakafurika kutupwa kama njugu na ole wako kama ungechelewa kuyatupa yako. Na wakati wote huu Mwinyi hakuwa Raisi wa Tanzania. Tangu Mwinyi aondoke madarakani shilligi ndio imedidimia ile mbaya kiasi ambacho kama hapo nyuma iliitaji makapu metaphorically (and I hope that is what you meant) sasa hivi inahitaji magunia. Hivyo si Mwinyi wakulaumiwa kwa kuanguka shillingi, wakulaumiwa ni yule aliyeifanya ikaanza safari hiyo na si mwengine bali Mwalim Julius Kambarage Nyerere.
2. Rushwa:
Tulipopata uhuru neno rushwa halikujulikana lakini siasa za Mwalim Nyerere nazo zikatuletea hili. Baada ya kupata shida za kuishi alizozisasababisha Mwalim kwa tutaifisha kila kitu kikubwa bila ya kujali mwenye kitu hicho alikipataje na kuwalipa watu mishahara peanuts kiasi ya kutokumudu kujipatia chakula, wabongo wakagundua njia za kujikimwi njaa kwa kupokea hongo, na hongo vilipowapunguzia njaa wakagundua kuwa kumbe wanaweza kujipatia mapesa for doing nothing, hivyo wakaanza kudai rushwa. Matokeo yake tunayavuna leo, rushwa babu kubwa imekita mizizi kila mahali na ambayo imekuwa inakuwa out of proportion hadi kufikia akina Nkapa kuuza nchi pamoja na taasisi zile zile vilivyotaifishwa kwa wageni kwa njia ambazo zinaashiria rushwa. Leo hii rushwa ni adui mkubwa wa maendeleo yetu. Ni nani alipanda mizizi ya rushwa hiyo - Jibu Mwalim Julius Kambarage Nyerere. Mwinyi, Mkapa na Kikwete wao wameikuta tu wapigane nayo na kupachikwa malawama wakati muanzilishi wake anasifiwa.
3. Ujambazi:
Maisha duni yalifanya watu wajiingize kwenye wizi na ubadhirifu ambavyo sasa hivi vinachangamshwa na utandawazi. Dunia nzima sasa hivi ina wauza madawa ya kulevya na ni vipi mtandao wa dunia apambikizwe nao mtu mmoja vinashangaza. Kwa mara ya kwanza ujambazi wa kutumia silaha hapa nchini ulitendeka kwenye Barclays Bank tawi la Market, Tanga mwaka 1969 ambapo shilingi laki tano zililambwa na majambazi yaliyokimbilia kwenye misitu ya kuelekea Kenya. Sehemu kubwa ya jeshi lilipelekwa huko kuwasaka na sidhani kama waalipatikan. Kwa hiyo ujambazi nao ulianza zamani. Na wakati huo vijana wengi tu walizamia melini nje ingawa hali haikuwa harsh kama sasa. Ubaharia ulihesabiwa kama kazi yenye kulipa sana.
Ni nini hasa lilikuwa tatizo la Baba wa Taifa? Huyu mzee hakuwa original katika mambo yake mengi kwa hiyo alikuwa anaigaiga mambo tu kwa kucharuka na akishaiga conviction yake haiteteruki.
a) Mfumo wake wa siasa na uchumi ni muigo wa China.
Hili ni kuanzia Arusha Declaration lenyewe, kutaifisha mali za watu, kuanzisha vijiji vya ujamaa, mfumo wa nyumba kumi kumi, jinsi alivyovaa nguo zake na hata vile alivyotaka tugutiane. Yeye alikuwa "Mwalim" kama vile Mao alivyokuwa "Mwenyekiti" na wengine wote tulikuwa "ndugu" kama vile Wachina wote walivyokuwa "comrades". Alijaribu kulable kuiga huko eti ni African Socialism lakini hamkuwa na uafrika hata chembe humo. Waafika ni socialists bali sio kwa mtazamo wke yeye. Muafrika alithamini kuwa na kitu chake mwenyewe iwe shamba, iwe nyumba ambavyo aliviudumia kwa jasho lake bali hakusita kushare matunda ya vitu hivyo na jamaa zake na hata wageni. Ndio maana hapo zamani ungeweza kuchuma ndizi kwenye shamba la mtu ukala bila ya kuulizwa neno. Cha msingi ni kuwa walitaka ijulikane kuwa vitu hivyo ni vyao. Chini ya Mwalim walinyang'anywa fahari hii kwa kupambikizwa mashamba ya vijiji ya pamoja yasiyojulikana mwenyewe hasa ni nani.
b) Umoja na ukombozi wa Afrika
Hii nayo ilikuwa ni adhima ya Kwame Nkrumah ambaye Waghana walimshtukia akapinduliwa. Kuanzia hapo Mwalim akalivalia njuga.
Bali si hivyo tu yeye hakuwa na itikadi inayoeleweka kwani WaBiafra walipotaka kujitenga kutoka Federation ya Nigeria yeye aliwaunga mkono!! Ieleweke kuwa karibu Biafra yote ni Wakristo kisha Waroman Catholic. Je dini ilikuwa ni kigezo hapa? Hata hivyo Nigeria ni moja hadi leo!!
c) Mwalim alikuwa fundi wa kuiga kwa kutafsiri kazi za wengine, hasa zile za William Shakespear. - i) Mabepari wa Venisi, ii) Julius Caesar.
Swali ni kuwa ni mangapi mengine ambayo Mwalim alikuwa akiigaiga tu. Na nini zimekuwa athari zake kwetu?
Haya niliyoyataja bayana hapo juu kuhusu Mwalim sio dhana ni mambo factual bali haya yenu ya Mzee Rukhsa ninaona ni hatihati tupu ambazo ni wazi zina udini ndani.
Quote:
Originally Posted by mkuyuga
Jizalendo, tunamshuru saaaaaaaana mzee mwinyi kwa kuletea unga ambao umesaidia sana vijana wetu kufaika na huo uchumi wake!!
kuna vijana wetu wamefungwa Pakstani, wengine greece, Italy etc,
Ametutengezea alikaida ndiyo maana vijana wetu kama kufungwa huko marekani.
wakati wake wapasitani walizunguka nchi nzima wakihubiri dini!!
Wakati wa mwinyi alikuza saaaaaaaaana uchumi hadi watu wakawa wanabeba hela kwenye magunia!!
Uchumi wake ulikuwa sana akawa na maduka ya vito arabuni, je unjua kwa nini bodyguard wake alikufa huko arabuni?
Hongera mwinyi kukuza uchumi wa tanzania, hadi wanya wetu sasa wanauzwa nje, pia tausi walipewa kwa maswahiba wake(ref, bungeni).
ngoja niishie hapa sitabishana tena na wewe maana wewe unaoneka unataka kuvuruga umoja wetu humu kwa kugawa watu katika makundi ya dini!
wanabodi kuweni makini na huyu mtu.!
kiruma said:
ManjiMakuti, Kwani hujui,
kuwa wakati huo ndiyo madawa ya kulevya na unga vilianzA kujitokeza?
Mbona mengi aliyosema Mkuyuga yako wazi?
Ni ni ambacho unakibishia kwa mfano?
(1) Loliondo unaijua?
(2) Hujui wakatyi wa mwinyoi hela zilikuwa za kumwaga mifukoni? layman akiona hivyo basi uchumi safi sana!
etc.