Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Zanaki,

Yes we are. Jk hajafikia huko. He is still gud prez.

FD
 
Mtaona huyo askofu anaambiwa anyamaze? miye natakia kusikia Mufti au Shehe fulani anasema nini?
 
Fikaraduni, nakubaliana nawe pamoja na Zanaki, JK na Idd Amin Dada, ni vitu viwili visivyofananashika! Lakini sikubaliani nawe kuwa 'he is till gud prez'. He wasn't, he still isn't and I'm not sure if he will ever be! Of course, yote ni maoni tu!
 
Mwanakijiji: Kama ambavyo hatukusikia Pengo akimkemea Mkapa katika utawala wake, hutasikia mufti au sheikh yeyote akinyanyua mdomo wake dhidi ya JK. Tutashuhudia maaskofu wengi wakimshukia JK kadri siku zinavyokwenda kama walivyofanya kwa Mwinyi! At the end of the day, viongozi wengi wa dini wamekaa kiainaaina sana!
 
Damn! I am lost,

yaani Butiku anatokea wapi tena? Butiku na foundation yake walikuwa wakipewa shillingi millioni 300, na Mkapa kila baada ya miezi sita, hela za walipa kodi! Butiku akaanza njama za ktaka kumpitisha Salim kwa kum-blackmail na kumu-intimidate Mkapa, akaenda mikoani kuanzisha ziara ya kuwasikiliza wananchi, akafanya vikao vya public na kuwaita wananchi waanze kuitukana serikali, akaita na waandishi kibao, alipooona Mkapa hashituki,

Yeye na Salim, wakaamua kwa makusudi kufanyia sherehe za kumuadhimisha Mwalimu, kwa kumuomba M7 awafanyie kwenye bunge la Uganda, wakaenda wakafanyia kule, ndipo kwa mara ya kwanza JM akamfuata, Mkapa na kumpa darasa kuhusu Butiku na mipango yake, Mkapa akakata msaada wa miillioni 300 ukawa hakuna tena?

Waliporudi Uganda wakaanza kampeni za chini chini za urais wa Salim, wakamuita Mzee Ndejembi na kumpa gari ya aina double cabin ili aanza kuzunguka mikoani kumfanyia kampeni, but, at the same token huyu mzee naye alikuwa njiani kugombea tena uenyekiti wa CCM wa mkoa wa Dodoma, ambako JM tayari alikuwa ameshamtayarisha mtu wake, Masima.

Mkapa akasikia kuhusu Ndejembi na kupewa gari na Butiku/Salim, akamtuma mwenyekiti wa CCM Tabora, aende Dodoma na kumpa ujumbe Ndejembi, kwamba "........aache mara moja hizo kampeni zake, maana Mwarabu hatakuja kuiongoza Tanzania........", Mtandao wakaona opportunity, Rostam akampa Mzee Ndajembi, shillingi millioni 10 kwa ajili ya kampeni zake Dodoma za uenyekiti wa CCM, kwa sababu Rostam alijua kuwa JM hana hela za kutosha kumpa mgombea wake, Ndejembi akamshinda mgombea wa JM lakini kwa taabu sana. Huyu mzee akaendelea kumfanyia kampeni Salim anyway, ndipo Rostam akaanza kumtumia wajumbe kwamba arudishe hela zake yeye alikuwa amemkopesha tu, au aache kampeni za Salim. Huyu Mzee akabidi aache kampeni maana hakuwa na hela za kurudisha.

Warioba naye akajiunga na hizi kampeni za Butiku for Salim, ndipo Mkapa akaamua kuwapiga marufuku Ikulu wote wawili, na hata kuonana nao tena mpaka leo hajawahi. Kufika Dodoma Jm akatolewa kwanza mapema na Mkapa, kwa hiyo Warioba na Butiku wakaenda kwa Jm, na kumuomba awasaidie ili wajumbe wake wahamie kwa Salim, Jm akawatukana sana kwamba nyinyi si ndio mlikuwa mnamfurahia Mwalimu alipokuwa akinipiga vita, akakataa kuwasaidia, pamoja na kwamba aliwadanganya atawasaidia, kwa sababu Muuungwana alishawawahi usiku akaonana na Jm na wakaelewana.

Matokeo Muungwana akashinda, Butiku akaondoka na hasira isyokuwa na kifani akamuandikia barua Mkapa na kuwapa copy wajumbe wote wa kamati kuuu, na wenyekiti wa CCM wa mikoa yote, ya kumtukana Mkapa kwa kumpitisha Muungwana, na akataja mpaka kiasi cha hela alizopewa na Muungwana, yaani dola millioni moja na kwamba CCM is dead sivyo kama Mwalimua alivyomuachia, akajaribu kuwa mjanja kwa kumalaumu kutompitisha Jm, badala ya mgombea wake Salim, Warioba kuona mambo yameharibika, naye akawa mjanja, akatukana tukana alip[oona no body is paying attention akajingiza kwenye kampeni ya mtandao dakika za mwisho, MFN ikaachwa ndio mwisho wake kabisaaaa. Sasa since then maisha yamekuwa magumu sana kwa Mzee Butiku, na foundation kwa ujumla.

Sasa with all that said, ninasema kwamba hiii njaa ya bongo itatufikisha mahali tutaanza kulana wenyewe kwa wenyewe, kama mbwa mwitu, no question kwamba huyu Mzee sasa anakuwa motivated na njaaa kali, tena sana, maana hela hana, kama kuna alizochukua kwenye zile enzi zilishaisha maana jamaa ni mjinga sana kwa kinamama, ninajua kuwa ana njaa maana sasa ni karibu mwaka mmoja na nusu hajatoka nje ya nchi kama ilivyokuwa zamani. Barua aliyomuandikia Mkapa ya kumtukana it was a good thing, lakini viongozi wengi nilipowauliza maoni yao, walisema barua should never had came from him, maana hana record nzuri au sio msafi, na mfano mzuri ni jinsi alivyoshirikiana na Nyakyoma, kula Gapex yote mpaka chini.

Butiku, anahitaji kurudi kijijini na kukubali kwamba maisha ya mjini hayawezi, maana sasa anaanza kuwa kichekesho, leo Tanzania hakuna mtu yoyote aliye-serious na rushwa maana inawajumuisha karbu viongozi wote wa nji, na Butiku anapaswa kuwa mtu wa mwisho duniani kuzungumzia rushwa, sheria zilikuwepo siku zote za kuzuia rushwa kuna mpaka tume ya kuzuia rushwa, je haikuwa na sheria? Kwa nini viongozi wa bongo wanapenda kuwachezea wananchi kila wakati na PR za kitoto? Butiku anaongelea nini? Alipokuwa Ikulu kilichomshinda kukomesha rushwa ni nini? Eti rais ameonyesha kusikitishwa na rushwa wakati wa uchaguzi, uchaguzi upi huo? Kwani yeye aliiingiaje kwenye power? Sasa Butiku amesahau zile dola millioni moja? Na mahela yote aliyokuwa akipewa Mzee anayemiliki Ngurudoto kunakofanyia mikutano yote ya serikali, kutengeneza fulana na kofia zilitoka wapi? Hela za kuwapa kina Darwesh na magari mawili mapya kuzunguka bongo nzima kumpaka Salim zilitoka wapi? Mzee Butiku, huu mji una wenyewe ndugu yangu, basi imetosha rudi kijijini maisha ya kuruka kwenye ndege yalishaisha, madaraka ulikuwa nayo for 28 years, sasa leo ni kitu gani tena ambacho hukukifanya then, aibuuu mtu mzima, wewe ni kurudi tu kijijini na kukubali yaishe na ninajua kuwa mtandao sio wajinga hawatakupa kitu, maana wao wenyewe bado wanatafutana vyeo havitoshi.

Jamani huyu mzee ni njaaa tu inamsumbua! Nyie kina Zanaki hebu mwambieni huyu mzee kuwa Mang'ana Gasalikilire, amnga'ang'anie Mama Kamba ili amlishe na ajifunze kuacha kupora wake za watu, ila cheo hamna tena!
 
Mzee ES,Maneno yako makubwa yana mguso mzito,cha maana na msingi ni kumwambia Mzee mzima Butiku arudi Musoma kwani enzi zake zimekwisha! Ndugu Zanaki naomba ufafanuzi nani huyo amepewa tender na watu wa MNF ni Gunini,Mayenga au Liku?kwani hao ndio watoto wa Mama Kamba,ambao Baba yao alipelekwa Brussels ili Mzee Butiku apate muda na huyo mama!Oooh wazee wetu wana mambo machafu ambayo hayawezi kusemeka.Kwa mtazamo wangu "kiongozi mzuri ni yule anayejali familia yake"lakini kwetu ni versi versa kwani kiongozi mzuri ni yule mjuzi kwa wanawake!.
 
Mzee ES, kwa mara nyingine tena, umekuja na maneno mazito.. ndo maana hawaupendi huu mtandao!!! Kijiwe kiko bomba!!!!
 
Kama ilivyo kwa mada nyingi, sina cha kuongea hapa. Lakini walao safari hii napenda tu kusema wazee mmewiva.....hii forum idumu. Natamani kama kila mtanzania mwenye umri wa kupiga au kupigiwa kura angekuwa na nafasi ya kusoma mambo yanayojadiliwa humu.
 
Shukrani, ninajaribu kutoa my best kabla sijaaaga rasmi, na ndio hasa kilichonipa unga zaid kwa sababu wazito walikuwa wanalia kila siku kwamba hii forum ifutwe lakini mzito mmoja alikuwa anakataa kwa kufkiri nitamsamehe,

Sasa yamemshinda, but, kijiwe lazima kendelee na watakuja wakali zaidi siku zijazo kuungana na wakali alioko sasa hapa, leo bongo kuna habari ya Rich-Monduli yaani magazeti yamechacha mot ile mbaya, leo pia nilishuhudia mahojiano ya waandishi na mzito Jm, yaani maswali yote ya kuhusu Rich-Monduli wameyatoa hapa yaani I could not be more proud ya hiki kijiwe, nilipowauliza wale waandishi wakaniambia huwa wanashinda hapa!

Kwa wana forum wote, ndugu zangu kuna mzito ameniomba nimpatie all the facts za Rich-Monduli kutoka hapa, ili alinganishe na zile alizonazo, anasema sasa ameamua kulivalia njuga, kwa wazee wangu nitashukuru kama kuna asiyejali kunitumia kwenye PM au mtuwameli@yahoo.com, ninajua mengi yameandikwa hapa lakini ninataka kuzikusanya nimfanyie faili kamili kwa hiyo ninarudia kuwa nitashukuru sana kwa wazee wote tukishirikiana, siwezi tu kumsema hapa lakini sina tatizo kumseam ni nani pembeni, shukrani wazee kwa yeyote mwenye hiii habari please, na hasa wazee wa Texas na wote huko majuuu!

Shukrani!
 
Mzee Es

Shukrani kwa taarifa hiyo. Unajua topic hapa zimechanganywa sana kama hii ya Rich-monduli kuna facts kule kwenye kabrasha la hii topic vilevile na jana kuna mtu aliuliza kuhusu bei za majenerator na hiyo topic iliunganishwa na ile ya WHO TWISTED CRDB ETC NA IPO NYINGINE TENA YA HUU UMEME KWENYE KABRASHA.

Kwa hiyo una kazi kubwa ya kusaka details, lakini kama unakumbuka ulichangia nini kwenye hiyo topic – ukienda kwenye topics zako halafu unascan one by one, I know it's a tedious job lakini its worth it. Hawa jamaa ni lazima waache wizi hawaoni aibu wanakuja majuu wanaona mabo mazuri halafu wanawakumbatia wezi very disgusting.

HILI LINANIPA MOYO KUENDELEA KUWAPIGA MAWE HAWA VIBAKA.
 
Jasusi.
nimekukubali kwa mara ya kwanza umeonyesha uzalendo zaidi kuliko.....

keep it up!

Mwanakijiji/mwanasiasa.

masheikh hawana maneno hata siku moja kwani Nyerere alikuwa muislam?mbona masheikh hawakumtukana?
Ila nongwa iko huko soon tutaona barua za kichungaji kwa JK.
 
Mwanasiasa,

Jamani ebu twendeni mbele turudi nyuma. Nakuombeni mnipe machache ambayo mlitaka kuyaona akiyafanyia kazi ktk Kipindi hicho cha mwaka! Na hasa itakuwa vizuri mkinambia kama Chadema wangeweza kufanya yapi ktk kipindi cha mwaka mmoja na kwa mbinu zipi?... To talk is very cheap siku zote tusiwe na madai bila kuwa na ushahidi kuwa ingewezekana kabisa ktk kipindi hiki kiongozi fulani kuyafanya haya na haya.

Pili, JK ni sawa na mume wa nyumba. Kutoka kwake nje sidhani kama ni makosa kwani hakuna mwanamke ama mtoto anayetaka baba anayekaa ndani tuuu eti anaangalia matatizo ya nyumba!.. A father has to go out! atafute kazi, akutane na watu na mitikasi na mengine mengi. Naweza kukubali tu kwamba ktk ziara zake nyingi hatujaweza kuona la maana zaidi ya hizo hadithi lakini je, Kuna mmoja kati yetu anayefahamu mikataba aliyoweza kuitimiza huko nje?
What if, mikataba mingi ni ujenzi ambao matunda yake hatuwezi kuyaona ila baada ya miaka mitano ijayo?...
Malalamiko mengi humu ni kumtaka JK abadilishe mikataba ya Mkapa!...
Kama mlisoma mahojiano ya Mkapa kuna kipengele alichosema yeye Mkapa kuwa mikataba yote waliyowapa wawekeshaji (migodi) ni ya UHAKIKA - sealed yaani haiwezi kupindwa hadi mwisho wa mradi mzima (miaka 10-15). What can JK change?
Msinielewe vibaya ila nataka kujua upande wa pili wa shilingi hii!... lawama bila kuzitaja dawa sidhani kama ni uganga mzuri!
 
Mzee ES,
kabla hujaondoka tunaomba utuletee barua aliyoandika Butiku kwa kamati kuu ya ccm. tulikuomba toka tulipokuwa BCS times kabla mtandao haujakorofisha.
 
Malalamiko mengi humu ni kumtaka JK abadilishe mikataba ya Mkapa!...
Kama mlisoma mahojiano ya Mkapa kuna kipengele alichosema yeye Mkapa kuwa mikataba yote waliyowapa wawekeshaji (migodi) ni ya UHAKIKA - sealed yaani haiwezi kupindwa hadi mwisho wa mradi mzima (miaka 10-15). What can JK change?



Kama hivyo ni kweli kwa nini kwenye mikataba kunakuwepo na kitu kinachoitwa arbitration?

Kuna mikataba ya aina nyingi tu – tusijifunge kamba hapa – kuna kitu kinachoitwa unfair contract?

Vile vile JK alisema cha kwanza ni kuhakikisha mikataba inapitiwa upya:
Unamaanisha JK alikuwa hajui alichokuwa anakisema?

Kwa nini inachukua muda mrefu? Huoni hapa kuna kitu au mchezo unafanyika ambao wabongo tunafichwa ukweli?

Je ni vipi Edward Richmonduli anawanyamazisha wabunge kuuliza Kulikoni kuhusu umeme kama hivyo unavyodai ndivyo? huoni hapa tayari kampuni ya umeme ya Richmond ambayo imeuzwa ili kupoteza ushahidi?

Watu ni lazima wachukuliwe hatua ili tuweze kuelewa nini kinaendelea. Tanzania itakuwa ni nchi ya kwanza ulimwenguni kutokusitisha mikataba bomu na waliohusika kutochukuliwa hatua za kisheria.
 
Mkandara,
huyu JK ndiye aliyetoa kwa waandishi wa habari gharama za ziara ya Sumaye alipotembelea marekani. Waandishi tulimlaumu sana Sumaye, na kuziba masikio kwamba ni JK kama waziri wa mambo ya nje aliyeandaa ziara hiyo.

Kwanini leo hii JK hatuelezi gharama za safari anazofanya nje? Kuna ulazima gani wa Raisi, na Waziri Mkuu, kufanya ziara NNE Marekani na Canada ndani ya muda wa miezi 6?

USANII UMEZIDI!!!.....Kwenye hotuba yake ndani ya Bunge JK alihoji kuhusu vigogo kutibiwa nje kwa ugonjwa mdogo hata mafua. Baadaye JK akajidai anakerwa sana na hali ya hospitali ya muhimbili. waandishi wa habari tukamsifia sana kwa kutembelea hospitali ya muhimbili.

baada ya mwezi mmoja JK akaenda Ujerumani kuangalia afya yake. mpaka leo hakuna mabadiliko yoyote muhimbili.

watanzania tujifunze kwamba nchi yetu ni changa mno, na tuwe makini sana tunapochagua viongozi, haswa raisi. uchumi unadidimia kwa kasi ya kutisha.
 
Mzee Dua,

Nimekusikia, je kuna ufundi wowote kwa wenye kujua ambao unaweza kunifanya nizipate posting zote kwa mara moja, au inabidi nianze kupitia mada moja moja?

Kama kuna anyejua ufundi huo nitashukuru akinimegea maana hii issue sasa ni moto mkali huku bongo, sasa ni wakubwa wengi wanataka info!

Mzee Joka,

Nilishaonywa huko nyuma kuwa hiyo barua ni nyara ya serikali, adhabu yake ni kuanzia miezi sita jela kama alivyofanywa ndugu yangu Balinagwe kule Songea, walimfunga kama mchezo na habari kama hiii.

Ila finally, killio kimesikika yaani sasa bongo ni Rich-Monduli tuuu, kila mtu anataka kujua what happened?

Shukrani
 
Dua,

Hapa kumbuka najaribu kuangalia upande wa pili wa hii shilingi na kati ya haya nayoyasema nimejaribu kuyatazama kwa undani ili tusije fanya makosa ya Kulaumu bila kuonyesha kitu tunacholaumu.

MIKATABA:- Umezungumzia Arbitration...nadhani JK kesha fanya hiyo na hao Barricks! jambo ambalo wengi hatuweza kulikubali ni kile tulichopewa!.. ongezeko la dau kidogo hali hakuna mahesabu!..
Tumetaka zaidi lakini haikuwezekana kwa sababu tulisha jifunga na hiyo 3%. Swala la hisa ni nje ya mjadala kabisa labda JK akubali kupindua mikataba! Labda nikuwekee upya maneno ya Mkapa mwenyewe kuhusu hii mikataba
Alisema hivi:- BENJAMIN MKAPA: we have assured [potential foreign investors] that we will not put any unfair restrictions upon them at all. It's all legislated for, and in some sectors there's even special legislation. For instance, we had a particular legislative and tax regime for the mining sector, and they've been able to come in quite confident that they are secure for the life of their mines, which is anything between 15 and 20 years.
Sasa mshikaji wewe unaweza kupindua wapi? esp pale kwenye special lagislation mbovu kama hizo?
Trust me, sidhani kama kuna Mtanzania ambaye yupo tayari kumtetea JK pindi ikitokea hali ya Zimbabwe!.. That is a Fact na tumeyaona kwa Wazimbabwe wenyewe ambao walipiga makelele kwa mikaa zaidi ya ishirini. Mugabe akawaambia tusubiri hadi mwisho wa ahadi ya Waingereza kisha tutaidai ardhi yetu kwa nguvu kwani kisheria hawawezi kutufunga. Well, Mugabe kayafanya aliyowaahidi leo hii wanamlaumu kwa kila kitu. Sheria ile ile aliyoiogopa kwa miaka ishirini pia imepindishwa aonekane yeye mkosa!

Jokakuu,
Umesema JK kaenda US na Canada mara nne..haya maneno kweli au unahesabu kichina? -(Utani)
JK kaenda US mara moja ya pili ni kwa sababu ya mkutano wa UN hiyo ni lazima siwezi kuhesabu kama ziara. Kifupi hadi leo hajafanya ziara rasmi ya kumwona Bush, ile ya kwanza ni kutuuza, hali ambayo wengi Wadanganyika na hasa CCM ndivyo walivyotaka. Tanzania ilikuwa ikiuzwa soko la tandale (South Afrika) JK kaamua kama ni kuuza bora apeleke mali zake Kariakoo (USA)...ndivyo sera zao zinavyosema na tulichagua JK kutokana na sera hizo au sio?
Je, kuna kiongozi yeyote anaweza kufanya mazuri nje ya sera zilizomchagua kwa asilimia 80%?.
Matumizi ya serikali yapo wazi ktk vitabu! Kama wewe umewahi kufanya kazi kitengo cha Uhasibu utagundua kuwa kila safari ya kiongozi yeyote huwa accounted for ili kuweka mahesabu sawa na sidhani kama kuna hata siku moja wananchi tumepewa wazi mahesabu ya hizi wizara unlesss kuna matatizo. Those with access ya hizi hesabu ndio wanaotakiwa kusimama na kutupa habari pale mahesabu hayakubaliani. Besides that tunatafuta sababu ambazo sijawahi kusikia maishani mwangu kuwa rais anatoa hesabu za misafara yake kwa wananchi wote waone.
JK alitoa mahesabu ya Sumaye kwa sababu hazikuwa wazi na sawa pia kulikuwepo na utumiaji mbaya wa hizo fedha. Nadhani kama JK anatumia vibaya hizo funds basi inatakiwa mtu asimame na kutuonyesha hesabu hizo na sio sisi kufanya dhana. nakubali sana kuwa hawa jamaa wana spend kishenzi na nasikia kuna baadhi ya Balozi wetu hawajalipwa mishahara yao kwa miezi.....
Lakini hizi habari bado ni uvumi ambao mimi siwezi kusimama na kum-acuse JK kwa sababu tu baadhi viongozi wetu wamenunua majumba USA mara wanakaa mahotel ya 5 stars...It has been like that since Mwinyi guys!
Pia kuna hili jingine, Mfumo wa siasa wenyewe unawaruhusu watu hawa kuwa wafanya biashara, jambo ambalo hakuna kati yetu anayeweza kunambia mtu kama Karamagi anaingiza kiasi gani kwa mwaka!...What he can or can't afford!
Kwa hiyo hapa kuna kimchezo ambacho kimeanzishwa toka Mwinyi ama Mkapa kuwa Viuongozi wanaruhusiwa kufanya biashara!..Hivyo ipo possibility ya wao kuweza kuwa na utajiri bila kupitia moja kwa moja wadhifa wao. wadhifa ni nyenzo tu ya kumsukuma mbele na kirahisi ktk Kutajirika kwake!..Sheria ambayo imepiata bungeni na inakubalika na vyama vyote vya Upinzani...
 
Mzee Es

Nitakuwekea kwenye pdf na kukutumia kwenye e-mail yako topic zote zinazohusu rich-monduli lakini na wewe fanya hivyo ili baadae ufanya comparison uone pale ambapo sikuona. That will be with you by Friday.
 
Back
Top Bottom