Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Huyu ndiye ‘the real’ Kikwete!

Mzee Sam,

Heshima yako mkuu, nimekusikia inatia uchungu kwetu wananchi kuendelea kuchezewa na ukweli tunauouna, tena mimi ninasikia uchungu zaidi kwa sababu ukiongea na viongozi wake JK, in private wanacheka kila kitu anachokifanya kuwa ni mazingombwe, sasa imefikia hata viongozi wa nje ya nchi yetu wanashangaaa kwamba what is going on!,

Kiongozi mmoja wa nje alikuwa anauliza hivi majuzi in private, hivi hawa viongozi wenu wanachaguliwa kwa vigezo gani? Huyu ni kiongozi toka London, unajua nilikuwa hapo majuzi, sasa alikuwa anauliza balozi hapa mmeleta wakili wa kujitegemea, na sasa nasikia katibu mkuu mpya wa foreign amewahi kufanya kazi ubalozi wa Zimababwe tu, sasa haya mambo ya diplomasia atayaweza vipi? Ilikuwa aibu maana hata mimi sikujua kuwa huyo katibu hizo ndizo CV zake na bado siamini!

Viongozi karibu wote walioko karibu na Muungwana JK, huishia kucheka kila kitu anachokifanya na kusema, je hiyo inasema nini kuhusu maendeleo ya nchi yetu? Hiii ya Richmond ndio aibu hata kusema ukiwauliza wote hucheka sana kuwa ati ni kichekesho cha mwaka!

Sasa Mzee Wangu JK, madaraka uliyataka mwenyewe, umeyapigania weeeeee kwa udi na uvumba, sasa sisi wananchi tufanye nini? Umetaka kura ukatuambia wengine wote hawafai, unayefaaa ni wewe, sawa mwanangu tukakupa na kukupigia kampeni nzito, sasa sio siri mambo yamekushinda mwanangu, siku njema huonekana asubuhi, sasa miezi 11 ya kwanza wananchi hatuna hamu, tena sasa hutaki misifa tena, sasa kuna viongozi ambao wameshaanza kumuomba Mzee JM, asiondoke maana wanasema akitoka tu basi huu usanii serikali sasa utahamia kwenye CCM pia, na ndio basi tena, NO mimi ninasema huyu mzee ni lazima aondoke ili huyu Rich-Monduli Lowassa, anayekilalia macho hicho cheo anyimwe na apewe mtu mwenye uwezo, ambaye ataweza kuikemea serikali na labda hata kubadili muelekeo wa sera za serikali. In private wanasema inaonekana the goal ilikuwa kumpa ukatibu wa CCM a standing comedian of Makamba's calliber, sasa why not Meya wa zamani wa Dodoma, Mzee Mavunde ambaye wanasema ni more of a true comedian than Makamba?

Ninaweza kwenda on and on, maneno ya viongzi wa karibu yako Muuungwana, fanya mabadiliko ndugu yangu, hao wenzako wakaribu wanakucheka hao, rekebisha nji, rudisha umeme kwanza tuonane usiku, sisi wazaramo wa mjini gazeti la kesho husoma usiku wa leo, sasa hatuwezi tena mwanangu tuleteee umeme!
 
Mzee Es na wanabodi tuendeleeni kupiga kelele hawa jamaa hii ndio lugha wanayoijua.

What is wrong with Blair? I beg to differ and I think it is wrong to compare Blair and JK. DrWHO I think lets leave Britain on this issue and concentrate on Tanzania. I don't want to spoil this issue of JK.

If this was about UK it would have been o.k.

Matatizo ambayo yanatokea hivi sasa na policy za JK matokeo yake yataonekana wakati yeye mwenyewe ameacha kazi; itakuwa ni malipo makubwa ambayo hata yale ya vita ya Uganda ambayo tunaambiwa Britain walilipa (If that is correct) kuwa peremende.

Nchi haina ilichoshika mashirika yanauzwa kama karanga, maneno mengi hamna vitendo. Maamuzi ya msingi ambayo Tanzania inatakiwa kufanya yanafanywa na watu wachache kwa manufaa yao binafsi.

Kama kweli sifa inakinaisha kwa nini rais hajiulizi maswali haya:

1. Kwa nini marais wa Uganda, Kenya, Rwanda na Burundi na nchi za magharibi wanamsifia? (wameona kitoweo kipo nje nje tena sio mbali………………&#8230😉

2. Kwa nini watanzania waliobobea kwenye fani mbalimbali bado hawataki kwenda Tanzania kufanya kazi bali ni wageni kutoka Ulaya na nchi jirani? (maombi ya watanzania kurudi kufanya kazi nyumbani hayakuanza leo ni kutoka enzi ya rais Mwinyi, baadaye Mkapa ambaye kila alikokwenda alisema hayohayo vilevile wakati yeye ni waziri wa mambo ya nje)

3. Kwa nini anamsikiliza sana Edward Richmonduli ambaye ni kibaka wa rushwa wa kutisha?

4. Ni lini atamwezesha mtanzania kutembea kifua mbele nchini mwake na sio wageni?

5. Ni lini ataanza kuwachukulia hatua madhubuti wageni wanaofanya kazi kiholela ambazo wabongo wana uwezo nazo?



You can go on and on na matatizo ni mengi na JK is not up to it (kwa nini asijiuzulu). One year has passed and what we have seen so far is recycling people and try and error business. We are dealing with people's lives and a country. 45 years from independence we should be able to remove failures appropriately without much damage and any fuss.
 
Haya ni maneno ya balozi mmoja wa nje aliyeko hapa bongo,

Shillingi Billioni nne za bongo, zimetumika kwa ajili ya sherehe ya miaka 45 ya uhuru, je kulikuwa na umuhimu gani wa kufanya sherehe nzito kwa ajili ya miaka 45, badala ya kusubiri ifike 50?

Kwa sheria za kizungu miaka 25 inaitwa Silver, halafu 50 inakuwa golden na pia ku-make more sense, hizo hela zisingeweza kuongezewa ili zisaidie kutatua kwenye tatizo la umeme?
 
In a quite differing comparison, JK is more like IDD AMIN DADA, in intellect....
 
Wambandwa,
Sasa mzee wangu umekwenda nje...hiyo comparison yako haina ground kabisa...unless hili neno intellectual lina maana nyingine tusiyoifahamu
 
Approach ya JK kwenye maswala ya ki uchumi ni sawa sawa na Idd Amin alipomwamrisha waziri wake wa fedha a - print noti nyingi akifikiri wingi wa noti ndo kukua kwa uchumi.
 
Wambandwa,
Sawa hilo la Idd Amin, kweli alisema hivyo. Sasa tupe la JK ambalo kiuchumi linalingana na hilo la Idd Amin!
 
Kikwete apumzikia Serengeti

Na Mwandishi Wetu

RAIS Jakaya Kikwete ameanza mapumziko ya mwisho wa mwaka katika Hoteli ya Seronera iliyopo katika Mbuga ya Wanyama ya Serengeri mkoani Mara.

Habari zilizopatikana na kuthibitishwa na Mwandishi Msaidizi wa Rais, Maura Mwingira, zilisema kuwa Rais atakuwa mapumzikoni katika sikukuu za Krismasi na Mwaka Mpya na anatarajia kurejea jijini Dar es Salaam kati ya Januari 2 au 3, mwakani.

Maura alisema endapo mambo hayatabadilika, hata hotuba ya mwisho wa mwaka ya Rais Kikwete ataitoa akiwa mapumzikoni.

Katika hotuba hiyo Kikwete anatarajiwa kuzungumzia masuala mbalimbali, yakiwemo ya rushwa na upatikanaji wa haki nchini, ambayo aliahidi wakati akizungumza na makundi mbalimbali wakati wa maadhimisho ya mwaka mmoja wa utawala wake mkoani Dodoma wiki iliyopita.

Hoteli ya Seronera aliyopumzika Rais Kikwete ipo katikati ya mbuga ya Serengeti, ni ya hadhi ya nyota nne ikiwa na vyumba 75 vya kulala, kikiwemo kimoja chenye hadhi ya rais (Presidential suit). Bei za vyumba hivyo ni kati ya dola za Marekani 87 na dola 418 kwa siku.

Hii ni mara ya pili Rais Kikwete kwenda mapumzikoni baada ya yale aliyofanya kati ya Agosti mosi hadi Agosti sita mwaka huu alipokuwa mkoani Mwanza.

Hata hivyo, wakati huo Rais Kikwete alikatiza muda wake wa mapumziko na kufanya kazi mbalimbali, ikiwemo ziara katika Kiwanda cha nguo cha Mwatex aliyofanya Agosti 4, mwaka huu.


Mapumziko ni haki ya kila mfanyakazi lakini huyu jamaa naona kama pumzi imemuishia ndio maana mapumziko yamekuwa yakifukuzana.Naona mwandishi wa habari hiyo hapo juu amesahau kuyataja mapumziko aloyafanya Zanzibar kipindi cha Idd na kipindi flani alienda kuzembea Dodoma.
Halafu naona huu sasa ni kama utamaduni mpya wa Rais kwenda kupumzikia hoteli ya kitalii ambapo mamilioni ya shilingi yatatumika "kufanikisha" mapumziko yake,ikiwa ni pamoja na gharama za wapambe wake.Kwanini asiende kupumzikia nyumbani kwake Bagamoyo na hivyo kuokoa mamilioni ya fedha zitakazotumika kulipia makazi yake huko hotelini Serengeti?Nyerere alikuwa akienda kupumzikia Butiama,Mwinyi alikuwa anakwenda Zenji na Beni alikuwa anakwenda Masasi.Sasa huyu Vasco Da Gama ina maana hana kwao au anaendekeza matanuzi tu huku Watanzania wanaendelea kutaabika na matatizo kibao yanayowakabili!
 
Kikwete apumzikia Serengeti


Mapumziko ni haki ya kila mfanyakazi lakini huyu jamaa naona kama pumzi imemuishia ndio maana mapumziko yamekuwa yakifukuzana.Naona mwandishi wa habari hiyo hapo juu amesahau kuyataja mapumziko aloyafanya Zanzibar kipindi cha Idd na kipindi flani alienda kuzembea Dodoma.
Halafu naona huu sasa ni kama utamaduni mpya wa Rais kwenda kupumzikia hoteli ya kitalii ambapo mamilioni ya shilingi yatatumika "kufanikisha" mapumziko yake,ikiwa ni pamoja na gharama za wapambe wake.Kwanini asiende kupumzikia nyumbani kwake Bagamoyo na hivyo kuokoa mamilioni ya fedha zitakazotumika kulipia makazi yake huko hotelini Serengeti?Nyerere alikuwa akienda kupumzikia Butiama,Mwinyi alikuwa anakwenda Zenji na Beni alikuwa anakwenda Masasi.Sasa huyu Vasco Da Gama ina maana hana kwao au anaendekeza matanuzi tu huku Watanzania wanaendelea kutaabika na matatizo kibao yanayowakabili!



Rais sharti apumzike ila hizi holidays kama unavyoeleza hapo juu zimekuwa nyingi. Wanamtandao wanataka kuishi peponi wakiwa Tz kwa cost ya mlalahoi.

Mlalahoi mimi naona huenda makazi ya JK huko Bagamoyo hayastahili hadhi ya raisi, hivyo subiri kwanza watumie mafedha ya walipa kodi kugeuza hayo makazi kuwa kama hotel ya 4 stars ya hadhi ya rais then naona atakuwa anaenda huko.

Kuna mtu anaweza kujua kama huyu bwana mkubwa alikuwa anapumzika hivi alipokuwa waziri....???
 
Mnajua akipumzika Bagamoyo basi "Waswahili" watakuwa wengi wakitaka kumtembelea na kumueleza matatizo yao, kuanzia miggoro ya viwanja na mashamba Bagamoyo, mpaka wengine kuomba hela ya sikukuu ya Idi El Haj! Na yeye kwa vile "mtu wa watu" basi anaweza kulazimika kuwasikiliza na kuwapa vijisenti kidogo!

Kwa kuwa anahitaji utulivu ili aandae hotuba nzuri ya kufunga na kufungua mwaka basi heri akae huko "mbali". Tena ni bora awe huko badala ya kusema anaenda Puerto Rico au Shelisheli!

Akikaa Serengeti wakati anafikiria DPP mpya labda anaweza akamteua mkali kama chui (safari hii atakuwa mwanamke?). Pia atafikiria vizuri Gavana mpya wa BoT atakayekuwa makini kama simba!
 
Katika Ziara Yake Ya Japan Rais Kikwete Alipokwenda Kumwaona Mfalme Wa Japan.

Balozi Wa Tanzania Uk Alipokwenda Kujitambulisha Kwa Mfalme Wa Uingereza
 

Attachments

Dua,

Eeeeeh bwana weee! hivi huyo ni JK?.... Looooh kwa mila za kiafrika hapa mshikaji - KASUJUDU!
Na waulize waumini wa dini zao kama kweli wanaweza kumsujudia binadamu mwingine!..
HUyu JK nadhani bado anatakiwa kupewa darasa... hii aibu!
 
Wakati unakula kuku hapo Serengeti bila aibu naona nikukumbushe wale waliokutangulia jinsi walivyotuhadaa na bila aibu wanaendelea kula kile ambacho hawastahili kwa sababu kama kweli serikali yetu na bunge lake vingekuwa vinafanya kazi kikamilifu ilibidi wawe lupango wakihojiana na brother Dito kwa madhambi yao.

Mwinyi alipoingia alipewa fagio la chuma pale magogoni. Je ni nani anafahamu fagio lile lilifanya nini au kazi gani? Au liliishia wapi? Aliondoka kwa misifa isiyokuwa na msingi.

Mkapa alikuja na uloho wake kama fisi usio kifani; maana ulafi haufanani na ule uliopita hivyo akabuni hadithi ya viongozi kutaja mali zao? Je ni nani anakumbuka utajiri wake binafsi wakati alipoingia madarakani na alipostaafu yeye mwenyewe?

Wewe na awamu yako umeingia kwa vimbwenga kivyake vyake umepewa kila jina la wauza unga pamoja na wala rushwa cha kushangaza uliwapigia magoti ati waache biashara hizo na wajisafishe – Je kwanini usiwachukulie hatua kama majambazi? Au rafiki yako Edward Richmonduli amekuahidi ndito? Utamaduni wa Swazi naona utatushinda kama kweli tunataka nchi yetu iendelee.

Kutokana na chati ya marais wa Bongo hadi hivi sasa unaendelea kushika mkia KUFUATANA NA TAKWIMU NILIZONAZO ingawaje uliingia kwa kishindo na mbwembwe tosha.

Uongozi wako utakuwa hauna maana kwa kutegemea vi-nchi ambavyo vinategemea Tanzania kuongoza, lakini hadi hivi sasa umekuwa mwepesi kuchukua maoni ya dikteta kutoka Uganda kama vile yeye ndiye alikuchagua. Tuliokuchagua tupo hapa na tunataka ukate mzizi wa fitna hivi sasa yaani UANZE KUONGOZA NCHI SIO KUONGOZWA:

1.Wote ambao majina yao unayo uwashughulikie hii ni pamoja na kiporo cha Edward Lowasa ambaye jina lake lilitajwa na mwalimu kule Dodoma 1995.

2. Washughulikie wauza unga mara moja kwani vijana ambao ni taifa la kesho wanateketea,

3. Ahadi yako kwa mikataba ya madini inachukua muda mrefu bila utatuzi kulikoni?

4. Wote waliopitisha mkataba wa umeme wa Richmond wachukuliwe hatua kwa kulitia hasara taifa.
 
Jamani, JK hajaagiza ku print noti, ila ana zifuja. wengi katika baraza lake la mawaziri ni kama kalipa fadhila kwa sababu badala ya kuwepo madarakani wakatutumikie sisi tuliowapa ridhaa ya kuwepo pale wanarumia mianya hiyo kujilimbikizia mali.
Jk na wenzie kuwa kwao ktk uongozi imekuwa kama wamepata mtaji usiokuwa na riba na wala haurudishwi.
JK na viongozi walio chini yake wanapaswa waweke kipau mbele maslahi ya umma mzima wa Tz badala ya wao binafsi.
Kwa mantiki hiyo, kumfananisha JK na Idd ni huo uhayawani ambao unamfanya apuuze kugundua ni nini mwananchi anahitaji - sio wapambe wake wanahitaji.
Amekuwa akiwafurahisha wapambe wake toka alivyoingia madarakani kuliko sisi tulio fanya makosa ya kumchagua.
SIONI TOFAUTIU KATI YAKE NA IDD
 
Wambandwa,

Hili la ridhaa yetu ni jukumu la kila rais lakini hakuna tofauti kati ya JK, Mwinyi wala Mkapa.
Nikiwa na maana kwamba hakuna kiongozi hata mmoja leo hii kaupata Utajiri wake kupitia kwa JK. Hawa wote wameanza kutajirika toka tulipokubali Ubinafsishaji na Uwekezaji...Kifupi, ukifuatilia hili swala, ulimbizakaji mali kwa viongozi ni mfumo wa CCM kiutawala lakini huwezi kuuona ktk maandishi.
Tunachogomba hapa ni jinsi huyu msanii wetu anavyotaka wananchi waamini kuwa hii sinema yake sio fiction ila non - fiction.

Mimi, binafsi kusema kweli natofautiana na wengi waliochangia hii mada. Namtazama JK kama vile watawala wengine wa kiafrika ambao hili neno Ridhaa ya wananchi ni neno ambalo halipo ktk utamaduni wao... JK kama watawala wengine hawafahamu tafsiri ya neno to GOVERN ktk leadership zaidi ya ile - To RULE.
Sasa inabidi Wadanganyika muweze kuelewa nini majukumu ya MTAWALA..kwani kila mtawala lazima awe tajiri kuliko wananchi wake na wale waliokuwa karibu ya hii Royal family ndio kwanza hupewa kipaumbele cha Utajiri. Mliobaki ni kutazama ahadi za huyu Mtawala... so far JK hana tofauti na watawala waliomtangulia. Huu ndio mtazamo wangu na kweli JK kafanikisha mengi ktk Utawala wake.
Expectation led us to believe he was/is a LEADER...kulingana na vyeti vyake. (Mwanajeshi, mwanafunzi wa Nyerere, mtoto wa mjini, mwafrika kwa asili, handsome boy - boyz to men n.k...
Sasa huwa najiuliza mjinga nani?...
 
Wambandwa,

Hili la ridhaa yetu ni jukumu la kila rais lakini hakuna tofauti kati ya JK, Mwinyi wala Mkapa.
Nikiwa na maana kwamba hakuna kiongozi hata mmoja leo hii kaupata Utajiri wake kupitia kwa JK. Hawa wote wameanza kutajirika toka tulipokubali Ubinafsishaji na Uwekezaji...Kifupi, ukifuatilia hili swala, ulimbizakaji mali kwa viongozi ni mfumo wa CCM kiutawala lakini huwezi kuuona ktk maandishi.
Tunachogomba hapa ni jinsi huyu msanii wetu anavyotaka wananchi waamini kuwa hii sinema yake sio fiction ila non - fiction.

Mimi, binafsi kusema kweli natofautiana na wengi waliochangia hii mada. Namtazama JK kama vile watawala wengine wa kiafrika ambao hili neno Ridhaa ya wananchi ni neno ambalo halipo ktk utamaduni wao... JK kama watawala wengine hawafahamu tafsiri ya neno to GOVERN ktk leadership zaidi ya ile - To RULE.
Sasa inabidi Wadanganyika muweze kuelewa nini majukumu ya MTAWALA..kwani kila mtawala lazima awe tajiri kuliko wananchi wake na wale waliokuwa karibu ya hii Royal family ndio kwanza hupewa kipaumbele cha Utajiri. Mliobaki ni kutazama ahadi za huyu Mtawala... so far JK hana tofauti na watawala waliomtangulia. Huu ndio mtazamo wangu na kweli JK kafanikisha mengi ktk Utawala wake.
Expectation led us to believe he was/is a LEADER...kulingana na vyeti vyake. (Mwanajeshi, mwanafunzi wa Nyerere, mtoto wa mjini, mwafrika kwa asili, handsome boy - boyz to men n.k...
Sasa huwa najiuliza mjinga nani?...
:

Ni sisi wapiga kura mheshimiwa Mkandara! Inauma lakini ndo ukweli huu.
 
Dua,
Ushauri wako ni muruwa. Lakini kumbuka Mwalimu alituasa kuwa kiongozi yeyote atakayeingia Ikulu kwa kutumia rushwa atawakumbatia wala rushwa. It is happening before our own eyes.
 
Back
Top Bottom