Huyu ndiye mume wangu

Huyu ndiye mume wangu

Nilipokuwa mdogo nilikuwa nachukia sana Bi mkubwa alipokuwa ananifundisha kupika, kufua, kuchota maji, kuosha vyombo, kupiga pasi nguo ili hali Mimi ni mwanaume.

Kumbe alikuwa anajua kwenye maisha kuna wakati unaweza kuoa akina Sky Eclat
Kwa hili namshukuru sana Bi mkubwa, kwani waifu hapati wasiwasi kuhusu watoto kuogeshwa, kufuliwa uniform wala kula kwani ninapokuwa nyumbani natimiza yote hayo hata kama atakuwa amesafiri.
Hata nikiumwa hakuna haja ya kutafuta ndugu wa kusaidia. Mambo yanakwenda kama kawaida.
 
Japo kapicha kake please


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Ni m-Tanzania, hajawahi kunipiga, Hulipia huduma zote ndani kuanzia umeme, maji na gesi. Jumamosi anakwenda sokoni asubuhi, Ana kumbuka mpaka pilipili na ndimu. Anajua kupika hivyo hata nikichelewa sina wasiwasi kuwa atakuwa na njaa.

Nguo zake anafua na kupiga pasi mwenyewe. Ni msafi na anapenda vitu vikae katika mpangilio. Hajali hata kukiwa na wageni anaosha vyombo vyote baada ya kula.

Siku za likizo kwenda kusalimu ndugu na jamaa nauli ni juu yake kwa familia nzima.

Lakini ana upande wa pili pia. Maua yote si mawaridi.
Huo upande wa pili kazima atakuwa anapumuliwa kisogoni.

Kazi za kike anafanya yeye ili iweje?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata nikiumwa hakuna haja ya kutafuta ndugu wa kusaidia. Mambo yanakwenda kama kawaida.
Absolutely!
Ila fanya umsaidiage kazi kidogo mumeo kwani akifanya kazi za nyumbani yeye kila siku hawachelewi kusema umemwinamisha.😁😁😁
 
Ni m-Tanzania, hajawahi kunipiga, Hulipia huduma zote ndani kuanzia umeme, maji na gesi. Jumamosi anakwenda sokoni asubuhi, Ana kumbuka mpaka pilipili na ndimu. Anajua kupika hivyo hata nikichelewa sina wasiwasi kuwa atakuwa na njaa.

Nguo zake anafua na kupiga pasi mwenyewe. Ni msafi na anapenda vitu vikae katika mpangilio. Hajali hata kukiwa na wageni anaosha vyombo vyote baada ya kula.

Siku za likizo kwenda kusalimu ndugu na jamaa nauli ni juu yake kwa familia nzima.

Lakini ana upande wa pili pia. Maua yote si mawaridi.
Babu Asprin hongera kwa kuunga mkono juhudi za bibi Sky Eclat za kubwia limbwata kwa hiari yako.
Bibi malizia hapo chini awe anakufulia nguo zako, kupiga deki pamoja na kuosha vyombo.

Maendeleo hayana chama
 
Babu Asprin hongera kwa kuunga mkono juhudi za bibi Sky Eclat za kubwia limbwata kwa hiari yako.
Bibi malizia hapo chini awe anakufulia nguo zako, kupiga deki pamoja na kuosha vyombo.

Maendeleo hayana chama
No no nguo zangu ninafua na deki ninapiga pia ndugu zake ninawapenda sana.
 
No no nguo zangu ninafua na deki ninapiga pia ndugu zake ninawapenda sana.
Hongera bibi, siku zote nlikua sijui kama babu Asprin ni mpemba mpaka leo ulivyosema jumamosi anachukua kikapu chake anaweka kwapani anaenda zake markiti na hasahau hata pilipili.

Maendeleo hayana chama
 
Umemtengeneza vizuri sana , hicho ndicho tunachotakiwa kufanya, tengeneza mtu unayempenda kichwani mwako, mpe sifa zote halafu basi ishi nae utaona maisha rahisiiii...hongera bibie!
 
Ndio mana Asprin analala sana...manake baada ya kazi za kufua na kupiga pasi anatakiwa aje amalizie na kwa bed
akishafanya yote hayo hapo kwa bed ataishia kupakapaka rangi tu.

Maendeleo hayana chama
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom