Huu ni ukweli? Kwa nini kimefichwa?

Huu ni ukweli? Kwa nini kimefichwa?

Salaam, katika Biblia ya kikatoliki, kuna kitabu cha Judith, huyu alikuwa msichana wa kiyahudi aliyejifanya kahaba ili anunuliwe na mfalme pinzani wa Israel, inasemekana aliponunuliwa akamkata kichwa mfalme akatoka nacho akiwa amekibeba juu juu, na vita ikaishia hapo(Israel ikapata ushindi).

Kina ukweli hiki? Mwanamke akate kichwa cha mtawala? Wajuzi njoeni

Mkuu Moja Kati Ya Siraha Hatali Ulimwenguni Kuliko Zote Ni Mwanamke Mrembo Anaejua Kuitumia Akili Yake Vyema Lejea Stor Ya Creopatra
 
sitaki kuongelea kitabu hicho, kwasababu ninyi wakatoliki kuna vitabu vingi tu mmevikubali ambavyo shetani alileta ili kupotosha ukweli. ila kwa habari ya spy wa kike au wanawake hodari wa vita, hata Debora kwenye agano la kale alimuua adui wa israel. sio kitu cha ajabu hicho.
Hivyo vyenyewe unavyovijua ni kwasababu wakatoliki wameidhinisha.Na nakala zote original za source na barua na nyaraka za mitume e.g waraka wa Mtume Paulo kwa wakolosai zote zipo Vatican.Je wasingeidhinisha ungevijulia wapi?
 
Biblia ni kitabu cha kutungwa tu kama riwaya nyingine. Japo kina mafundisho mengi mazuri (kila riwaya ina mafundisho) lakini usiamini story zake sio za kweli.
Wewe unakaribia kuijua kweli mda sio mrefu utakua mwinjilisti wa kimataifa

#hata sauri alikua kama wewe ila alikuzidi kidogo lakini ndo akawa chombo kiteule cha Mungu na kubeba maumivu yaleyale kama alokua akiwafanyia wenzake
 
Kumbe shetani aliwahi kuandika vitabu[emoji15]
Sikuwahi kulijua hili[emoji1]

Lakini ni vyema kabla hujaanza kunyooshea kidole kanisa katoliki, ni vizuri ukajifunza historia kidogo ya haya maandiko, machapisho yake na editions

Biblia inayotumiwa na wakatoliki ndio biblia ya kwanza kuwahi kutengenezwa na kutumiwa na wakristo wa makanisa yote ulimwenguni kabla ya hiyo yenu mnayoita tafsiri ya ulimwengu mpya

Jifunze, acha kukaririshwa kunyooshea vidole makanisa ya wenzako huku kanisa lako halina hata historia yoyote kwenye ukristo
Ni sahihi lakini lazima ujue wa-catholic wa mwanzo hawa kukubaliana kwa kila jambo na kila andiko
ndani ya u-catholic kulikuwa na makundi mengi sana ikiwemo gnostic wa-catholic hawa walipokuja kuungana
na warumi wakaanza kuwaua wapinzani wao ndani ya kanisa na nje ya kanisa.
Kunawatu walikuwa hawakubaliani na ucatholic ulivyo tafsir bible japo walikuwa wa-catholic
wapo waliodai haiwezekani Mungu wa agano jipya na lake akawa mmoja,
kwa sababu Mungu wa agano jipya ni wa upendo, msamaha tofauti kabsa na Mungu
wa agano lake.
Mpaka ikaenda kupelekea dark age kanisa linatawaliwa na mapapa wawili
kila mmoja anajitangaza yeye ni papa akishindwa kumtambua mwenzake.
Mtu kama Martin Luther ameeandika vitabu vingi sana kwenye u-catholic vinavyotumiwa mpaka
leo anakuja kutofautiana na kanisa papa alipotangaza kuwa mtu anapaswa kununua kitabu flani
ambacho kila muumini atakaye nunua atabarikiwa na Mungu na hela itayo patikana itaenda kufanya
ujenzi wa kanisa la vatican Martin akasema Mungu anatoa baraka bure hawezi kutoa baraka kwa fedha.
Hii ndio inapelekea Martin kutangazwa mzushi wa kanisa na kuondoka.
Hawa walioondoka kwenye ucatholic walikuwa wanaujua vizuri sana.
 
Mkuu Moja Kati Ya Siraha Hatali Ulimwenguni Kuliko Zote Ni Mwanamke Mrembo Anaejua Kuitumia Akili Yake Vyema Lejea Stor Ya Creopatra
Hata kama, ila sidhani kama Judith alikuwa mrembo, hakuna andiko lisemalo alikuwa mrembo.
 
Soma Vizuri Wakati Judith Anaenda Kupelekwa Kwa Jemedali Wale Walinzi Wake Walisemaje,
Ukishasoma Ndo Uje Tena Kubisha
Sasa nielekeze hicho kitabu kinapatikana wapi! Siwezi kukuamini kuwa walinzi walimsifia kwani huna proof!
 
Kwa wote mnaopenda vita vya dini.

AS LONG AS UNAABUDU MUNGU ALIYEUMBA MBINGU NA NCHI, NA HUYO MUNGU HATAKI MAOVU UPO SAHIHI BILA KUJALI UNAMUITA JINA GANI.

MENGINE YOOOOTE NI JANJA JANJA ZA KUKUZA SADAKA.
 
Sasa nielekeze hicho kitabu kinapatikana wapi! Siwezi kukuamini kuwa walinzi walimsifia kwani huna proof!

IMG_1887.jpg

Soma Vzr Mstari Wa 19
 
Kwa wote mnaopenda vita vya dini.

AS LONG AS UNAABUDU MUNGU ALIYEUMBA MBINGU NA NCHI, NA HUYO MUNGU HATAKI MAOVU UPO SAHIHI BILA KUJALI UNAMUITA JINA GANI.

MENGINE YOOOOTE NI JANJA JANJA ZA KUKUZA SADAKA.
Jabali la karne! Nakukumbusha kuwa katika kumuabudu Mungu huyo ni pamoja na kutoa sadaka!
 
Back
Top Bottom