Huu ndio Ulinzi wa Rais Samia Suluhu

Huu ndio Ulinzi wa Rais Samia Suluhu

Suala la kuwa na ulinzi mkali linategemea na tabia za Rais au kiongozi mwenyewe jinsi anavyoishi na watu,anaweza akawatengeneza maadui yeye mwenyewe na akawa anaogopa hatima ya usalama wake na ndio kupeleka kuwa na maulinzi makubwa,ama anaweza akatengeneza marafiki wengi watu Safi na uhusiano mzuri na raia wake na hi ikapelekea kuwa na ulinzi wa kawaida.
Ni mapema mno Samia kumpa sifa hiyo,so long as yeye Ni CCM ,na CCM Ni ileile.tusubiri tuone.
Hata uwe msafi mpaka unawaka kama almasi ulinzi madhubuti ni muhimu No matter what...No offense.

_Kiislam hakuna aliye msafi kama Mtume (S.W.A) na alishambuliwa na mawe.

_Kikristo hakuna aliyemsafi zaidi ya Yesu na alishambuliwa.

Ulinzi madhubuti ni muhimu no excuse...akili mfu tu ndio itapinga.
 
Mtu hajatengua hata mwenyekiti wa mtaa mmoja utegemee alindwe kwa "mbwembwe".

Subiri aanze kutengeneza maadui lazima atashauriwa na kuimarishiwa ulinzi.

"Muda unaodhani uko salama ndiyo huwa wa hatari zaidi"
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa na walinzi wake akiwasili Chato kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Hayati John Pombe Magufuli.

Nimependa jinsi ulinzi wa Rais Samia ulivyo, yaani hakuna mbwembwe nyingi kama za mtangulizi wake. PSU ya Rais Samia naipa kongole kubwa[emoji91]
View attachment 1734785
kwahyo yule wa Magufuli anastaafu au anarudi kambi?
 
Kwanza ni matumizi mabaya ya fedha za umma na pili kutokujiamini kama kweli unakubalika na jamii.
Kuna aliyekubalika na jamii Duniani zaidi ya Mtume Muhammad na Yesu na walishambuliwa.

Tuache Thinking za hovyo
 
Rais yupo smart Sana huyu , Ila mtangulizi wake kamuachia mzigo mzito Sana , kuna miradi hapo ni ya kupiga chini bila kupepesa macho , na aongeze mzunguko wa pesa mtaani , fungua uhusiano wa kimataifa ,ajiri watu , ongezea mishahara ...... Maisha mafupi haya bhana sio tuanze kutishana tishana tena, mwisho tufe tunasubiriaga Tanzania hewa ya viwanda
Live wewe ni mhanga wa vyeti feki
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa na walinzi wake akiwasili Chato kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Hayati John Pombe Magufuli.

Nimependa jinsi ulinzi wa Rais Samia ulivyo, yaani hakuna mbwembwe nyingi kama za mtangulizi wake. PSU ya Rais Samia naipa kongole kubwa[emoji91]
View attachment 1734785
Duh....aisee...watu wengine dah...yaani kimbelembele Cha kutaka kutuaminisha kuwa anajua masuala ya ulinzi na usalama...duh...
 
Ndo kwanza hana ata wiki 2 utazani usha muona akiwa mtaani.
Huu ukinzi uko poa.
Unatoa ujumbe kuwa rais ni wa nchi ya amani na utulivu.
Ni rais atakae tekeleza majukumu yake kwa haki akifuata katiba aliyoapa kuilinda.
Mtangulizi wake alikuwa akilindwa na wanajeshi wenye magwanda na mibunduki mizito mizito kama marais wa nchi za vita ya wenyewe kwa wenyewe.
Bwana asipoulinda mji wakeshao wanafanya kazi bure (zaburi 127:1)
 
Samia is Magufuli 2
Rais yupo smart Sana huyu , Ila mtangulizi wake kamuachia mzigo mzito Sana , kuna miradi hapo ni ya kupiga chini bila kupepesa macho , na aongeze mzunguko wa pesa mtaani , fungua uhusiano wa kimataifa ,ajiri watu , ongezea mishahara ...... Maisha mafupi haya bhana sio tuanze kutishana tishana tena, mwisho tufe tunasubiriaga Tanzania hewa ya viwanda
 
Kuna aliyekubalika na jamii Duniani zaidi ya Mtume Muhammad na Yesu na walishambuliwa.

Tuache Thinking za hovyo
Hayo ni mawazo mgando! Kwa hiyo alikuwa anategemea mabunduki na si Mungu kama alivyokuwa anajinadi!
 
Mnajuaje kwani ndo hao tuu? si kuna wale wanajeshi lazima wawepo na silaha nzito?
 
Hayo ni mawazo mgando! Kwa hiyo alikuwa anategemea mabunduki na si Mungu kama alivyokuwa anajinadi!
Pumbafu

Hemu soma mtiririko wa hoja basi vipi wewe jinga kabisa.

Nimekupa mfano hekima ikiwa uwone kuwa msafi sio tiketi ya kuwa salama hivyo ulinzi muhimu Instead kujua dhumuni la mfano ni nini....umeshindwa kuelewa unandika sijui Mungu sijui nini Rubbish.

JF kuwe na vigezo vya mtu kujiunga kupunguza kuchoshana mtu haelewi hata Mfano.

Alafu nikufundishe kitu uwelewa wako mdogo sana kuhusu Mungu...Mungu hakulindi kimiujiza ulinzi wa Mungu anapitisha kwa njia za kawaida unahitaji kujilinda na CCTV, Electric Wire, Bunduki nk ndipo Mungu anapitisha ulinzi wake humohumo sio umekaa kahasarahasara useme Mungu anakulinda uwo ni upuuzi.
 
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania akiwa na walinzi wake akiwasili Chato kwa ajili ya kushiriki mazishi ya Hayati John Pombe Magufuli.

Nimependa jinsi ulinzi wa Rais Samia ulivyo, yaani hakuna mbwembwe nyingi kama za mtangulizi wake. PSU ya Rais Samia naipa kongole kubwa[emoji91]
View attachment 1734785
Mbona wale wanajeshi wenye makombora ya kivita siwaoni?
 
Back
Top Bottom