Husein Tuwa ni habari nyingine bana,natafuta riwaya za huyu jamaa kwa anayefahamu wapi zinapatikana tafadhari tupeane taarifa
Kucompare watu maarufu si kitu kibaya, mara nyingi ni kuangalia mazuri na kuyaendeleza na yale mapungufu kuyarekebisha.
Kwenye suala la hadithi(riwaya) za magazetini, mimi nilijitahidi sana kufuatilia hadithi za Eric Shigongo(Ijumaa) na hadithi mbili tu za Hussein Hassan Tuwa(Mtuhumiwa na Mkimbizi).
Kwa maoni yangu, hadithi za Mr. Tuwa zilikuwa zina msisimko zaidi. Zilikuwa zinakupa nafasi ya muhusika kuwa kama ndiye uliyeko kwenye hadithi. Ilikuwa unapata picha kabisa.
Kwa maoni yangu naona Hussein Hassan Tuwa ni mtunzi mahiri na hodari kuliko Eric Shigongo.
Constructive comparison please!!
View attachment 66403
Story za shigongo ndefu na zinachosha
makali ni tuwa hata sultan tamba,story zake zina msisimko sana
Husein Tuwa ni habari nyingine bana,natafuta riwaya za huyu jamaa kwa anayefahamu wapi zinapatikana tafadhari tupeane taarifa
sijawahi kusoma za Tuwa, lakini nilisoma Shigongo - Rais anampenda mke wangu- mwisho wa siku niliboreka nikakiachilia mbali huku mwanzo aliaanza vizuri lakini hapo katikati akatoka kwenye mtiririko kama wanavyosema watu hafanyi utafiti.Hussein Tuwa huwezi kumfananisha na Shigongo,jamaa mkali sana,he is the best!