BigTall
JF-Expert Member
- Mar 9, 2022
- 422
- 1,049
Hivi karibuni kumekuwa na hoja kadhaa kuhusu vifurushi vya Huduma za Bima ya NHIF, kuna mengi yanazungumzwa lakini leo nataka kushea moja ambalo limenikuta na inawezekana likawa na madhara makubwa katika jamii japokuwa Watu wengi hawalitazami kwa jicho hilo.
Katika vifurushi ambavyo vinalipiwa na Bima ya NHIF hakuna huduma ya Mwanasaikolojia.
Mfano kama Hospitali inatoa huduma ya mtu wa Psychology (masuala ya saikolojia) basi utalipia cash hata kama una bima, mfano mimi nina bima kubwa ile ya Supplementary lakini unaambiwa lipa cash.
Hivi kwa mazingira yaliyo kuhusu changamoto za afya ya akili kwa sasa wanategemea hii issue ya Afya ya Akili Itaponaje?
Inawezekna katika jamii inamaini ili ufikie hatua ya kutambulika una changamoto ya afya ya akili basi mpaka uanze kuokota makopo au kuvua nguo hadharani?
Kuna watu wengi wana changamoto hiyo hasa kutokana na purukushani za kimaisha, ndio maana matukio ya watu kujiua, kujeruhi wengine, kufanya vitu vya ajabu mbalimbali vimekuwa vikiripotiwa kila mara.
Nashauri NHIF, Serikali, Taasisi za Afya na Wadau wengine wa afya kuliangalia hili, ni suala kubwa na linaloweza kuwa na maana kubwa kwenye kizazi kilichopo.
Katika vifurushi ambavyo vinalipiwa na Bima ya NHIF hakuna huduma ya Mwanasaikolojia.
Mfano kama Hospitali inatoa huduma ya mtu wa Psychology (masuala ya saikolojia) basi utalipia cash hata kama una bima, mfano mimi nina bima kubwa ile ya Supplementary lakini unaambiwa lipa cash.
Hivi kwa mazingira yaliyo kuhusu changamoto za afya ya akili kwa sasa wanategemea hii issue ya Afya ya Akili Itaponaje?
Inawezekna katika jamii inamaini ili ufikie hatua ya kutambulika una changamoto ya afya ya akili basi mpaka uanze kuokota makopo au kuvua nguo hadharani?
Kuna watu wengi wana changamoto hiyo hasa kutokana na purukushani za kimaisha, ndio maana matukio ya watu kujiua, kujeruhi wengine, kufanya vitu vya ajabu mbalimbali vimekuwa vikiripotiwa kila mara.
Nashauri NHIF, Serikali, Taasisi za Afya na Wadau wengine wa afya kuliangalia hili, ni suala kubwa na linaloweza kuwa na maana kubwa kwenye kizazi kilichopo.