Hongera Rais Samia, matendo huongea kwa sauti kuliko maneno

FaizaFoxy

Platinum Member
Apr 13, 2011
92,883
109,213
Hakika inabidi tukupe hongera kubwa sana mama Samia, umetufundisha Watanzania kuwa "matendo huongea kwa sauti kuliko maneno" (actions speaks louder than words).

Tukitazama mitandaoni na jinsi mambo yanavyodhaniwa na wapenda maneno kuwa ndiyo yalivyo, inabidi nikupe heko na hongera nyingi sana tena sana mama Samia, tumeona uchapaji kazi wako na tumeona jinsi unavyotutakia mema Waanzania bila kukurupuka.

Wanaotaka maandamano wanafanya, wanaotaka mikutano ya hadhara wanafanya, wanaotaka kwenda mahakamani wanakwenda, wanaosema hovyo wanasema. Wewe tuliiii, mama unawatia watu "presha" hivyo. Tulidhani unatufanyia tashtiti, kumbe la hasha, wewe unachapa kazi. Sasa nimeamini, kiongozi wa kweli hutenda, Wengine bila maneno maneno.

Kweli umetufundisha somo kbwa sana sote, umetufundisha tuwe watendaji zaidi ya waongeaji. Binafsi naamini na umezidi kuniyakinishia hilo, kuwa wasemaji sana hutaka yaaminiwe maneno yao siyo vitendo vyao na uhalisia uliopo.

Tulitaka na tunatamani sana mama ukurupuke, kama tulivyozoeshwa, lakini kwa hekima zako, unatuwachia tuwe huru kwa maoni yetu. wewe unachapa kazi tu.

Mama tuliyozowea maneno maneno na umbeya unatutia "plesha". Tunaona kama unatufanyia tashtiti.

Mama nakupongeza kwa hilo, tulishazowea siasa za kufokafoka na kuaminishwa maneno ya kuliko uhalisia.

Mama ahsante kwa kutufundisha kwa vitendo, inabidi tubadili mbinu. Twende kama unavyokwenda wewe "boss wetu" kisheria, kidemokrasia, kiusalama na amani, siyo kimihemko.

Kweli nimeamini "Matendo huongea kwa sauti kuliko maneno".
 
Hakika inabidi tukupe hongera kubwa sana mama Samia, umetufundisha Watanzania kuwa "matendo huongea kwa sauti kuliko maneno" (actions speaks louder than words).

Tukitazama mitandaoni na jinsi mambo yanavyodhaniwa na wapenda maneno kuwa ndiyo yalivyo, inabidi nikupe heko na
Kwa kweri Matendo Huongea Kwa Sauti. Kwenye Kuuza Bandari zetu Tumemkoma maana angeongea mapema angepigwa Mawe .


Siku Nyingine ujisemee wewe mwenyewe amekufurahisha. SIYO ametufurahisha. Amewafurahisha Pamoja na nani? Wakati wengine woote tuna hasira naye
 
Wapingaji na waongeaji wameangukia pua huko Temeke. Sasa ndo wajifunze kwamba watanzania wa 2023 sio watanzania wa 2013.

Maneno mengi mitandaoni na ID zao kumi kumi, kumbe tukienda kiuhalisia hamna kitu mkutano wa kupinga bandari ulidoda, japo waandaji hawana cha kupoteza baada ya kulipwa chao na wakwepa kodi na ushuru wa bandarini.
 

Attachments

  • 96b1cb7b-6117-48fc-80e4-ef0f5ee7f754.jpg
    96b1cb7b-6117-48fc-80e4-ef0f5ee7f754.jpg
    88.4 KB · Views: 5
FaizaFoxy ingekuwa DP World sio waarabu nina yakini pasi na shaka ungeshupaza shingo kupinga maana sijui ni ulimbukeni ama kutoelewa unahisi kila Muarabu anasimamia uislamu.
Na ungepinga zaidi kama ingekuwa alie kwenye hatamu ni mkristo.

Jinsi ulivyo biased kwenye mambo ya dini hakuna lolote utakalosimamia humu JF lionekane na tija.
 
Hakika inabidi tukupe hongera kubwa sana mama Samia, umetufundisha Watanzania kuwa "matendo huongea kwa sauti kuliko maneno" (actions speaks louder than words).

Tukitazama mitandaoni na jinsi mambo yanavyodhaniwa na wapenda maneno kuwa ndiyo yalivyo, inabidi nikupe heko na hongera nyingi sana tena sana mama Samia, tumeona uchapaji kazi wako na tumeona jinsi unavyotutakia mema Waanzania bila kukurupuka.

Wanaotaka maandamano wanafanya, wanaotaka mikutano ya hadhara wanafanya, wanaotaka kwenda mahakamani wanakwenda, wanaosema hovyo wanasema. Wewe tuliiii, mama unawatia watu "presha" hivyo. Tulidhani unatufanyia tashtiti, kumbe la hasha, wewe unachapa kazi. Sasa nimeamini, kiongozi wa kweli hutenda, Wengine bila maneno maneno.

Kweli umetufundisha somo kbwa sana sote, umetufundisha tuwe watendaji zaidi ya waongeaji. Binafsi naamini na umezidi kuniyakinishia hilo, kuwa wasemaji sana hutaka yaaminiwe maneno yao siyo vitendo vyao na uhalisia uliopo.

Tulitaka na tunatamani sana mama ukurupuke, kama tulivyozoeshwa, lakini kwa hekima zako, unatuwachia tuwe huru kwa maoni yetu. wewe unachapa kazi tu.

Mama tuliyozowea maneno maneno na umbeya unatutia "plesha". Tunaona kama unatufanyia tashtiti.

Mama nakupongeza kwa hilo, tulishazowea siasa za kufokafoka na kuaminishwa maneno ya kuliko uhalisia.

Mama ahsante kwa kutufundisha kwa vitendo, inabidi tubadili mbinu. Twende kama unavyokwenda wewe "boss wetu" kisheria, kidemokrasia, kiusalama na amani, siyo kimihemko.

Kweli nimeamini "Matendo huongea kwa sauti kuliko maneno".

Wewe mdini sana na huna akili, long ago i told you this and from your background sishangai, arrogance is your second nature, you have the darkest mind ever...!!
 
Kwa kweri Matendo Huongea Kwa Sauti. Kwenye Kuuza Bandari zetu Tumemkoma maana angeongea mapema angepigwa Mawe .


Siku Nyingine ujisemee wewe mwenyewe amekufurahisha. SIYO ametufurahisha. Amewafurahisha Pamoja na nani? Wakati wengine woote tuna hasira naye
Nafahamu kuwa umeaminishwa ujinga na ulivyo poyoyo umekubali. Kuna kesi mahakamani au siyo? Mama kimyaaa. Kuna waliofanya maandamano au siyo? Mama kimyaaa. Kuna wanaofanya mikutani, au siyo? Mama kimyaa.


Yeye anachapa kai zake na wengine mnachapa kazi zenu.

Sasa si umpopoe mawe, wenye kazi zao watafanya. Mambo kwa vitendo siyo kwa maneno.
 
Tunashukuru kwa mauzo haramu ya bandari yetu.
Naama, upo huru kushukuru, au ulizuiliwa? Upo huru kushukuru, kwenda mahakamani, kufanya maandamno, kufanya mkutano wa hadhara, kubishana na mumemo / ,keo katika hilo, ndiyo mama Samia atakavyo, tuwe huru kiukweli.


Sisi pia tunashukuru, AlhamduliLlah, hatujaiona bandari iliyouzwa. Tupo huru kushukuru pia, au siyo?
 
Wewe mdini sana na huna akili, long ago i told you this and from your background sishangai, arrogance is your second nature, you have the darkest mind ever...!!
Kwani kuwa "mdini" katiba inanikataza au kuna sheria inayonikataza?

Sasa unasema mimi ni "mdini" halafu unaji "contradict" unasema nna "darkest mind" hivi mwenye dini na asiye na dini nani yupo kizani?


Hapo sasa.
 
Huyo Samia atakuwa mpuuzi sana kama anafurahia kila siku kusifiwa na mjinga yule yule, hajiulizi hamna wajinga wapya wamsifie?
 
Back
Top Bottom