mengi ni chadema moyoni na ccm machoni mwa jamii. kwa kifupi anajifanya yupo ccm tu kwa ajili ya maslahi ya biashara zake na jinsi ya kupata nafasi za kuliibia taifa hiki kama vile alivyotaka kutuibia visima vya gesi.
Wana JF naomba mnisaidie kujua hili kwa uwazi pasipo matusi na kejeli.
Najua wazi kuwa Mengi kuwa mwanachama fulani cha Siasa siyo dhambi wsla kosa, lakini hoja yangu ni pale anapotumia fursa aliyo nayo kutumia vyombo vya habari kukashfu chama tawala, anatoa fursa kwa viongozi wa Chadema kutoa kashfa kwa vyama vingine na kuyapa muda mwingi sana matukano na kejeli hizo, mfano ITV hutangaza habari nyinngi sana za Chadema hususan ni zile za maneno ya wabunge wanaozungumza mambo ya kuiponda Serikali, Pia kuna tukio jingine nalo lilitushangaza Watanzania, Kwanini Mtei alizindua kitabu chake cha "gother to governor" kwenye Hotel ya Mtei? Je tuamini kwamba ni kwa vile wote wanatoka ukanda mmoja? Naomba majibu ya hoja siyo kejeli na matusi.