Hivi Reginald Mengi ni CHADEMA?

Hivi Reginald Mengi ni CHADEMA?

Wana JF naomba mnisaidie kujua hili kwa uwazi pasipo matusi na kejeli...Kwanini Mtei alizindua kitabu chake cha "gother to governor" kwenye Hotel ya Mtei? Je tuamini kwamba ni kwa vile wote wanatoka ukanda mmoja? Naomba majibu ya hoja siyo kejeli na matusi.
Mods mngekuwa mnatimiza wajibu wenu na kuwa fair kwa hili jamvi letu, ujinga kama huu wa mleta mada usingeruhusiwa kudumu hata kwa dakika tano. Kwa kweli mnaonesha dharau kubwa kwetu wana JF...fikiria mtu anaingia humu kwa mara ya kwanza kabisa halafu anakutana na upuuzi kama huu ulioletwa na anayejiita Makusudically; bila shaka akitudharau ni halali yake. Makusudi hapa ya Makusudically ni kuishushia hadhi JF, nothing more nothing less!

CC:
Cookie, Mhariri, Active, Moderator
 
Mengi ni mnafiki sana, Hana uzalendo hata chembe, yeye anaangalia nani analinda maslahi yake tu! Ndio maana sasa anawatumia CHADEMA na wabunge wake kwenye ugomvi wake Binafsi na Prof.Muhongo.

Mkuu, Niambie Nani Mzalendo Kati Ya Mengi Na Muhogo?? Anadharau Na Kusema Watz Wana Hela Ya Juice Badala Ya Kutoa Mawazo Mbadara
 
Mimi Naona Itv Ndo Hamana Upendeleo Wowote, Naona Itv Ndo Iwe Televsn Ya Taifa
 
Mkuu, Niambie Nani Mzalendo Kati Ya Mengi Na Muhogo?? Anadharau Na Kusema Watz Wana Hela Ya Juice Badala Ya Kutoa Mawazo Mbadara

muhongo alimwambia lissu eti anauliza maswali ya form one.
Jamaa ni nunda,tundu lissu akapiga kimya.
 
  • Thanks
Reactions: R.B
Wana JF naomba mnisaidie kujua hili kwa uwazi pasipo matusi na kejeli.
Najua wazi kuwa Mengi kuwa mwanachama fulani cha Siasa siyo dhambi wsla kosa, lakini hoja yangu ni pale anapotumia fursa aliyo nayo kutumia vyombo vya habari kukashfu chama tawala, anatoa fursa kwa viongozi wa Chadema kutoa kashfa kwa vyama vingine na kuyapa muda mwingi sana matukano na kejeli hizo, mfano ITV hutangaza habari nyinngi sana za Chadema hususan ni zile za maneno ya wabunge wanaozungumza mambo ya kuiponda Serikali, Pia kuna tukio jingine nalo lilitushangaza Watanzania, Kwanini Mtei alizindua kitabu chake cha "gother to governor" kwenye Hotel ya Mtei? Je tuamini kwamba ni kwa vile wote wanatoka ukanda mmoja? Naomba majibu ya hoja siyo kejeli na matusi.

Vipi kuhusu TBC mali ya walipa kodi wote kupendelea chama kikongwe? Jaribu kuwa fair. Kama hupendi nawe wekeza kwenye habari uwape nafasi uwapendao
 
Mkuu, Niambie Nani Mzalendo Kati Ya Mengi Na Muhogo?? Anadharau Na Kusema Watz Wana Hela Ya Juice Badala Ya Kutoa Mawazo Mbadara

Mengi ukigusa Masilahi yake tu ndipo huwa Mkali saana lakini Mengi ni CCM amekulia CCM Mali zake zote kapata Akiwa CCM , aliifirisi NBC kwa mikopo ya Viwanda vya Revola,komesha nk Akiwa ccm,umiliki wa Utitiri wa Ma-tv ,maredio na magazeti kaupata Akiwa ccm,sisi Chadema siku tukiingia ikulu lazima tumkalize chini tumuhoji kwa Lugha ya kichaga Maana si mnajua hapa wote sie ni wachaga ,akina Zito na marehemu chacha tuliwakataa mapema, mengi ni ccm katajirikia ccm tu huku Chadema anajipendekeza tu
 
Mengi ni ccm ana kadi ya ccm tena anayo kadi ya TANU chama tawala kabla ya ccm ni mwanachama mkongwe wa ccm figisu figisu zake na Muhongo sasa kazilazimisha zije kwa Wananchi ili wamwonee Huruma, huwa anajua kucheza na watizamaji na wasililizaji wa Tv na Radio zake mpaka wanamwonea huruma na kuonekana anaonewa,anatumia pesa nyingi kusaka huruma ya wananchi huku wafanyakazi kwenye Kampuni zake wakilipwa mishahara midogo sana,Mengi ni ccm isipokuwa huwa anaamini ipo siku Chadema watazama mjengoni anahofia asipojipendekeza sisi Chadema tutamtoa nduki japo ni mchaga mwenzetu.
 
Vipi kuhusu TBC mali ya walipa kodi wote kupendelea chama kikongwe? Jaribu kuwa fair. Kama hupendi nawe wekeza kwenye habari uwape nafasi uwapendao

Hapa ni mwendo wa kila mtu kuvutia kwake TBC ni Tv ya Taifa walipaswa wa-balance wasipendelee ccm , Mengi kakomaa kukikomoa chama chake ccm si kwamba anakichukia saana Bali ni wana ccm wenzake wamemnyima Vitalu vya Gesi sasa kabuni Mbinu ya kuwakomoa kwa kujipendekeza huku Chadema ili na sisi Wachaga wenzake tumwonee huruma ,tunasema Chadema Hakuna huruma hata ufanyeje hata ukiwa mchaga mwenzetu Hakuna nafasi baki huko huko ccm Maana umetajirikia huko huko na ccm ndio wamekulea mpaka hapo ulipo sasa.
 
mtoa mada hukujpanga hoja haina mashko mbona huuliz tbc imegeuzwa ccmbc
 
kama chadema ni chama cha wachaga na mengi ni mchaga basi mpeni kaisari yaliyo ya kaisari. Ungeanza na tbc!

Ni kweli TBC nao wana mapungufu yao lakini si kigezo cha Mengi Ku-copy kila wanachofanya TBC ,si mnajua Mtu wetu Tido Mhando alijaribu Ku-balance kila Vyama Majanga yakamkuta, Mengi ni ccm damu lakini Masilahi Binafsi yanamfanya aweweseke na kujipendekeza Chadema lakini nina imani Mengi akipewa Vitalu vya Gesi kesho hutamsikia akijiteta Chadema atakaa Kiimya na Tv na Radio zake watakuwa Waki-balance Habari za vyama vyote.
 
Anashabikia Ccm, Na Sabodo Je Utasema Anashabikia Chama Gani??

Sabodo ni ccm machoni lakini Chadema moyoni,ni tofauti na Mengi ni ccm moyoni lakini ni Chadema machoni tu kwa nia ya kusaka huruma za wanachadema zimusaidie kwa masilahi yake Binafsi ,lakini akifanikiwa analudi ccm tu.
 
Si mlidai CDM ni chama cha wachaga?? Mengi ni mchaga, sasa sijui unalalamika nini?? Waachieni wachaga wajenge chama chao........................!!

Ni kweli Mengi ni mchaga na Chadema yetu ni Full uchaga kwa kwenda mbele,lakini tatizo linakuja Kuwa mengi ni ccm lakini anajaribu kusaka huruma za wanachadema zimusaidie kwa masilahi yake binafsi.
 
Uwiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiii jiulize kwann cdm inapotea?mchawi......
 
Mengi ni mnafiki sana, Hana uzalendo hata chembe, yeye anaangalia nani analinda maslahi yake tu! Ndio maana sasa anawatumia CHADEMA na wabunge wake kwenye ugomvi wake Binafsi na Prof.Muhongo.
Huu ndio Ukweli wenyewe yaani hakuna ubishi juu ya hili Mengi hana Uchungu na kero za jamii yeye anachojua ni kuyatetea masilahi yake kwa mbinu zozote Ikibidi hata kwa kukichafua chama chake CCM.
 
Back
Top Bottom