The unpaid Seller
JF-Expert Member
- Oct 27, 2019
- 1,876
- 5,443
Salaam,
Hapa nilikua nasikiliza hotuba ya waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa alipokua anazungumza na maafisa Mawasiliano wa mikoa, aise jamaa kamtaja rais zaidi ya mara 20.
Ndio kuna mahala katika hotuba kuna uhitaji wa kumtaja rais labda kuna maagizo au nukuu au kufanya rejea ya matukio nk ila jamaa anataja hata ambapo hamna logic katika mtiririko wa hoja wala umuhimu wa kumtaja.
Yani anaweza kua anaongelea jambo fulani afu ghafla tu "nampongeza rais mama yetu mpendwa mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama yetu mpendwa sana Samia Suluhu Hassan " . Yani mpaka hotuba inaisha kaitaja hiyo paragraph ya kumpongeza rais zaidi ya mara 20.
Na sio yeye tu ukichunguza mawaziri wakuu wa mikoa na wilaya wote wana huu utaratibu. Hili limekaaje ? au ndio woga, au kumjaza kichwa mama yetu, au ni kutojiamini, au vyote ?! Au ni nini?
Hapa nilikua nasikiliza hotuba ya waziri wa TAMISEMI, Innocent Bashungwa alipokua anazungumza na maafisa Mawasiliano wa mikoa, aise jamaa kamtaja rais zaidi ya mara 20.
Ndio kuna mahala katika hotuba kuna uhitaji wa kumtaja rais labda kuna maagizo au nukuu au kufanya rejea ya matukio nk ila jamaa anataja hata ambapo hamna logic katika mtiririko wa hoja wala umuhimu wa kumtaja.
Yani anaweza kua anaongelea jambo fulani afu ghafla tu "nampongeza rais mama yetu mpendwa mheshimiwa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama yetu mpendwa sana Samia Suluhu Hassan " . Yani mpaka hotuba inaisha kaitaja hiyo paragraph ya kumpongeza rais zaidi ya mara 20.
Na sio yeye tu ukichunguza mawaziri wakuu wa mikoa na wilaya wote wana huu utaratibu. Hili limekaaje ? au ndio woga, au kumjaza kichwa mama yetu, au ni kutojiamini, au vyote ?! Au ni nini?