Hivi Rais au Waziri Mkuu na Mawaziri wanatembelea ukurasa huu?

NANCA

Member
Jun 23, 2023
92
100
Hivi jamii forum ni ukurasa wa watu gani? Hivi Rais au Waziri mkuu na mawaziri wake wanatake time kutembelea ukurasa huu? Au wanadhani ukurasa huu ni wa wapiga kelele na upinzani? Hivi hawajui kua masikini wengi wasomi na wanaokandamizwa na wakoloni weusi ndo wako huku?

Hivi Rais hajui kua kitendo cha kutembelea Jamii forum japo kila siku kitamuwezesha kujua changamoto nyingi sana zinazowakumba watu wadogo na hatimae kuzitatua? Hivi hajui kua kwa kuutembelea ukurasa huu na kutatua changamoto zete kutamwezesha kua maarufu wa kweli hata kushinda uchaguzi 2025 bila hata kutumia nguvu.

Mimi nimshauri Rais Samia na jopo lake wajipe mda japo mara moja kila siku kutembelea jukwaa hili ili kuwafahamu wananchi wake. Badala ya kusafiri hata ulaya na kila kona duniani kututafutia mapesa bila kujua changamoto zetu ambazo zinaweza kutatuliwa bila mapesa hayo mapesa yanakua hayana maana sana.

Kama Rais anahangaika kutafuta mabilioni ili kujenga reli au barabara afu huku labda Kuna mbunge wake au mkurugenzi wake wanaendesha mchakato wa kunitapeli ardhi yangu hayo mapesa na mabarabara kwangu yanakua na maana gani?

Rais na waziri mkuu sisi kapuku mahala pa kuwapata nyie bila kikwazo ni huku mitandaoni na mahala pa heshima pa kuwapata nyie na kuwafikishia kero zetu ni hapa jamiiforum. Maana tukienda kwa wakurugenzi au wakuu wa wilaya na wa mikoa kwasababu wote wapo kiutafutaji na kiuzulumati basi matatizo yetu yanaishia kuwekwa kapuni ila hapa JF yanawekwa hadharani. Hivyo kwa kuingia hapa JF mtakua katika nafasi nzuri ya kutupatia haki zetu

Pia niwashauri JF muweke jukwaa maarum kwaajili ya high government officials ambapo hapo mtakua mnatupia malalamiko ya maana juu ya haki za watu yanayowalenga serikali kuu, na iwe ni page ambayo mtu hawezi post wala kukomenti ila ni nyie tu baada ya kuchuja lalamiko la mtu. Lisiwe jukwaa la kisiasa bali la malalmiko ya wananchi juu ya haki zao labda hapo serikali itaona kero zetu.

Binafsi nipo kwenye mapambano ya haki yangu ya ardhi na nipo njiani kwenda kumiona waziri wa ardhi, mkuu hadi rais. Ktk mapambano haya mkurugenzi na watu wake na huyo anaewatuma waamue kuniachia ardhi yangu au wanaipoteze vinginevyo sirudi nyuma hadi nazeeka na nazikwa. Ata sisi marofa Kama Kama wanavyotuita tunahaki ya kuandaa maisha bora ya wanetu.
 
Labda kutokana na majukumu tu ila wanapita vizuri tu na wanaperuzi kama kawa, kabla hajawa kiongozi wa umma walishawahi kuwa members kabla pitia hii platform
 
Yaani mpaka naenda mahakamani nimehakikisha rais na mawaziri wake husika ni mfumo Kama huu wa mkurugenzi na watu wake. Mimi ntaenda mahakamani kama ni mwananchi mwenzangu ndo anataka kunitapeli ila kama ni mbunge kwa kushirikiana na mkurugenzi na maafisa ardhi kamwe mahakama yangu itakua yule aliewachagua hadi hapo ntapojiridhisha kua lao ni moja ndo ntaenda kupoteza pesa na mda mahakamani kulinda haki yangu.
 
Itakuwa wapo hata kama mguu nje Kwa mguu ndani , asikilizwe mleta mada ardhi ya kurithi tamu kama mkate wanavyoula waliolithishwa uongozi Kwa namna nyingi.
Ungemjua wa kukushika mkono simu moja tu.
 
Hivi jamii forum ni ukurasa wa watu gani? Hivi Rais au Waziri mkuu na mawaziri wake wanatake time kutembelea ukurasa huu? Au wanadhani ukurasa huu ni wa wapiga kelele na upinzani? Hivi hawajui kua masikini wengi wasomi na wanaokandamizwa na wakoloni weusi ndo wako huku?

Hivi Rais hajui kua kitendo cha kutembelea Jamii forum japo kila siku kitamuwezesha kujua changamoto nyingi sana zinazowakumba watu wadogo na hatimae kuzitatua? Hivi hajui kua kwa kuutembelea ukurasa huu na kutatua changamoto zete kutamwezesha kua maarufu wa kweli hata kushinda uchaguzi 2025 bila hata kutumia nguvu.

Mimi nimshauri Rais Samia na jopo lake wajipe mda japo mara moja kila siku kutembelea jukwaa hili ili kuwafahamu wananchi wake. Badala ya kusafiri hata ulaya na kila kona duniani kututafutia mapesa bila kujua changamoto zetu ambazo zinaweza kutatuliwa bila mapesa hayo mapesa yanakua hayana maana sana.

Kama Rais anahangaika kutafuta mabilioni ili kujenga reli au barabara afu huku labda Kuna mbunge wake au mkurugenzi wake wanaendesha mchakato wa kunitapeli ardhi yangu hayo mapesa na mabarabara kwangu yanakua na maana gani?

Rais na waziri mkuu sisi kapuku mahala pa kuwapata nyie bila kikwazo ni huku mitandaoni na mahala pa heshima pa kuwapata nyie na kuwafikishia kero zetu ni hapa jamiiforum. Maana tukienda kwa wakurugenzi au wakuu wa wilaya na wa mikoa kwasababu wote wapo kiutafutaji na kiuzulumati basi matatizo yetu yanaishia kuwekwa kapuni ila hapa JF yanawekwa hadharani. Hivyo kwa kuingia hapa JF mtakua katika nafasi nzuri ya kutupatia haki zetu

Pia niwashauri JF muweke jukwaa maarum kwaajili ya high government officials ambapo hapo mtakua mnatupia malalamiko ya maana juu ya haki za watu yanayowalenga serikali kuu, na iwe ni page ambayo mtu hawezi post wala kukomenti ila ni nyie tu baada ya kuchuja lalamiko la mtu. Lisiwe jukwaa la kisiasa bali la malalmiko ya wananchi juu ya haki zao labda hapo serikali itaona kero zetu.

Binafsi nipo kwenye mapambano ya haki yangu ya ardhi na nipo njiani kwenda kumiona waziri wa ardhi, mkuu hadi rais. Ktk mapambano haya mkurugenzi na watu wake na huyo anaewatuma waamue kuniachia ardhi yangu au wanaipoteze vinginevyo sirudi nyuma hadi nazeeka na nazikwa. Ata sisi marofa Kama Kama wanavyotuita tunahaki ya kuandaa maisha bora ya wanetu.
Mama Samia anapitia humu na kupata madini kwa 100%.
Kuna mada nilitoa humu na aliishughulikia kama mwewe.
Asante mama.
 
Mama Samia anapitia humu na kupata madini kwa 100%.
Kuna mada nilitoa humu na aliishughulikia kama mwewe.
Asante mama.
Mwenye macho mazuri ni yule anaeona hadi kile kilichokidogo kabisa na kiongozi mzuri ni yule anaeona mambo madogomadogo sana ya watu wadogo sana maana ni makubwa sana kwa hao wadogo. Hivyo akiliona hili la kwangu pasi hapo atakua amefaulu kipimo changing cha uongozi na ajiandae kupewa zawadi ya kura 100 ktk sanduku la kura 2025 maana si ntakua na sbb yoyote tena ya kutokumpa karatasi langu.
 
Mwenye macho mazuri ni yule anaeona hadi kile kilichokidogo kabisa na kiongozi mzuri ni yule anaeona mambo madogomadogo sana ya watu wadogo sana maana ni makubwa sana kwa hao wadogo. Hivyo akiliona hili la kwangu pasi hapo atakua amefaulu kipimo changing cha uongozi na ajiandae kupewa zawadi ya kura 100 ktk sanduku la kura 2025 maana si ntakua na sbb yoyote tena ya kutokumpa karatasi langu.
Mama Samia ni msikivu na namsapoti sana.
Nilimlima sana wakati wa DP Weldi , lakini aliposahihisha mambo, aaah kama kawa
 
Fun fact is.. High official figures wanapitia hadi ule uzi wa kula tunda vizuri tu .
 
NANCA unalalamika badala ya kueleza tatizo lako la ardhi lipoje.

Muda uliyoutumia kulalamika ungekuwa umemaliza kuielezea changamoto yako.

Tuliza akili. Haki inaweza ikawa upande wako, lakini ukiwa na papara utaikosa.
 
NANCA unalalamika badala ya kueleza tatizo lako la ardhi lipoje.

Muda uliyoutumia kulalamika ungekuwa umemaliza kuielezea changamoto yako.

Tuliza akili. Haki inaweza ikawa upande wako, lakini ukiwa na papara utaikosa.
Kwann haki yangu afu niikose? Wakati wowote ntaanza ujenzi kwakua hakuna taarifa yoyote nliyopewa kwa kadri ya sheria ya utwaaji sura 118 fungu la 6 ambalo linataka taarifa rasmi kupewa muhusika kabla ya zoezi la utwaaji. Nimekua mpole sana sasa nachhkua hatua Kama watakuja kunisimamisha waje ila ntaendesha Jambo hili kisheria mahala ambapo hawajazingatia sheria ila ubabe ili kumpatia eneo langu mtu wanaemtaka basi mimi ntaendelea na ishu zangu.
 
NANCA unalalamika badala ya kueleza tatizo lako la ardhi lipoje.

Muda uliyoutumia kulalamika ungekuwa umemaliza kuielezea changamoto yako.

Tuliza akili. Haki inaweza ikawa upande wako, lakini ukiwa na papara utaikosa.
Taarifa inatakiwa itoke wiki 6 kabla ya zoezi tena itangazwe kwenye gazeti la serikali nia ya rais kutwaa eneo lako ili Kama unamalalamiko umuone waziri wa ardhi. Sasa hawa wahuni na genge lao wameitana eti Kuna mtu anayataka haya maeneo hvyo wamekuja kwa gia ya serikali direct to the site.
 
Taarifa inatakiwa itoke wiki 6 kabla ya zoezi tena itangazwe kwenye gazeti la serikali nia ya rais kutwaa eneo lako ili Kama unamalalamiko umuone waziri wa ardhi. Sasa hawa wahuni na genge lao wameitana eti Kuna mtu anayataka haya maeneo hvyo wamekuja kwa gia ya serikali direct to the site.
Umepeleka malalamiko kwao?
 
Umepeleka malalamiko kwao?
Kwa mkurugenzi, kwa mkuu wa wilaya na penginepo tena kwa barua lkn kote yapata miezi miwili kimya. Nkaandika tena kimya. Na nangojea barua zao ili iwe kiambata siku za mbeleni.
 
Umepeleka malalamiko kwao?
Kuna mtu mmoja mkubwa yeye ni mroho wa maeneo hata ya watu na anatabia ya kuyachukua kibabe, au kwa lazima utamuuzia au anatumia njia za panya za kiserikali kwa kushurutisha mamlaka zitwae kimabavu bila kufuata taratibu za kisheria za utwaaji ili apate maeneo hayo. Sasa mimi Kama mimi naona Kama watapata ugumu hivi maana sijawai onea mtu ktk chake na wala sitaki kuonewa na kupelekeshwa
 
Taarifa inatakiwa itoke wiki 6 kabla ya zoezi tena itangazwe kwenye gazeti la serikali nia ya rais kutwaa eneo lako ili Kama unamalalamiko umuone waziri wa ardhi. Sasa hawa wahuni na genge lao wameitana eti Kuna mtu anayataka haya maeneo hvyo wamekuja kwa gia ya serikali direct to the site.
Sisi Nkuhungu broad acre dodoma Waziri katuambia kwenye uvamizi Kuna Wavamizi halali na Wavamizi pandikizi na kuwa Wavamizi halali atawapa maeneo yetu yenye miliki

Sasa tunajiuliza
Waziri anasema Mama Samia katoa maelekezo Wavamizi nao wapewe ndani ya miliki zetu!

Kwanini asitumie Sheria inayo mruhusu kutwaa maeneo yetu ijulikane moja kuepusha ujanja wa Mafuru na genge lake linalo ongozwa na Magige kupora maeneo yetu

Kwanini Wavamizi wasiwajibike mojakwa moja Kwa mmiliki halali wa Eneo
Maana kumeshakitokeza watu wanajiita toka CCM wanawakingia vifua Wavamizi kwamba wanaenda kupewa na chama maeneo yetu Bure!!

Waziri naamini ni mwanasheria msomi hili la Wavamizi halali na Wavamizi pandikizi limekaaje
Mbona Waziri pale Itega block T no 1,2&3 tumeona unatoa maamuzi sahihi ya kisheria Ndachi kunashida Gani?!!!
 
Back
Top Bottom