Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 15,262
- 9,714
Ndugu zangu Watanzania,
Napenda kuwafahamisheni ya kuwa Rais wetu mpendwa na jemedari wetu Dkt Mama Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita,nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge hii leo amefanya maamuzi mazito na magumu sanaaa.
kwa kutoa kwa mkono wake mwenyewe na kauli yake mwenyewe Helikopta ya kuwapeleka mawaziri wa ujenzi Mheshimiwa Innocent Bashungwa pamoja na naibu waziri wa TAMISEMI, ili waweze kufika kwa haraka sanaa liwale mkoani Lindi kutatua na kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya miundombinu ambayo imeharibika ikiwepo kubomoka kwa madaraja pamoja na kujaa maji kwenye barabara.
Mawaziri hao ambao wametua kijeshi mithiri ya mashujaa na makomandoo waliotumwa na Marekani nchini Pakistani kumnasa Gaidi namba moja Duniani Osama Bin ladeni ,waliambatani na mkuu wa mkoa wa Lindi Mheshimiwa Zainabu,wataalamu kutoka TANROADS pamoja na TARURA.
Mheshimiwa Rais anafanya haya yote kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila sehemu katika ardhi ya Tanzania inapitika na kufikika muda wote na wananchi wanasafiri kutoka eneo moja kwenda jingine bila shida ya aina yoyote ile.hii ndio maana ya uongozi na kiongozi jasiri na shupavu.huu ndio maana ya Rais Samia kuitwa komandoo na jemedari wa vita.maana muda wote ni mtu wa maamuzi makini na weledi.
Rais Samia Ni mpango wa Mungu Mwenyewe aliyeinuliwa kwa mkono wa Mungu Mwenyewe kuwatumikia watanzania wanyonge wanaohitaji msaada. Ni kiongozi msikivu na mnyenyekevu sana.ndio maana kwa usikivu wake na kuwajali Watanzania sasa anakwenda kuanzisha utaratibu wa kumsikiliza mtanzania mmoja mmoja mwenye kero binafsi.
Hii maana yake ni kuwa Rais Samia anaijali hata sauti ya mtu mmoja tu,anathamini na yupo tayari kutumia muda wake kumsikiliza mtu mmoja mwenye kero au changamoto ya aina yoyote ile.anataka kila mtu katika Taifa letu ajione ana nafasi ya kusikilizwa mbele ya Rais wake.anataka watanzania wajuwe kuwa kura yako ya ndio kwa Rais Samia na CCM yake inakupa tiketi na fursa ya kuzungumza na mkuu wa nchi bila kikwazo cha aina yoyote ile.
Hii ndio maana ya kauli yangu kuwa Rais Samia Ametufikia Watanzania kwa utumishi wake.maana hakuna mtu au mtanzania atakaye achwa nyuma au kutokusikilizwa kero yake.watanzania wenzangu tuendelee kuwa na imani kubwa sana kwa Rais wetu na mama yetu mpendwa anayetupenda sana Watanzania.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.
Napenda kuwafahamisheni ya kuwa Rais wetu mpendwa na jemedari wetu Dkt Mama Samia Suluhu Hasssan mama wa shoka, chuma cha Reli, shujaa wa Afrika, jasiri muongoza njia, simba wa nyika, komandoo wa vita,nyota ya matumaini na nuru ya wanyonge hii leo amefanya maamuzi mazito na magumu sanaaa.
kwa kutoa kwa mkono wake mwenyewe na kauli yake mwenyewe Helikopta ya kuwapeleka mawaziri wa ujenzi Mheshimiwa Innocent Bashungwa pamoja na naibu waziri wa TAMISEMI, ili waweze kufika kwa haraka sanaa liwale mkoani Lindi kutatua na kutafuta ufumbuzi wa changamoto ya miundombinu ambayo imeharibika ikiwepo kubomoka kwa madaraja pamoja na kujaa maji kwenye barabara.
Mawaziri hao ambao wametua kijeshi mithiri ya mashujaa na makomandoo waliotumwa na Marekani nchini Pakistani kumnasa Gaidi namba moja Duniani Osama Bin ladeni ,waliambatani na mkuu wa mkoa wa Lindi Mheshimiwa Zainabu,wataalamu kutoka TANROADS pamoja na TARURA.
Mheshimiwa Rais anafanya haya yote kwa lengo la kuhakikisha kuwa kila sehemu katika ardhi ya Tanzania inapitika na kufikika muda wote na wananchi wanasafiri kutoka eneo moja kwenda jingine bila shida ya aina yoyote ile.hii ndio maana ya uongozi na kiongozi jasiri na shupavu.huu ndio maana ya Rais Samia kuitwa komandoo na jemedari wa vita.maana muda wote ni mtu wa maamuzi makini na weledi.
Rais Samia Ni mpango wa Mungu Mwenyewe aliyeinuliwa kwa mkono wa Mungu Mwenyewe kuwatumikia watanzania wanyonge wanaohitaji msaada. Ni kiongozi msikivu na mnyenyekevu sana.ndio maana kwa usikivu wake na kuwajali Watanzania sasa anakwenda kuanzisha utaratibu wa kumsikiliza mtanzania mmoja mmoja mwenye kero binafsi.
Hii maana yake ni kuwa Rais Samia anaijali hata sauti ya mtu mmoja tu,anathamini na yupo tayari kutumia muda wake kumsikiliza mtu mmoja mwenye kero au changamoto ya aina yoyote ile.anataka kila mtu katika Taifa letu ajione ana nafasi ya kusikilizwa mbele ya Rais wake.anataka watanzania wajuwe kuwa kura yako ya ndio kwa Rais Samia na CCM yake inakupa tiketi na fursa ya kuzungumza na mkuu wa nchi bila kikwazo cha aina yoyote ile.
Hii ndio maana ya kauli yangu kuwa Rais Samia Ametufikia Watanzania kwa utumishi wake.maana hakuna mtu au mtanzania atakaye achwa nyuma au kutokusikilizwa kero yake.watanzania wenzangu tuendelee kuwa na imani kubwa sana kwa Rais wetu na mama yetu mpendwa anayetupenda sana Watanzania.
Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Kijana mzalendo na mpenda nchi yangu.