Rais Samia nimekuangukia mguuni, keki ya birthday yako mpe Thadei Ole Mushi uokoe uhai wake

Gilbert A Massawe

JF-Expert Member
May 14, 2015
4,686
3,398
RAIS wangu Samia Suluhu Hassan, kwa unyenyekevu mkubwa mama yetu mpendwa, leo ni siku yako ya kuzaliwa. Keki zimekatwa kila mahali nchi nzima kukusherehekea. Hongera sana Rais Samia kwa miaka aliyokuruhusu Allah uendelee kuishi na kuvuta pumzi chini ya jua. Hiyo ni zawadi ya Mungu.

Lakini mama yetu yupo kijana wako, Thadei Ole Mushi ambaye anaishi kwa kutumia mashine hapa KCMC. Moyo wake una-fail kufanya kazi. Ukichomoa tu ile mashine baada ya dakika 20 Ole Mushi atakuwa amefariki. Chumba alicho ninaambiwa ni zaidi ya ICU. Huduma ya kumponya ni Aircraft Ambulance kumpeleka Nairobi ili aokolewe roho yake.

Rais Samia, unaweza kujiuliza Ole Mushi ni nani hasa? Ni wachache sana nchi hii watumiaji wa mitandao ya kijamii wasimjue Thadei Ole Mushi. Huyu ni kada wa kindaki-ndaki wa CCM. Ole Mushi ni muibuaji wa mada na mijadala anuai iliyoisaidia sana CCM akiwa ni Mwalimu kitaaluma. Katika mgogoro wa mkataba wa Bandari na DP World Ole Mushi alisimama na wewe mwanzo mwisho. Maandiko ya Ole Mushi kwa CCM hakuna mwenye shaka nayo.

Ole Mushi moyo umesimama. Anaishi kwa msaada wa mashine hapa KCMC. Msaada ni ama amepelekwe India au Nairobi. Mawaziri wako Ridhiwan Kikwete, David Kihenzile, Dotto Biteko (NW/Mkuu) wametoa msaada wa Hali na mali kasoro Waziri Ummy Mwalimu aliyeshindwa kufanya nafasi yake kama wizara.

Nakusihi Mama yetu sema neno moja kada mwenzetu apone. Ole bado ni kijana na mchango wake kwa Taifa ni mkubwa sana. Walimu wa CWT walipojaribu kukudhalilisha kwa uteuzi wako Ole Mushi alisimama na wewe. Mama mpe keki ya Uhai Ole Mushi naye aishi kukumbuka birthday yako.

Vijana wa upinzani wanavumisha uongo wa kukataa kumchangia Ole Mushi kwamba alipewa sumu na watu wa "mfumo" kwamba afe. Kwamba "mfumo" utafurahi akifa. Hii kashfa mbaya Kwa chama chetu. Mama yetu okoa kwanza maisha ya Thadei Ole Mushi kwa kila unaloweza kufanya kama raia namba moja nchi.

Itakuwa ni faraja ukimpigia wewe mwenyewe mke wa Thadei Ole Mushi kupitia simu namba 0714 742 243 au 0620 300000 Victor Tesha ambaye ndiye yuko pembeni mwa kitanda alikolazwa Thadei Ole Mushi ambaye ameishi na tatizo la moyo kwa muda mrefu bila kujua.

Kama mwenye upendo na utu, sambaza ujumbe huu kadri uwezavyo Hadi umfikie mama yetu Samia Suluhu Hassan na huo unaweza kuwa mchango wako. Tumuombee Thadei Ole Mushi.
27/1/2024

Mungu Amlinde Thadei
 
Huyu ni kada wa kindaki-ndaki wa CCM. Ole Mushi ni muibuaji wa mada na mijadala anuai iliyoisaidia sana CCM akiwa ni Mwalimu kitaaluma. Katika mgogoro wa mkataba wa Bandari na DP World Ole Mushi alisimama na wewe mwanzo mwisho.

MTU MWALIMU HANA TAALUMA YA SHERIA ANAJUAJE MAMBO YA MIKATABA HUU NI UKUDA ILA ANYWAY KWA KUWA NI MGONJWA BASI ASAIDIWE
 
Huyu ni kada wa kindaki-ndaki wa CCM. Ole Mushi ni muibuaji wa mada na mijadala anuai iliyoisaidia sana CCM akiwa ni Mwalimu kitaaluma. Katika mgogoro wa mkataba wa Bandari na DP World Ole Mushi alisimama na wewe mwanzo mwisho.

MTU MWALIMU HANA TAALUMA YA SHERIA ANAJUAJE MAMBO YA MIKATABA HUU NI UKUDA ILA ANYWAY KWA KUWA NI MGONJWA BASI ASAIDIWE
Majority wako against na DP ila Mushi amesimama na wewe kwenye mkataba. Mungu amponye japo ni CHAWA mwandamizi
 
Ila mimi huwa nachukia nikikutanaga na campaigns mitandaoni za kumsaidia mtu fulani 'maarufu' anaeugua. Najiuliza hivi kuna watu wangapi wanaougua na hakuna mtu hata anaewakumbuka bali ni familia zao zinahangaika tu.

Kwanini akiugua mtu 'maarufu' ndio watu hutumia nguvu kubwa kuhamasisha achangiwe/asaidiwe? Kwanini msitumie nguvu hizo kushinikiza serikali iboreshe sekta ya afya (BIMA) ili kila mwananchi aweze kupata matibabu?
 
Mambo mengine ni bora madokta waelezee mgonjwa anasumbuliwa na nini hasa, kuliko kusikiliza na kuamini maelezo ya ndugu, jamaa na marafiki kabla ya kumchangia mgonjwa.

Ombi ni la jumla mno utadhani magonjwa yote ya moyo yanafanana, for all we know kuna ‘heart failure’, kutokana na maelezo. Lakini hakuna sababu imesababishwa na nini in details.

Mgonjwa mwenyewe kwa sasa tunaambiwa bila ya mashine anapotea and that is serious health deterioration stage inaweza kuwa beyond repair hata apelekwe hospitali gani duniani.

Mara nyingi katika situation kama hizo ndugu huwa awataki kuelewa, wao wana amini labda kwengine inawezekana awataki kukubali matokeo.

Busara ni hospitali kutoa maelezo ya condition ya mgonjwa ili jamii ipate elimu na kuamua kuchangishana au vipi kutokana na uhalisia.

Ushaanza kulaumu baadhi ya viongozi kumtupa, wakati kuna wastaafu kibao wenye matatizo ya moyo matibabu yao yanafanywa Tanzania. Hizo ni dalili tosha za hasira na kukataa uhalisia wa mazingira halisi na situation. Sasa hatujui uhalisia gani mwingine wa medical advise hamtaki kuelewa.

Ni bora hospitali itoe maelezo au daktari, kuliko hizi general accusations.
 
Mambo mengine ni bora madokta waelezee mgonjwa anasumbuliwa na nini hasa, kuliko kusikiliza na kuamini maelezo ya ndugu, jamaa na marafiki kabla ya kuchangia mgonjwa.

Ombi ni la jumla mno utadhani magonjwa yote ya moyo yanafanana, for all we know kuna ‘heart failure’, hakuna maelezo imesababishwa na in details.

Mgonjwa mwenyewe kwa sasa tunaambiwa bila ya mashine anapotea and that is serious health deterioration stage inaweza kuwa beyond repair hata apelekwe hospitali gani duniani.

Mara nyingi katika situation kama hizo ndugu huwa awataki kuelewa wana amini labda kwengine inawezekana awataki kukubali matokeo.

Busara ni hospitali kutoa maelezo ya condition ya mgonjwa ili jamii ipate elimu na kuamua kuchangishana au vipi kutokana uhalisia.

Ushaanza kulaumu baadhi ya viongozi kumtupa, wakati kuna wastaafu kibao wenye matatizo ya moyo matibabu yao yanafanywa Tanzania. Hizo ni dalili za hasira na kukataa uhalisia wa mazingira halisi na situation; sasa hatujui uhalisia gani mwingine wa medical advise hamtaki kuelewa.

Ni bora hospitali itoe maelezo au daktari, kuliko is general cries.
Ana waalaumu wapinzani pia humo

Ova
 
Kigezo hapa ni kada kindaki ndaki. Na sio utanganyika wake. Hakika.kwa tusio na vyama imekula kwetu. Sawa KIZIMKAZI Yuko bze na cku yake ya kuzaliwa huku taifa likiwa GIZANI na hakuna sukari pamoja na kua kilo moja ni 4500.
 
Ana waalaumu wapinzani pia humo

Ova
Ukisoma kwa makini ni andiko la kutoka kwa mtu wake wa karibu ambae anasumbuliwa na ‘emotional distress’ hataki kukubali situation ndio maana he is all over the place.

Sihitimishi kwamba situation ya jamaa ndio ntolee tena achomoki, ila mambo kama hayo kwenye jamii ukiambiwa uchangie matibabu ni vyema ukasikia upande wa medics pia.

Shida ya nchi yetu hatujafikia bado hatua za kutengeneza policies/services za ‘holistic care approaches’, kwa wagonjwa pamoja na jamaa zao wa karibu kwenye maswala ya ‘significant life events’ and ‘end of life care’.

Hakuna support system ya ndugu hasa partner kwenye kwenye maswala ya ‘bereavement support’ on how to accept the situation and cope.

The funny thing nishawawekea module zote za hayo mambo humu ndani, wao wanadhani ni li pdf tu la hovyo; wakati hilo lina cover kila kitu utakachofundishwa maswala ya ‘health and social care management’ kuanzia diploma, mpaka masters. Wao ni upuuzi tu mwingine wa JF.
 
TAARIFA KUHUSU HALI YA RAFIKI YETU THADEI MUSHI

Tunayo furaha kuwajulisha kuwa hali ya kiafya ya rafiki yetu Thadei inaendelea vizuri. Tunasubiri taratibu za hospitali atakayoenda zikamilike ili tuweze kumsafirisha wiki hii hapa.

Tunapenda kuishukuru kwa dhati kila mmoja wenu aliyechangia, kupiga simu kumjulia hali, na kumtembelea mgonjwa. Tunaomba Mwenyezi Mungu awabariki sana.

Shukrani za kipekee ziwaendee viongozi wetu wa kiserikali, akiwemo Mheshimiwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Dotto Biteko, Waziri wa Afya Ummy Mwalimu, Naibu Waziri wa Uchukuzi David Mwakiposa Mhenzi, na Naibu Waziri wa Utumishi Ridhiwan Kikwete.

Pia, tunawashukuru madaktari na wauguzi wote mnaojitolea kwa moyo kumhudumia Thadei, mkiongozwa na Dk. Masenga, Kiongozi wa KCMC.

Tunawapongeza wana-KS kwa michango yenu inayoendelea kuchangia. Mungu awabariki sana.

VT.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom