Hivi Mengi ni Team Lowassa?

Hivi Mengi ni Team Lowassa?

Hana tofauti na wale walioipa CHADEMA mwaka mmoja itakuwa imeshakufa.mwaka umekatika,ndio kwanza CHADEMA inazidi kuchanja mbuga na sasa inakwenda kutinga Ikulu chini ya UKAWA.

Mkuu kuhusu haya nenda kwenye uzi husika
 
Mkuu meningitis, wewe ndio hujui!, wenzako wenye akili, wameisha soma upepo, yule 'jamaa yangu' ndie rais wetu 2015 ndani ya CCM au nje ya CCM!. Hivyo jamaa is right!.

Pasco
Anaweza kuwa right lakini hiyo haindoi dhambi ya asili ya unafiki.Jiulize kwa nini Rostam haitwi mnafiki?Jibu ni rahisi tu always yuko upande aliouamini no matter what.Huyu jamaa yetu ni mfuata upepo tena kwa kujidai yuko upande wa wanyonge...shame.

KKuhusu jamaa kuukwaa nje ya ccm ameshachelewa ....ameshapoteza fursa akiwa Shekh Amri Abeid siku ilee aliyotakiwa kufunguka ....siku ile aliyoandaliwa na kibonde ndio ilikuwa one moment one opportunity one bullet and one shot to make.
 
Kuna bwana mmoja mjanja mjanja sana na anapenda kutumia vyombo vyake vya matangazo ikiwa ni pamoja na TV,Radio na magazeti.

Ni mjanja sana wa kukimbilia media pindi anapobanwa kwa hoja.

Ni mnafiki kwelikweli na ametumia makundi ya kijamii yenye shida kujijengea umaarufu asiostahili.

Amejidai ni mwenye nguvu ya media yenye uwezo wa kuangusha serikali!

Amewalaghai hata chadema kwa kujidai kurusha mikutano yao.


Ni mlaghai mno na mjanja sana wa kufuata upepo.

Ninachomuhurumia ni kwamba mwaka huu amaingia pabaya(wrong turn)

Kosa la kujiunga na kambi ya kifisadi ni kosa atakalojutia maishani kwani kwa mara ya kwanza ATASHINDWA na hapo ndio itakuwa kikomo cha UNAFIKI wake.


Bado majuma kama mawili tu kitaeleweka.

Unakokwenda hauko sahihi.
Chama cha Mapinduzi kinamilikiwa na watu milioni saba waliojiwekea utaratibu wao
wa kupata wagombea wa nafasi za uongozi katika nchi yetu.
Nafasi ya Urais, kwa utaratibu wa CCM, wagombea hujadiliwa na Kamati Kuu.
Nimemsikia mwalikwa wa Dar kwenye Star tv akilalama kunyimwa nafasi ITV kuwajadili watia nia.
NAWAPONGEZA SANA ITV. Nawapongezapia Star tv kwa kutimiza matakwa ya kimaadili ya vyombo vya habari.
Hakuna mwanaCCM mwenye mamlaka ya kunyakua au kubaka mamlaka ya CC-CCM.
Mmejiuliza kuwa huyo mgombea mnayeshirikiana naye kutishia Watanzania kuwa watahama nchi
ataishije kama hatakuwa mgombea wa CCM?
Kama hamkubaliani na utaratibu wa CCM, uwanja hapa Tanzania ni mpana sana.
Acheni kuwatisha Watanzania.
 
Anaweza kuwa right lakini hiyo haindoi dhambi ya asili ya unafiki.Jiulize kwa nini Rostam haitwi mnafiki?Jibu ni rahisi tu always yuko upande aliouamini no matter what.Huyu jamaa yetu ni mfuata upepo tena kwa kujidai yuko upande wa wanyonge...shame.

KKuhusu jamaa kuukwaa nje ya ccm ameshachelewa ....ameshapoteza fursa akiwa Shekh Amri Abeid siku ilee aliyotakiwa kufunguka ....siku ile aliyoandaliwa na kibonde ndio ilikuwa one moment one opportunity one bullet and one shot to make.

Mkuu kwa hiyo kosa lake ni kurusha habari za Lowasa?
 
Kuna bwana mmoja mjanja mjanja sana na anapenda kutumia vyombo vyake vya matangazo ikiwa ni pamoja na TV,Radio na magazeti.

Ni mjanja sana wa kukimbilia media pindi anapobanwa kwa hoja.

Ni mnafiki kwelikweli na ametumia makundi ya kijamii yenye shida kujijengea umaarufu asiostahili.

Amejidai ni mwenye nguvu ya media yenye uwezo wa kuangusha serikali!

Amewalaghai hata chadema kwa kujidai kurusha mikutano yao.


Ni mlaghai mno na mjanja sana wa kufuata upepo.

Ninachomuhurumia ni kwamba mwaka huu amaingia pabaya(wrong turn)

Kosa la kujiunga na kambi ya kifisadi ni kosa atakalojutia maishani kwani kwa mara ya kwanza ATASHINDWA na hapo ndio itakuwa kikomo cha UNAFIKI wake.


Bado majuma kama mawili tu kitaeleweka.

Sio yeye tu. Ni wanafiki wengi kabisa wataumbuliwa mwaka huu. Kuna wale mabingwa wa kusoma upepo unavyovuma ili wajichanganye kwenye msafara. Wote mwaka huu wanaumbuka kwani ''wa mbele watakuwa wa mwisho na wa mwisho watakuwa wa mbele''
 
ID yenyewe feki na bado unaogopa acha unafiki na uchimvi bana. Hapa tunajenga taifa
 
Taja huyo mtu unaleta mada za mafumbo ngumu watu kukuelewa.

Halafu unakumbuka ule uzi wako ulisema unawapa mwezi ACT-Wazalendo itasambaratika muda mbona umepita.

Teh teh teh

Teh teh atakua mpiga ramli hasi
 
Mkuu meningitis, wewe ndio hujui!, wenzako wenye akili, wameisha soma upepo, yule 'jamaa yangu' ndie rais wetu 2015 ndani ya CCM au nje ya CCM!. Hivyo jamaa is right!.

Pasco

Ni bora awe rais wenu 2015,tunamuomba Mungu usiku na mchana atuepushie hili balaa ili isije ikatokea akawa rais wa Tanzania ili tusije tukalia kilio cha mamba.
 
Kwa kweli hata mimi Mengi kanishangaza sana,katika watia nia wote yeye ni Lowasa tu,mpaka amempiga marufuku Mkinga kwenye media zake kisa anamsema sana Lowasa.kama unampenda sana Lowasa itisha mdahalo na Lipumba tuone

Leo makamanda mmemgeuka Mengi tena
 
Reginald Mengi fisadi papa
Rostam Aziz fisadi nyangumi

Wameunganishwa na fisadi mkuu , kubwa la maadui Edward lowasa , jamani tuwe serious hii nchi inaendwa kutafunwa na mafisadi waliolenga gas yetu
 
Kwani huyo mtu hana haki ya kuwa mwnanachama wa chama fulani au ni lazima awe Mwana CDM
 
wezi na matajiri wanaungama ili mtu wao aingie madarakani wakagawane vitaru vya gesi,
mengi chenge,rostamu,karamagi,tibaijuka na wengine wengi sana ,na kile kibeberu kidogo kisaliti na kinafiki zotto
 
Huy unaye mwita mnafik ubaya wake ni kuwa karib na kina Lowassa au ni nn hasa, na kama hamtaki mtu mwema kuw karb na mkosaji ss mnafikiri atabadilikaje! Kwny iman yang hat Yesu Kristo alikula meza moja na wasio haki! Kila mtu yuko na freedom of choice, unafiki wa watu wanaujua wenyew, hata mtoa mada vilevile unaweza ukawa mnafik pia cjasema Mengi ni mwema inawezekana akawa mnafiki pia japokuwa cna uhakika
 
Mengi ni sawa na akina Gwajima kwani wanafuata upepo. Mengi alishawahi mponda sana Lowassa na kumpongeza sitta lakini kwa sasa lowassa kwake ni lulu. Gwajima na Mengi n walewale.

Unajua maana ya neno fursa watu wenye akili za ki biashara wanalijua vizuri hilo neno, if u can't fight me join me.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom