Mkuu Meningitis, kusema ukweli kuna vitu vingine huwa vinasemwa tuu kwa madhumuni ya kitu kinachoitwa 'power consolidation', yaani kwa vile Mzee Mengi is a very powerful man, mtu yoyote mwenye kutafuta uongozi for the sake of gaining the powers, lazima atafanya alliances na the powerful ones, na hata asipofanya yeye, the hao 'the powerful ones' watamfuata kutaka alliances kwa sababu in politics, you never know atakuwa nani, hivyo ukijialign mapema you are safe na hivyo ndivyo wanavyofanya wafanya biashara wote wakubwa!.
Hebu fikiria jinsi Mengi na Rostam walivyotukanana kwenye ile vita ya Fisadi Papa na Fisadi Nyangumi!, halafu juzu hapa watu hawa wamekumbatiana hadharani na kukaa meza moja!.
Nijuavyo mimi Mzee Mengi ni kada wa CCM na yuko huru kumuunga mkono mtia nia yoyote na kumsupport kwa hali na mali bila kukiuka kanuni yoyote, ila pia nawajua baadhi ya makada wa CCM, (ukimuondoa Sabodo ambae ameisupport Chadema wazi wazi) wanaoisupport Chadema kwa siri!.
Kwenye politics hakuna urafiki wa kudumu wala uadui wa kuduma kuna urafiki tuu wa ki maslahi tuu, hivyo utashangaa hizo team Lowassa, team Membe team sijui nani, mgombea akiishapatikana zote zinakuwa kitu kimoja kumsupport!, kambi zote zinavunjwa, inatengenezwa kambi moja kubwa inayoitwa "the winning coalition", watu wanatinga tena ikulu kama kawa!.
Pasco