sasa wewe unaelezea kitu ambacho yeye hajasema Hayo uliyoandika sio kwa mke tu kuna Bond ukishatengeneza Na mtu ile ya mwanzo inaondoka.
Yeye anasema akishamla tu basi anaanza kumdharau na Kumuon wa kawaid tu ndio nikamwambia tendo halondoi thamani bali linaongeza labda tu kama hakukuwa na hisia ulisukumwa na mihemko au ulikuwa unatafuta ushindi au kama unaona Kumla mwanamke n jambo kubwa sana la kifahari yaani ni sehemu ya mafaniko yako
Mtazamo wake upo hivyo na yuko hivo (yeye) lkn haindoi kumchukulia wa KAWAIDA hata kama ni mke wako!
Sikia mimi kipindi nataka kuoa nilikua nikipata mwanamke nikidumu nae tu kwenye mahusiano (hata bila ngono) namuona wa kawaida sana kisha nasema sasa huyu namuona hana maajabu nitawezaje kuishi naye maisha yote ikiwa tu kwa sasa naona kabisa kama ananichosha?
Uzuri nilimwambia bibi yangu upande wa mama hiki ninachopitia....kisha nikamuuliza na mzee wangu majibu yalilingana.
Siku moja nasikiliza tena masomo ya ndoa kutoka kwa mchungaji wa kisabato anaitwa David mmbaga naye alichokisema ni kilekile nilichoambiwa na bibi na baba!
Kuna mchungaji mwingine mzungu wa marekani naye ni msabato jina somebody finely la mwanzo nimesahau katika mafundisho yake sijui kama alikuwa anahubiri au alikuwa na mkutano hukohuko kwao USA alimtolea mdano mke wake kuwa aliwahi kumuuliza kwanini kipindi unaniposa na sasa si kama hapo awali.....jamaa alisema nilimuhurumia mke wangu nikamtazama kwa upole kisha nikamwambia ukweli kuwa sisi ndivyo tulivyo kwa sasa nakuona kama mama yangu nakupenda kama mama pole na nielewe(naweza kukoswa kiswahili sahihi cha kuandika kama alivyosema maana ni mzungu ila maana yake inakuja hivyo ukitaka kumwambia mtu kwa kiswahili aelewe)
Baada ya mimi kuoa tena binti alikuwa mdogo akiwa bado..... lkn hakutoboa miezi 3 nikamuona wa kawaida tu japo kwa wengine ni tishio hadi leo!
Sisi tunao fuga mifugo mambo yako hivyo tena iwe kwenye kuku ukileta koo majogoo yatafukuzana mnoo.
Nenda shuleni akihamia msichana awe mzuri au wa kawaida si walimu si wanafunzi walikuwa wanafukizia vibaya mno ila baada ya muda ilikuwaje?
Nahitimisha kwa kukwambia kipya I kipya na kikukuu si kama kipya la hasha!