Hivi dini zingine hawaruhusiwi kuchinja?

Hivi dini zingine hawaruhusiwi kuchinja?

Tatizo siyo Kuchinja , Tatizo unachinja kwa ajili na kusudio lipi , China kwa Jina la Mola wetu ???
 
Kwa sisi tunaopenda nyuma ya porini!

Nyati au Mbogo huchinjwa na nani Mara anapopigwa risasi na muwindaji?
 
Tatizo siyo Kuchinja , Tatizo unachinja kwa ajili na kusudio lipi , China kwa Jina la Mola wetu ???
Mola wenu na Mungu kuna utofauti wowote, au wenu anahusika zaidi na kitengo cha uchinjaji? Mimi nachinja mwenyewe, hats ukichinja we we hainiathiri chochote, unaweza kunipa madhara ya kula nyama isiyochinjwa kwa jina la Mola wako?
 
Mola wenu na Mungu kuna utofauti wowote, au wenu anahusika zaidi na kitengo cha uchinjaji? Mimi nachinja mwenyewe, hats ukichinja we we hainiathiri chochote, unaweza kunipa madhara ya kula nyama isiyochinjwa kwa jina la Mola wako?
Mkuu ukinialika nitaishia kula pilau na mlenda.
 
Wakati wa mgogoro wa kuchinja kule mwanza tungu zetu waislam waliulizwa watoe iyo aya kutoka kwenye quaran inayozuia wa kristo kuchinja nasikia ikashindikana japo sina uhukakika na hiyo habari, hebu mwenye aya atupatie.
 
Wakati wa mgogoro wa kuchinja kule mwanza tungu zetu waislam waliulizwa watoe iyo aya kutoka kwenye quaran inayozuia wa kristo kuchinja nasikia ikashindikana japo sina uhukakika na hiyo habari, hebu mwenye aya atupatie.
Hakuna aya kama hiyo chaumbile imulungu ni cha kumemena kinacho takiwa ni Shukrani kwa Mungu wetu
 
Hakuna dhehebu linalokatazwa kuchinja.
Yesu alipokuja pazia la hekalu lilipasuka,kila kitu tumekabidhiwa.

Ndugu usifunguwe nira na wasio amini,vigeu geu eti wachinje wao ila wale nyama ,huko ni kujipendekeza kwa shetani na hakuna tija yeyote ile.

Mpaka mkuu mmoja wa mkoa tena mpendwa aliyeokoka anatoa fedha yake kusaidia ujenzi wa hekalu la Shehe -wa-Baali,thats nonsense!
 
Mkuu usihofu, kwenye mshuko nakuita unachinja wewe, sisi sote ni ndugu, hizi dini tumeletewa haziwezi kuvunja uhusiano wetu.
Mkuu lazima nitie timu mboka krismasi hii,walwa lisikosekane tu, si unajua tena..ila mkuu mimi ninakawaida walwa likikolea huwa naanza kuimba univumilie tu mkuu.
 
Karibu mboka mkuu, ila kuwa makini maeneo ya stendi ukifika unitaarifu wasije watoto wa ng'ambu wakakuibia mabegi yako.
 
Mola wenu na Mungu kuna utofauti wowote, au wenu anahusika zaidi na kitengo cha uchinjaji? Mimi nachinja mwenyewe, hats ukichinja we we hainiathiri chochote, unaweza kunipa madhara ya kula nyama isiyochinjwa kwa jina la Mola wako?
Sisi tunaamini katika MOLA , Mungu Mmoja asiyekuwa na Mshirika hajazaa wala Hajazaliwa. Muumba mbingu na Dunia na vilivyopo ndani Yake. Kama na wewe unaamini katika hili ni Ruksa Kuchinja ilimuradi kabla ya Kuchinja uchinje kwa Kumtaja yeye na Kumkusudia yeye MOLA WETU. ! !
 
Kuchinja ni tendo la ibada siyo kula nyama tu ! ! Tendo lililo asisiwa na Baba wa Mitume wote Nabii Abraham/Ibrahim hivyo nitendo tukufu kwa wenye Imani iliyo kamilika siyo tendo la dhihaka na la kuchezea chezea tu.
 
Walii anakua ni nani? Pia samahani mkuu mbona huwa kuna kukinzana kwa wanazuoni juu ya hili. Kuna wengine wanasema hairuhusiwi kumuona asiye muislam na vice versa. Imekaa vp hiyo?
Muislamu karuhusiwa kumuoa
1. Mwanamke wa kiislamu
2. Mwanamke wa kiyahudi
3.mwanamke wa kikristo.
Ama washirikina wengine au makufaar haruhusiwi.
Pamoja na kuwa wakristo na wayahudi ni makafiri na washirikina,tumepewa ruhusa maalum kwakuwa wao walipewa kitabu. Ni makafiri waliopewa kitabu toka kwa Allah wakakiharibu na kuwa chanzo cha kupotea kwao.
Pale wanapo abudu wao huamini wanafanya ibada sahihi kumbe walisha potea.

Ama uwalii una daraja zake. Na huenda kwa utaratibu.
1. Baba mzazi.
2. Mtoto wa kiume wa mwanamke.
3. Baba mdogo au mkubwa.
4. Kaka wa mwanamke kwa baba na mama.
5. Babu mzaa baba
6. Qaadh/kiongozi.

Hao ndio wenye haki ya kumuozesha binti. Na wanakwenda kwa mpangilio. Akiwepo baba mtoto hawezi kumuozesha mama yake.
Akiwepo mtoto Ammi hawezi kuozesha.
Kwa maana walii wa juu akiwepo wa chini yake hana mamlaka.

Huo mpangilio wangu inawezekana sikuipanga vizuri
 
Msitusumbue....huko ma-supermakert mnakonunua kuku mnajua wamechinja vp?? Kuku wangu mtu anipangie jinsi ya kumchinja.....yaan tena mgeni akiwa mwislam akija namuambia kabisa huyu kuku tumechinja wenyewe so ukila ni maamuzi yako....cha kushangaza sioni wakimkataa ndiyo kwanza wanamsosomola vizuri tu
 
Back
Top Bottom