Hili la waziri mkuu kupumzika halikupaswa hata kuwa mjadala; Waandishi tafteni mambo ya msingi ya kujadili acheni kupiga ramli

Hili la waziri mkuu kupumzika halikupaswa hata kuwa mjadala; Waandishi tafteni mambo ya msingi ya kujadili acheni kupiga ramli

Samico Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Feb 6, 2022
Posts
768
Reaction score
1,803
Nawashangaa sana waandishi wa habari siku hizi sijui kwanini mmekuwa kama waganga wa kienyeji!

Mnapiga ramli chonganishi kwenye kauli za viongozi!

Mnatufikishia wananchi habari ambazo wala hazitusaidii sana!

Tunayotaka mtueleze hamsemi; Yasiyo na maana ndiyo mnatufikishia.

Kauli ya waziri mkuu zote zimenyooka kabisa! HAKUSEMA AMEJIUZURU BALI KASEMA ANAPUMZIKA ANAWAACHIA VIJANA.

Alipokuwa akihitimisha hotuba yake bungeni ni kweli alitumia nafasi ile kuwashukuru wananchi wake na kutamani kuendelea kuwatumikia.

Lakini baada ya kutafakari kaona wapo vijana wengine wenye nguvu wanaweza kumpokea kijiti akaona siyo busara kwenda kuminyana nao kama mlezi!

Wakati wa mchakato wa fomu kaona vijana wengi wanania hiyo ya ubunge! Hivyo Kawapa nafasi zaidi! (HILI JAMBO LA KIUNGWANA KABISA)

Hajataka mambo kama ya mwenyekiti Mbowe kwenda kuminyana na vijana wanaotegemea busara zake.

Alichokifanya ni sawa na MBOWE alivyosema HATOGOMBEA lakini BAADAE Wanachama wakamuomba agombee akawasikiliza!

Waziri naye kaona atoe nafasi kwa jamii kushiriki ubunge.

Shida kubwa inayoonekana na wengi wanaohoji ni WAFUASI WA CHADEMA Washazoea kudumu kwenye kiti na aliyekuwa mwenyekiti mbowe!

CCM KUNA Hekima kubwa na kupeana nafasi tofauti na upinzani.

Sasa kwanini KUPUMZIKA KWAKE waziri Igeuke kuwa ni hoja badala ya PONGEZI?

Kila siku vijana mnataka mpewe nafasi.
waziri kaonesha njia halafu vijana walewale Mnahoji tena IMEKUAJE KUAJE!

Nyie si ndiyo mnataka wazee wawape nafasi halafu nyie tena mnahoji imekuaje kuaje!

Hivi kupumzika napo ni nongwa?

Kwenye kauli yake majibu yote yapo pale, hata ile swali la kwanini lipo pale JIBU! kawaachia kijiti na wengine!

Waandishi achenj kuficha habari za msingi na kuleta mijadala ambayo haina tija kwa wananchi hii ni sawa na ramli chonganishi!
 
Ni kweli jambo hili halikupaswa kuwa mjadala mkubwa kwani Majaliwa kahudumu nafasi hiyo ya uwaziri mkuu kwa miaka kumi mfululizo huku akiwa mbunge wa Ruangwa kwa miaka kumi na tano. Inatosha kupumzika siasa na kuachia wengine akiwa bado ana nguvu
 
Kwenye kioo changu namuona Dr Suleiman Jaffo, kijana mzalendo, mwenye weredi, mbunifu na mchapakazi akiteuliwa kuwa PM huku akipitishwa na bunge kwa kura nyingi za kishindo.
 
Bongo hakuna media yoyote inayoweza kujadili siasa kwa akili.
 
Nawashangaa sana waandishi wa habari siku hizi sijui kwanini mmekuwa kama waganga wa kienyeji!

Mnapiga ramli chonganishi kwenye kauli za viongozi!

Mnatufikishia wananchi habari ambazo wala hazitusaidii sana!

Tunayotaka mtueleze hamsemi; Yasiyo na maana ndiyo mnatufikishia.

Kauli ya waziri mkuu zote zimenyooka kabisa! HAKUSEMA AMEJIUZURU BALI KASEMA ANAPUMZIKA ANAWAACHIA VIJANA.

Alipokuwa akihitimisha hotuba yake bungeni ni kweli alitumia nafasi ile kuwashukuru wananchi wake na kutamani kuendelea kuwatumikia.

Lakini baada ya kutafakari kaona wapo vijana wengine wenye nguvu wanaweza kumpokea kijiti akaona siyo busara kwenda kuminyana nao kama mlezi!

Wakati wa mchakato wa fomu kaona vijana wengi wanania hiyo ya ubunge! Hivyo Kawapa nafasi zaidi! (HILI JAMBO LA KIUNGWANA KABISA)

Hajataka mambo kama ya mwenyekiti Mbowe kwenda kuminyana na vijana wanaotegemea busara zake.

Alichokifanya ni sawa na MBOWE alivyosema HATOGOMBEA lakini BAADAE Wanachama wakamuomba agombee akawasikiliza!

Waziri naye kaona atoe nafasi kwa jamii kushiriki ubunge.

Shida kubwa inayoonekana na wengi wanaohoji ni WAFUASI WA CHADEMA Washazoea kudumu kwenye kiti na aliyekuwa mwenyekiti mbowe!

CCM KUNA Hekima kubwa na kupeana nafasi tofauti na upinzani.

Sasa kwanini KUPUMZIKA KWAKE waziri Igeuke kuwa ni hoja badala ya PONGEZI?

Kila siku vijana mnataka mpewe nafasi.
waziri kaonesha njia halafu vijana walewale Mnahoji tena IMEKUAJE KUAJE!

Nyie si ndiyo mnataka wazee wawape nafasi halafu nyie tena mnahoji imekuaje kuaje!

Hivi kupumzika napo ni nongwa?

Kwenye kauli yake majibu yote yapo pale, hata ile swali la kwanini lipo pale JIBU! kawaachia kijiti na wengine!

Waandishi achenj kuficha habari za msingi na kuleta mijadala ambayo haina tija kwa wananchi hii ni sawa na ramli chonganishi!
Mada za media za Bongo
-Umbea
-Siasa uchwara
-Michezo
-Mapenzo na ufuska.

Bahati mbaya ndio jamii yetu inataka kusikia huo upuuzi mda wote.

Hakuna aaetaka kusikia uchumi, biashara,Madini Wala Kilimo
 
Ni kweli jambo hili halikupaswa kuwa mjadala mkubwa kwani Majaliwa kahudumu nafasi hiyo ya uwaziri mkuu kwa miaka kumi mfululizo huku akiwa mbunge wa Ruangwa kwa miaka kumi na tano. Inatosha kupumzika siasa na kuachia wengine akiwa bado ana nguvu
Yes
 
Back
Top Bottom