Hii ndiyo CV ya Idd Azzan

Hii ndiyo CV ya Idd Azzan

Mbonamnakuwa na chuki za kijinga na azani,hajakuchukulia mama ako unaleta pumba hapa mbona cv ya baba ako huiweke.sasa iyo ndo cv yake so what?
 
Suala la Azan kuuza unga si la leo na wala siyo issue ya kuwa na chuki naye, huyu yanki anafahamika sana pale Kino kwa hii biashara na ana mtandao mzuri tu kwani imebainika kuwa anakula na wakubwa. Mh. Sumaye si mjinga kusema kwamba iko siku tutakuja kutawaliwa na wauza unga, si mnaona elimu na wasifu wake ziro, hamna kitu kichwani halafu kesho aje kuwa rais mnafikiri itakuwaje. Hii si chuki baki ukweli lazima usemwe tu.
 
Ukisema tufuatilie CV za wabubge wetu mbona wengi ni matatizo!!! Wengi wana elimu ndogo na wengine wameunga unga sana.

Najaribu kujiuliza hivi CV katika tovuti ya bunge ni kwamba zimekosewa au ndo za ukweli ambazo ndo wabunge wenyewe waliwasilisha wakati wa kuomba ubunge ili ziwauze kwa wananchi?

Ninachojua mimi CV yako ndo inakunadi at the first look hata kama mtu hajakuona katika interview kuwa unafaa au hufai, inakuwaje tunakuwa na wabunge wa aina hii na wananchi tunaendelea kuwachagua wakati sifa tu za kitaaaluma za kuanzia zikiwa ndogo au hawana kabisa?

Nini nafasi ya ofisi ya bunge katika kuhakiki CV na vyeti vya wabunge? Kama haifanyiki nadhani tuna shida katika mfumo wetu wa ajira mana tunawaumbua watoto wetu walimu na polisi kuiba vyeti tunaacha wengine tena wakubwa wakifaidi bila jasho.

Hebu tuangalie pia CV ya Mheshimiwa tena sana Freeman Mbowe, je hiyo ndo CV yake kweli au inechakachuliwa?


Tembelea tovuti ya bunge la Tanzania ujionee mwenyewe vituko.
 
Mbonamnakuwa na chuki za kijinga na azani,hajakuchukulia mama ako unaleta pumba hapa mbona cv ya baba ako huiweke.sasa iyo ndo cv yake so what?

Cv yake haina tofauti na ya Lema na Mnyika. Labda kidogo huyu kawa mkweli tofauti na Lema anayedai kusoma elimu ya msingi akiwa na miaka miwili.
 
Mi ninaowashangaa ni waliomchagua tu.
Afu itafikia hatua hizi cv zitafichwa huko mnapozipata kwenye tovuti ya bunge.
Si mnakumbuka sakata la kuonyeshwa live?
 
Ucc 2001 mpaka 2001 dah!!! Masomo
Ucc ni mwenzi wa saba to Start
 
Kwa mujibu wa kanuni za chaguzi za CCM, sifa ya elimu anayotakiwa kuwa nayo mbunge ni Elimu ya Darasa la Saba. Nadhani mjadala ukielekea huko utakuwa na tija zaidi ili kama kuna haja ya kufanya marekebisho basi hoja zijengwe in that context. Vinginevyo kwa mujibu wa kanuni za chaguzi za CCM, Mheshimiwa Azzan ni mbunge halali kwani Per kanuni za chama cha mapinduzi as of today, mgombea akiwa na kiwango cha elimu cha form four, form six, certificate, diploma, degree, n.k, hiyo inachukuliwa kama ni ziada tu na haipewi uzito na vikao vya kupitisha/kuchuja wagombea. Suala la elimu kwa sasa ni suala la wapiga kura mmoja kwa mmoja kuwa na uelewa tu kwamba je, itumike kama kigezo au lah.

Na mara nyingi ukiwa mgombea mwenye elimu kubwa, ni kawaida sana kujengewa fitina kwamba umechakachua au kampeni zako haziwatendei haki wagombea wasio na elimu, au kwamba peleka elimu yako kwingine ukajenge taifa, sio kwenye nafasi ya ubunge kwani mujibu wa kanuni ya CCM, darasa la saba linatosha, na wananchi hawana haja ya kuzingatia kiwango cha elimu kama ni kigezo cha kukuchagua kama mgombea/mbunge. Nadhani mjadala ungeelekezwa zaidi juu ya kanuni hii badala ya kumjadili Mh Azzan ambae katika mazingira haya, hana hatia na ni mwakilishi halali wa wananchi wa jimbo la Kinondoni.

hiyo ni kweli mkuu lakini wanafanya hivi kwa manufaa ya nani? Mbunge kama huyu Bungeni atafanya nini, atahoji mkata ulioandikwa kwa lugha ya kisheria? au atabaki ndioooooooooooo kila kinachosemwa? hata hiyo akili ya kupambanua chuya na mchele atakuwa nayo? Ifike wakati katiba mama ibainishe kiwango cha mwisho (min) kwa kila daraja la kisiasa na kuwe uwiano pia kati yake na madaraja ya kiutendaji;; pia siyo mbunge la saba, mtendaji wa kata awe na degree! Malipo la 7 juu; degree hali mbovu! hakika tunakoenda kuna kiza kinene kwa kukosa dira@qares.
 
inamaana mshikaj hata o-level alikua hajapiga akaenda college????????????? ina maana pia alikua mbunge na cheti cha darasa la 7???
 
bona cheti cha darasa la saba!
 
Last edited by a moderator:
Ahh, tanzania ni tanzaniatu haiwezi kuwa marekani. Hakuna uafadhali hapo, std 7 na profesa wote wote wezi, na katika akili wote mbumbumbu. Kawambwa, maghembe, Ghasia wote mbona janga la taifa tu? Mujini mipango nye pigeni kélele mpaka midomo iwakauke.
 
Suala la Azan kuuza unga si la leo na wala siyo issue ya kuwa na chuki naye, huyu yanki anafahamika sana pale Kino kwa hii biashara na ana mtandao mzuri tu kwani imebainika kuwa anakula na wakubwa. Mh. Sumaye si mjinga kusema kwamba iko siku tutakuja kutawaliwa na wauza unga, si mnaona elimu na wasifu wake ziro, hamna kitu kichwani halafu kesho aje kuwa rais mnafikiri itakuwaje. Hii si chuki baki ukweli lazima usemwe tu.

kwahyo ni zungu la sembe?
 
nchi hii bhana! eti std 7 idd azzan naye ni mtunga sera kupitia taasisi nyeti ya bunge.daa!.haya ndio ishakuwa na hakuna namna.

hivi prof maji marefu na azzan nani mwenye "ilm" kubwa.?.
 
ukitaka kuwa mbunge ujue kusoma na kuandika tu......hiyo mbona inakubalika na kutambulika.kuna viongozi hawajaenda shule lakini wanapiga kazi kuna wengine wana ma degree na maphd lakini hakuna lolote...cv ni wewe mwenyewe siyo kama namtetea idd azan ila ni kweli jamaa siyo mtendaji ubunge wenyewe alipewa tu na mkullu wa nchi kwa sababu mshikaji
 
Ahh, tanzania ni tanzaniatu haiwezi kuwa marekani. Hakuna uafadhali hapo, std 7 na profesa wote wote wezi, na katika akili wote mbumbumbu. Kawambwa, maghembe, Ghasia wote mbona janga la taifa tu? Mujini mipango nye pigeni kélele mpaka midomo iwakauke.

profesa hata kitabu hawatungi...kweli kabisa tanzania ukifatia utaumia tu kichwa...
 
Back
Top Bottom