Hii kero ya matrafiki Arusha imezidi

Hii kero ya matrafiki Arusha imezidi

Yupo sana anakaa usa, huyu ndiyo anawatia machungu wenzake coz huyu ni mfanyabiashara jumla, hiace zilizoandikwa ndesa ndiyo zake full wax saa kumi hesabu imetimia gari zinaoshwa.
Fuso za mchanga za kutosha, nyumba za kupanga usiseme lkn jamaa bado anakomaa na kupiga mkono magari na haachi hata buku.
"Morning ndessa" siku hizi sizioni sana barabarani.
 
Huyo mwenye matege ipo siku alitukamata akasema yy ana roho mbaya kama sura yake so hata tukimchukia haisaidii sababu anajijua yy ni mbaya
 
Aisee nilijua Dar tu kumbe mpaka A-TOWN. Siku moja nilikuwa kwenye hotel moja mitaa ya mbagala napata breakfast nikawasikia wanasema wameambiwa wapeleke faini makosa saba kila siku yaani sio chini ya 210,000/=Tsh kwa siku. Kwa usumbufu walio nao hawa jamaa ni lazima utembee na fedha mfukoni unapoendesha gari.
Kumbe hii ya kupeleka hesabu ni ya kitambo tu,tangu awamu ya 4 wanapeleka hesabu bado hazija jaa tu?
 
Thread ya June 2015 lkn mpk leo Hali ya ma-traffic haijabadiliki mazee.

Sanasana inazidi kua tete tu.
 
Huyo mwenye matege ipo siku alitukamata akasema yy ana roho mbaya kama sura yake so hata tukimchukia haisaidii sababu anajijua yy ni mbaya
Hahah ila watu wenye roho ngumu wanadumu sana,tangu ameanza kulalamikiwa mpk leo anadunda tu mamaeee.
 
Wako watumiaji wa barabara ambao ni maafisa wa takukuru na usalama wa taifa na wanashuhudia vitendo hivyo


Hawa ndiyo walitakiwa kuisaidia serikali lakini ndiyo kwanza miaka nenda rudi hawana msaada wowote, usishangae nao wanakamuliwa upepo
 
Kwa kweli ni kero tupu. Usumbufu wa makusudi wakati kwa teknologia ya sasa unapashwa na ni zaidi rahisi kujua gari zilizolipiwa zilizoko barabarani, zinazodaiwa leseni zilizokwisha muda wake, gari ambazo hazijakaguliwa nk. Kuna misuse ya resource kwa kwa hali ya juu tu. Kodi kwa maana ya mishahara kwa utendaji kazi wa aina hii ni dhuluma dhidi ya walipa kodi. TUKAJIFUNZE JAPO RWANDA WANAFANYAJE KWENYE HILI.

YAANI NACHALEA KUSEMA KWA SASA RUSHWA IMESHAMIRI KWELI KWELI NATHUBUTU KUSEMA KULIKO WAKATI MWINGINE WOWOTE.
 
trafiki arusha wanakula rushwa sana na ni wasumbufu mnoo ukiwa na kila kitu wanakuomba elfu tano ya supu.

hii inchi kila kona ni kero.
 
Huwajui vizuri Trafiki wa Arusha wewe eeh?,watakugusa tu,labda uwe na mkonge tu ndo hutasumbuliwa,otherwise,watakushambulia wote na wanataka pesa yako kwa ulazima,hata kama ni kubambikiziwa kakitu.
Huo ni uboya traffic police muache uonevu kwa maslahi binafsi
 
Wakuu naandika hii maada nikiwa na hasira isiyozuilika.

Hata kama Ni usalama wa barabarani sasa huu ni upumbavu.Rushwa imekuwa logo yao ya kazi hata kama unakila kitu kwenye gari.Imefikia hatua kama huna hela Arusha kamwe hutaendesha gari hata kama gari lingekuwa jipya hutothubutu.Mbaya zaidi kama unatokea kisongo unaenda Kia imekula kwako kila mita 600wapo.

Anzia uwanjani Kisongo wapo,TANAPA,kona Mbauda,mataa ya Esso,kona ya TCA,Mianzini,Sanawari,kwa Mrefu,Daraja la Nduruma,,shamba la mbegu,Kilala,Makumira university,Usa River ,Maji ya Chai,Kikatiti,Funga kazi Ni King'ori kuna kadada kana miguu kama vibua kapenda rushwa mbaya na kengine kana matege kapo Arusha mjini hako ndo kiboko,nafikiri Arusha inaongoza Kwa kuwa na matrafiki wengi kuliko maaskari wa kawaida.

Kilichobaki ni kuwalipua kwenye vyombo vya habari au kuchukuwa hatua mkononi tu,tumechoka.Siku hizi mimi huwa sisimami kabisa.Haya matrafiki yana njaa kama dumuzi.

Sasa wanajamvi tuwachukulie hatua gani zingine za ziada kukomesha upuuzi huu maana mimi naweza kuja vunja mtu miguu.

Nina hasira sana.
Siku zote najiuliza hivi hii takukuru yetu huwa inang'ata mpaka ipewe amri ?
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom