Hii kero ya matrafiki Arusha imezidi

Hii kero ya matrafiki Arusha imezidi

Siku hiyo nilikuwa Kanisani pale Christ Church, nilisikia bang, kinaendelea na ratiba ya ibada. Nilipotoka nilikuta gari lililowagonga na viatu pembeni, niliwaonea huruma lkn ndo hivyo ishatokea.

Ukweli Traffic police wa Arusha na Manyara (barabara ya Arusha-Babati) ni shida.

Miaka kadha iliyopita nilikuwa natoka Arusha Alfajiri kwenda mkoa. Nilipofika karibu na Magugu trafiki Polisi akanisimamisha. Nilipoondoka tu, kilometa moja mbele, nikamkuta trafiki mwingine akiwa anaendesha baiskeli, aliponiona akasimamisha baiskeli yake na kunisimamisha. Kwa hasira nikamwambia yaani mwenzako amenisimsmisha hapo nyuma kidogo nawe unanisimamisha! Akaona aibu akasema 'nenda'. Inaonekana alikuwa anatoka kukesha kazini na alikuwa anatafuta hela vitafunwa vya kwenda navyo nyumbani kwake.
Hao tena nao ni shida balaaa, kuanzia makuyuni, magugu, minjingu, vituo kibao wamejazana na wanataka hela kwa nguvu
 
Kahamishiwa Boma Ng'ombe ila bado anakaa USA asubuhi anaenda Boma

Hapo Hai hakuna OCD! Inawezekanaje askari aishi mkoa mmoja na kufanya kazi mkoa mwingine?

Ndio maana askari wetu wengi nidhamu zao ni hivyo kabisa.
 
attachment.php


Au tuwakolimbe kuwapunguza mzuka wa rushwa hawa watu?!! Mungu apishe mbali;
Ndugu yanhgu Jembe Afrika una hoja kubwa sana hapa na ya maana sana lakini; hawa ni ndugu zetu tu; shida ni mfumo wenyewe!! kama trafiki anapewa lengo (target figure) akusanye pesa kiasi fulani apeleke ama ofisini au kwa mkubwa fulani kwa sababu zake; trafik atafanyaje jamani?! hata wao ni binadamu; kazi ndizo zinatuweka mijini; wana familia kama sisi na malengo ya maisha mengine kama sisi?! kama huko juu wanakula rushwa kama panya!!; wao wafanyeje jamani au kanuni ya uadilifu inawahusu wao tu "foot soldiers on the beat"?!

Ushauri wa bure;
Option I:: Kuna dhana hii: if you can not fight them; better join them or else you will be the looser!; shauri yako Jembe Afrika; jiunge na mfumo; befriend or be polite to them utaiona Arusha kama free way za California au Autobhan za Ujerumani na kwingineko in the first world ambako mifumo na taasisi ziko so transparent kiasi kwamba kero kama hizi za hovyo hovyo huwezi kuziona huko Ughaibuni.

Option II: Jiunge na VuguVugu la mabadiliko; tuliondoshe hili Zimwi linaitwa CCM; Ukoo wa panya; lililovurugavuruga mifumo ya uwajibikaji likatufikisha hapa tulipo; Vilio kulia na kushoto, vilio juu na chini; Vilio katikati, magharibi, kusini mashariki na kaskazini; kila mahali ni UUUUUUUUUUUwiiiiiiiiiiiiiii!!
Jembe Afrika join the movement for reforms and reconstruction of mother Tanzania; that is UKAWA 2015

Mkuu MTK mimi Ni ukawa damu na ndo maana ninahasira na hawa trafikccm.
 
Last edited by a moderator:
  • Thanks
Reactions: MTK
Kweli ikifikia hivyo wanaudhi, sasa hiyo barabara moja wanajazwa matrafiki wangapi?

Huyo kamanda wa trafiki wa huko itakuwa ni Mchagga!
 
Hivi mbunge godbles lema anajua watu wanavyonyaswa na matrafiki?
 
Last edited by a moderator:
Kweli ikifikia hivyo wanaudhi, sasa hiyo barabara moja wanajazwa matrafiki wangapi?

Huyo kamanda wa trafiki wa huko itakuwa ni Mchagga!

Wanakaa kuanzia wanne, wanakaa kuanzia umbali wa mita 900 Kwa mjini... Na tatizo ni kero zao wanaweza wakakushika na ukawa na kila unachotaka bado wakakuomba hela, na kama ni binti usishangae ukatongozwa.....
Sasa we jifanye unajua saana usiwape hela uende kituoni utajuta, ni lazima ulipe fine na lazima umuhonge anaetoa funguo,ukizidi umuchknow utaandikiwa makosa zaidi Ya 5 na hapo lazima utolewe plate no ukatengeneze gari
Wengine hata uchafu wa gari unashikwa na RTO Mr Mwa........anawabeba saana
 
Kweli ikifikia hivyo wanaudhi, sasa hiyo barabara moja wanajazwa matrafiki wangapi?

Huyo kamanda wa trafiki wa huko itakuwa ni Mchagga!

Dada FaizaFoxy mimi nahisi huyu Rpc Ni mradi wake wa kukusanya pesa kwanini Arusha ina matrafiki wengi kuliko Askari wa kawaida?
Au Arusha ina magari mengi kuliko dar na mwanza?
Cc:mh @gobles lema mbunge
 
Last edited by a moderator:
si juzi kati kuna mtu aliwavunja miguu huko arusha.madereva wekeni mkakati.ikiwezekana malalamiko yenu yafike ngazi husika.wasipowasikia vunjeni mmoja mmoja mguu.kwa mwezi mara 30 mtakuwa mmepunguza angalau trafic wehu kadhaa
 
GODBLESS Lema , Matraffic ni kero au mnasubiri wagongwe mmpeleke vijana wakarushe ndege?? Siku Hizi utaskia umevuka taa upuuzi mtupu
 
Last edited by a moderator:
Yule mkuu wa matrafiki sadiki aliyehamishiwa USA river huyo ndo alikua kiongozi mzuri wa kuigwa.hawa wengine hovyo kabisa
 
Ushauri wa bure;
Option I:: Kuna dhana hii: if you can not fight them; better join them or else you will be the looser

Mimi nimeamua kufanya hivyo.........coz hata nizikiri uchi.........nothing will change..........nchi ishakuwa ya kipuuzi hii........
sitaki presha zisizo za lazima..........
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Kuna trafiki mmoja anaitwa Ndesa, hivi bado yupo Arusha?

Yupo sana anakaa usa, huyu ndiyo anawatia machungu wenzake coz huyu ni mfanyabiashara jumla, hiace zilizoandikwa ndesa ndiyo zake full wax saa kumi hesabu imetimia gari zinaoshwa.
Fuso za mchanga za kutosha, nyumba za kupanga usiseme lkn jamaa bado anakomaa na kupiga mkono magari na haachi hata buku.
 
Mimi nimeamua kufanya hivyo.........coz hata nizikiri uchi.........nothing will change..........nchi ishakuwa ya kipuuzi hii........
sitaki presha zisizo za lazima..........

Polisi si mtu wa kuungana nae hata siku moja. Jifanye rafiki yake then uwe na tatizo ufike ofisini kwao anakukimbia then anampasia jamaa yake aje akusulubu ukimpa rushwa anaenda kugawana na huyo rafiki yako polisi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom