Sote ni mashuhuda kwamba, hivi sasa muungwana anaonekana dhahiri ana tapatapa na kuropoka maneno ya mkosaji mithili ya mtu alieachwa kwenye mahusiano, hana contents kabsaa. Hata waliokua wakimfuatilia na kumsifu mropokaji Polepole, hasa chadema masalia, nao hivi sasa taratibu wameanza kumshtukia na kuthibitisha kwamba msukule Polepole anatunga story na porojo za kutafuta kiki tu na kutafuta umaarufu nonsense. Katika porojo zake hakuna uhalisia na ndio maana zimekosa mashiko na hazina athari zozote kisiasa nchini.
Anachoeleza kinasahaulika na kupuuzwa pale pale.
Ni upotoshaji wa kiwango cha chini sana ana fanya Polepole, Ex-wa CCM.
Ukiwa kama mdau wa jukwaa hili la heshima, unadhani kwanini hekaya za muungwana Polepole zimefikia hatua ya kuonekana ni umbea tu na ni kama maneno ya mtu mkosaji anaejaribu kuficha uovu wake na kuzungumzia watu badala ya issues?
why anapuuzwa hata na wale waliokua wakimuamini sana hususani Chadema masalia, na sasa hawapotezi muda wao tena kumfuatilia msukule polepole?🐒
Mungu Ibariki Tanzania.