Hayati Magufuli ameacha legacy ya kuthubutu kufanya kitu bila ya kuomba ruhusa kwanza kwa mfadhili yeyote

Phillipo Bukililo

JF-Expert Member
Dec 29, 2015
18,488
13,608
Viongozi wa kisiasa wana kazi ngumu sana. Kutakiwa kumridhisha kila wanayemuongoza kwa kadri ya uwezo binafsi, ni mtihani mgumu. Ni vigumu kwa kila anayeongozwa na kiongozi fulani kuwa na mtazamo ule ule kama wa mtu mwingine.

Naamini kabisa kwamba hayati John Magufuli hakuwa na sifa ya kiongozi mwenye diplomasia. Hakuwa na nguvu ya ushawishi wa mwanasiasa, yule wa asili. Alijawa na jazba na ile hali ya kutopenda kubishiwa hata kama mwisho wa mjadala hoja zake pengine zingeimarishwa kuliko alivyodhani. Hayati hakuwa na ile sifa aliyokuwa nayo mwasisi Julius Nyerere ya kuamini katika ushawishi wa hoja zinazotolewa.

Udhaifu wa JPM wa kukosa nguvu ya kidiplomasia ulifidiwa vyema na uwezo mkubwa wa kiutendaji. Uwezo wa kutoa maagizo na kuyafuatilia kwa ukali pasipo kuchekeana, ilikuwa ndio nguvu yake iliyomuwezesha kuanzisha miradi mikubwa na kuweka msukumo wa kuhakikisha inafikia hatua ya kumalizika.

Legacy ya JPM ipo katika uwezo wa kuthubutu kufanya maamuzi magumu. Suala la makinikia linaweza kuonekana ni jepesi lakini watangulizi wa hayati JPM walionekana kukosa uwezo wa kuwaambia wazungu wawekezaji kwamba hapa sisi tunasema hapana na hapa tunataka kifanyike hiki na hiki kwa faida yenu na yetu. Mabilioni ya pesa ambayo tunayapata kwenye mgao wetu baada ya kukaa mezani na kubadilisha mfumo mzima wa umiliki wa biashara ndio legacy yenyewe.

Ni rahisi kusema kwamba vitu vinavyojengwa kwa pesa ya kodi haviwezi kuwa legacy lakini mbona haikuwa rahisi kwa shirika la ndege kufufuliwa mpaka zikaanza kwenda India na kwingineko?. Mbona treni ya mwisho kwenda mpaka Moshi ilifanya hivyo miaka ya 1990 katikati?.

Mbona haikuwa rahisi kuzikarabati meli maziwani na watu wakiendelea kufa kwa kuzama na mitumbwi kila kukicha?. Mbona haikuwa rahisi kutekeleza kwa vitendo maamuzi ya kuhamia Dodoma tangu 1970 mwanzoni?, uthubutu wa JPM katika kutekeleza kile kinachowakera wengi ndio legacy yenyewe.

Hakujaliwa uwezo wa siasa za ushawishi lakini kukosa sifa hiyo hakuwezi kuyafanya yote aliyoyafanya kwa nguvu kubwa yasiwe na sifa ya kuwa legacy yake. Ukiwaambia wote watakaokwenda kufaidika na viwanda vya kupandisha thamani ya dhahabu ndani ya Tanzania kwamba JPM hakuacha legacy wanaweza wakakushangaa.

Ni rahisi sana kusema kuwa kodi zetu zinapofanya kazi yale matokeo yanayopatikana hayawezi kuitwa legacy. JPM ameacha urathi wa uthubutu. ameacha legacy ya ujasiri, ule moyo wenye kujivunia cha kwako mwenyewe hata kama kipo sawa sawa na nguo yenye viraka (vidabwada).

Apumzike kwa amani Hayati John Magufuli. Wenye kutazama masuala kwa kina wanajua ni kitu gani alikifanya kwa uwezo wake wote.
 
Kitu ambacho wengi hawaelewi ni kua mfumo wa Tanzania sio kama ule wa nchi kama Congo, Chad na Burundi au Central Africa ambazo raisi mnaona anapinduliwa bila kupepesa macho.

Tanzania rais kapinduliwa,kuna sababu ambazo zimegusa masilahi ya watu bila kujali uwiano.

Hili wengi hawajajua na hawaelewi lakini hatuwezi kuhoji kuhusu ndege John yalisha isha.
 
Viongozi wa kisiasa wana kazi ngumu sana. Kutakiwa kumridhisha kila wanayemuongoza kwa kadri ya uwezo binafsi, ni mtihani mgumu. Ni vigumu kwa kila anayeongozwa na kiongozi fulani kuwa na mtazamo ule ule kama wa mtu mwingine...
Maelezo yoooote haya ulikuwa na lengo la Kusema Hayati ameacha KUMBUKUMBU ya kufanya maamuzi ya KUKURUPUKA!

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
 
Viongozi wa kisiasa wana kazi ngumu sana. Kutakiwa kumridhisha kila wanayemuongoza kwa kadri ya uwezo binafsi, ni mtihani mgumu. Ni vigumu kwa kila anayeongozwa na kiongozi fulani kuwa na mtazamo ule ule kama wa mtu mwingine....
Kuna mengine yalihitaji ruhusa ya bunge...!! Laki I aliona muhimili wake una kina kirefu
 
Maelezo yoooote haya ulikuwa na lengo la Kusema Hayati ameacha KUMBUKUMBU ya kufanya maamuzi ya KUKURUPUKA!

Sent from my SM-A305F using JamiiForums mobile app
Kukurupuka kwake kumeweza kufufua shirika la ndege lililokuwa limekufa, reli imefufuliwa. Bandari zinakarabatiwa kwa kasi kubwa.

Kukurupuka kwenye faida nyingi sana kwa taifa.
 
Viongozi wa kisiasa wana kazi ngumu sana. Kutakiwa kumridhisha kila wanayemuongoza kwa kadri ya uwezo binafsi, ni mtihani mgumu. Ni vigumu kwa kila anayeongozwa na kiongozi fulani kuwa na mtazamo ule ule kama wa mtu mwingine...
Mi najiuliza..!! Kwa nguvu iliyokatumika kuupinga mradi wa umeme wa mto Rufiji nje ya Hayati nani angekuwa na uwezo wa kuutekereza? Mradi ambao ulijafiliwa mpaka kwenye bunge la ujerumani..!!

Hapana mi binafsi nitamkumbuka na ndiyo Rais wangu bora mpaka sasa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kukurupuka kwake kumeweza kufufua shirika la ndege lililokuwa limekufa, reli imefufuliwa. Bandari zinakarabatiwa kwa kasi kubwa.

Kukurupuka kwenye faida nyingi sana kwa taifa.
Ikiwemo na kushawishi mradi wa mafuta ya Uganda uje Tanzania.

Ujenzi wa bwawa la umeme mto rufiji uliopingwa vikali mpaka kwenye bunge la Ujeruman.

Ujenzi wa kiwanda cha kusafisha Dhahabu.

Kuzuia utoroshwaji wa madini.

Ujenzi wa masoko ya madoni.

Mzee alikuwa tayari ata kuzungushia ukuta mlima kilimanjaro kama wale mataperi wa kule juu wangemzingua.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Viongozi wa kisiasa wana kazi ngumu sana. Kutakiwa kumridhisha kila wanayemuongoza kwa kadri ya uwezo binafsi, ni mtihani mgumu. Ni vigumu kwa kila anayeongozwa na kiongozi fulani kuwa na mtazamo ule ule kama wa mtu mwingine.

Naamini kabisa kwamba hayati John Magufuli hakuwa na sifa ya kiongozi mwenye diplomasia. Hakuwa na nguvu ya ushawishi wa mwanasiasa, yule wa asili. Alijawa na jazba na ile hali ya kutopenda kubishiwa hata kama mwisho wa mjadala hoja zake pengine zingeimarishwa kuliko alivyodhani. Hayati hakuwa na ile sifa aliyokuwa nayo mwasisi Julius Nyerere ya kuamini katika ushawishi wa hoja zinazotolewa.

Udhaifu wa JPM wa kukosa nguvu ya kidiplomasia ulifidiwa vyema na uwezo mkubwa wa kiutendaji. Uwezo wa kutoa maagizo na kuyafuatilia kwa ukali pasipo kuchekeana, ilikuwa ndio nguvu yake iliyomuwezesha kuanzisha miradi mikubwa na kuweka msukumo wa kuhakikisha inafikia hatua ya kumalizika.

Legacy ya JPM ipo katika uwezo wa kuthubutu kufanya maamuzi magumu. Suala la makinikia linaweza kuonekana ni jepesi lakini watangulizi wa hayati JPM walionekana kukosa uwezo wa kuwaambia wazungu wawekezaji kwamba hapa sisi tunasema hapana na hapa tunataka kifanyike hiki na hiki kwa faida yenu na yetu. Mabilioni ya pesa ambayo tunayapata kwenye mgao wetu baada ya kukaa mezani na kubadilisha mfumo mzima wa umiliki wa biashara ndio legacy yenyewe.

Ni rahisi kusema kwamba vitu vinavyojengwa kwa pesa ya kodi haviwezi kuwa legacy lakini mbona haikuwa rahisi kwa shirika la ndege kufufuliwa mpaka zikaanza kwenda India na kwingineko?. Mbona treni ya mwisho kwenda mpaka Moshi ilifanya hivyo miaka ya 1990 katikati?.

Mbona haikuwa rahisi kuzikarabati meli maziwani na watu wakiendelea kufa kwa kuzama na mitumbwi kila kukicha?. Mbona haikuwa rahisi kutekeleza kwa vitendo maamuzi ya kuhamia Dodoma tangu 1970 mwanzoni?, uthubutu wa JPM katika kutekeleza kile kinachowakera wengi ndio legacy yenyewe.

Hakujaliwa uwezo wa siasa za ushawishi lakini kukosa sifa hiyo hakuwezi kuyafanya yote aliyoyafanya kwa nguvu kubwa yasiwe na sifa ya kuwa legacy yake. Ukiwaambia wote watakaokwenda kufaidika na viwanda vya kupandisha thamani ya dhahabu ndani ya Tanzania kwamba JPM hakuacha legacy wanaweza wakakushangaa.

Ni rahisi sana kusema kuwa kodi zetu zinapofanya kazi yale matokeo yanayopatikana hayawezi kuitwa legacy. JPM ameacha urathi wa uthubutu. ameacha legacy ya ujasiri, ule moyo wenye kujivunia cha kwako mwenyewe hata kama kipo sawa sawa na nguo yenye viraka (vidabwada).

Apumzike kwa amani Hayati John Magufuli. Wenye kutazama masuala kwa kina wanajua ni kitu gani alikifanya kwa uwezo wake wote.

Bila kupinga utetezi wako, kama alikuwa na uthubutu wa kutosha kwenye maamuzi, kipi kilimshinda kwenye mikataba ya gas mpaka akaamua kuwekeza 6.5t kwenye umeme wa maji?
 
..aliukuwa na uthubutu wa kuharibu uchaguzi, kupiga na kudhulumu wapinzani, ubaguzi, kutumia mahakama na vyombo vya dola kisiasa, kupendelea alikotoka, na kutumia lugha za matusi, kwa namna ambayo watangulizi wake hakuthubutu, wala kuamini kwamba inawezekana.
 
Back
Top Bottom