Haya maisha sio poa kwakweli

Haya maisha sio poa kwakweli

ndio mkuu.naishi dar kujichanganya najichanganya sema tunafanya kazi kwa ujira mdogo sana hadi mtu unajiuliza nitatoboa kweli kahela hii?

Vumilia ukiwa na malengo endelea kutegemea ndugu kwa muda ukiwa unazichanga kidogo kidogo.
Nunua tool box yako, jeki na vifaa vingine muhimu baada ya hapo tafuta kijiwe popote shinda hapo anza kazi. Huwezi kupata kazi nyingi kwa ghafla ila mbeleni watu watakuzoea utaletewa magari.
Kingine baada ya kua na vifaa vyako tengeneza kikampuni cha kuwafanyia service majumbani ‘movable garage’ ambapo utatengeneza business card zako na kuwagawia watu wa maeneo unapokaa, unaweza kufanya mwenyewe kwenye foleni za magari ukagawa, hao wakipata shida watakutafuta pole pole utakua.
Kufanikiwa kunahitaji jitihada, uvumilivu na mipango.
Ukianza lolote nishirikishe sina mapesa ila naweza kukuchangia hata kutengeneza business card kuitangaza movable garage yako.
 
Una mtoto au family?
Umri wako bado sana unaweza pigana vita vya aina yoyote Ile Ili upate mkate wako.
Kabra huja taka kujiua tembelea hata hospital za karibu yako uone wagonjwa tu
Zen urudi kwako ndo ukajiue.
 
Sasa miaka 24 tu ndiyo ujiue hujui watu wanafanikiwa hata 40+vipi wewe tuliza mshono omba Mungu, huo ujuzi ulio pata veta pambana au kama unaona upepo hausomi angalia namna nyingine hata saidia fundi upate pa kuanzia.
 
ndio mkuu.naishi dar kujichanganya najichanganya sema tunafanya kazi kwa ujira mdogo sana hadi mtu unajiuliza nitatoboa kweli kahela hii?
Usidanganywe na story za mtaan nipo ofisi x , mwanzon nliamin watu wanalipwa mishahara mikubwa sn ila nlipowaambia wang nkagundua nawazid mara 2 krb kila mwajiriwa wa ofisi x , punguza matumiz ya ajab hakuna ela ndogo
 
Wakuu ingekua kujiua sio dhambi ningejiua tuu maana sasa maisha yananinyoosha

Najuta kwanini sijasoma wenzangu wanamaliza mwaka wa mwisho chuo Mimi sina lolote la maana dah

Najiona mjinga sana kwanini nilienda veta kupoteza miaka mitatu Bora ningelima au kuanzisha biashara ningekuwa mbali kidogo

Hata chakula sitamani kwa mawazo dah

Yani sielewi asubuhi niende kuomba kazi wapi aisee

Ngoja tu niache dhambi kama miaka miwili niwe mtu wa ibada kwa sana then najigongesha road niepukane na haya mahangaiko

Haiwezekani miaka 24 bado tuu nategemea ndugu ni aibu mtoto wa kiume
1. Don't kill yourself (whether ni dhambi or not, una sababu za msingi zaidi kuishi so don't waste it)
2. Find watu wanaoweza kuturn ur lyf with real life advice...kwenda Ibada miaka miwili hapatakupa kazi
 
Wakuu ingekua kujiua sio dhambi ningejiua tuu maana sasa maisha yananinyoosha

Najuta kwanini sijasoma wenzangu wanamaliza mwaka wa mwisho chuo Mimi sina lolote la maana dah

Najiona mjinga sana kwanini nilienda veta kupoteza miaka mitatu Bora ningelima au kuanzisha biashara ningekuwa mbali kidogo

Hata chakula sitamani kwa mawazo dah

Yani sielewi asubuhi niende kuomba kazi wapi aisee

Ngoja tu niache dhambi kama miaka miwili niwe mtu wa ibada kwa sana then najigongesha road niepukane na haya mahangaiko

Haiwezekani miaka 24 bado tuu nategemea ndugu ni aibu mtoto wa kiume
Unaweza jigongesha na usife, ukaambulia ulemavu uzidi kusumbua watu
 
Kujiajiri n kuzuri ila sheria za kodi hii nchi ni ngumu mno. Just assume mm nmekodi frame
1.nalipa kodi ya frame kwa mwenye nyumba,,
2.nikinunua umeme nalipa tena kodi ya jengo kupitia luku ( na saiz kodi imepanda kutoka 1000 mpaka 1500 kwa mwezi)
3. Halmashauri bado hawajakufata ukakate lesen
4. Hujalipia bill ya maji na ulinzi
5. Hapo hujala
6.Hapo bado hujakutana na akina TBS,FIRE, WAKALA WA VIPIMO, etc
Wanatunyoosha kweli kweli
 
Wakuu ingekua kujiua sio dhambi ningejiua tuu maana sasa maisha yananinyoosha

Najuta kwanini sijasoma wenzangu wanamaliza mwaka wa mwisho chuo Mimi sina lolote la maana dah

Najiona mjinga sana kwanini nilienda veta kupoteza miaka mitatu Bora ningelima au kuanzisha biashara ningekuwa mbali kidogo

Hata chakula sitamani kwa mawazo dah

Yani sielewi asubuhi niende kuomba kazi wapi aisee

Ngoja tu niache dhambi kama miaka miwili niwe mtu wa ibada kwa sana then najigongesha road niepukane na haya mahangaiko

Haiwezekani miaka 24 bado tuu nategemea ndugu ni aibu mtoto wa kiume
Hujui ulichoandika. Nchi za kiafrika hazina maendeleo kwasababu watu wamewekeza kwenye elimu ya kuajiriwa kuliko ujuzi na kujiajiri.
Dunia ya sasa imebadilika, wasomi wamefungukia vyeti vyao makabatini wanapambana mtaani.
Maisha ya sasa ni hela siyo elimu. Harmonize sidhani hata form 4 kamaliza ila anakula maisha.
 
Wakuu ingekua kujiua sio dhambi ningejiua tuu maana sasa maisha yananinyoosha

Najuta kwanini sijasoma wenzangu wanamaliza mwaka wa mwisho chuo Mimi sina lolote la maana dah

Najiona mjinga sana kwanini nilienda veta kupoteza miaka mitatu Bora ningelima au kuanzisha biashara ningekuwa mbali kidogo

Hata chakula sitamani kwa mawazo dah

Yani sielewi asubuhi niende kuomba kazi wapi aisee

Ngoja tu niache dhambi kama miaka miwili niwe mtu wa ibada kwa sana then najigongesha road niepukane na haya mahangaiko

Haiwezekani miaka 24 bado tuu nategemea ndugu ni aibu mtoto wa kiume
Huko kuwategemea ndugu umeamua wewe. Na usipozinduka na kujitambua watakutumia sana.
Acha kudeka deka, vya ndugu ni vyao na familia zao.
Majukumu yakiwazidi utaona ni kama wanakunyanyapaa ama wana roho mbaya.
 
ndio mkuu.naishi dar kujichanganya najichanganya sema tunafanya kazi kwa ujira mdogo sana hadi mtu unajiuliza nitatoboa kweli kahela hii?
Ukitaka ufeli maisha, wewe komaa na kazi hizi za viwandani sijui unalipwa 6000, saidia fundi 10,000 n.k.
Gharama za maisha zimepanda sana. Ufundi ujenzi ilikuwa inalipa sana ila walipoanza kudhulumu hela, kazi ikawa n laana. Maisha ya ufundi ujenzi yanasikitisha sana bora hata mshona viatu
 
Usikate tamaa ndugu,bado una nafasi ya kufanya mageuzi. 24 ni kijana mdogo sana,hata ungekua na miaka 60 hilo bado haliahalishi kujiua.

Usione watu wanatembea road tu,kila mtu ana matatizo yake. Nitakupa mfano mimi binafsi nimepitia magumu ambayo kwa mtu mwenye roho nyepesi angefikiri kujiua kama wewe. Ila mimi ukataji wangu wa tamaa ulikua ni kinyume na wewe,mimi nilikata UNYONGE,sikukata tamaa.
Sikukubali kukaa chini na kulia lia,nikaamua kujichanganya kila chaka kusaka noti. Hata hapa JF nimekuja mara kadhaa kuomba kazi,ila bado sikupata mwanga. SIKUKATA TAMAA,nikaamua kuzama chaka nako bado sikuambulia kitu,ila katika kujitafuta nilikutana na mwana nikawa nampa mapito yangu kwa kifupi tu. Basi akasema wacha nikuconnect na mwana ili uwe unapata hata hela ya kula,ila matokeo yake kwa sasa mimi ndie namsaidia huyo mwana aliesema nipate japo hela ya kula.

So kwa kifupi kwa sasa napata mabunda Mzee,sio kinyonge. Point yangu ni kwamba,usichoke kujitafuta,usikae chini na kulia, au kujikatia tamaa. Mwanaume anapaswa kupambana mpaka tone la mwisho la jasho na damu yake.
Kama uko home hama,nenda huko mbali,poteaaa! Hata kwa miaka kadhaa,weka nia urudi umefanikiwa au urudi mwili wako.

Hustle hard!! Maisha sio rahisi,maisha ya mpambanaji yanahitaji kujitoa haswa,hayo mawazo ya kukata tamaa ukiyahamishia katika utafutaji utapiga hela sana.
 
ndio mkuu.naishi dar kujichanganya najichanganya sema tunafanya kazi kwa ujira mdogo sana hadi mtu unajiuliza nitatoboa kweli kahela hii?
Unataka ulipwe milioni ngapi kijana? Rizika na hata hicho kidogo ipo siku utafika mbali.

Haba na haba hujaza kibaba.
 
Kuna watu wamesoma hadi skull bas( yaana sasa shule basi tena)
Haina haja ya kujiua, sometime tunajifunza kwa vitendo ili tukomae kiakili. We fanya hivi chukua kila kilicho chako nenda bila kuaga,halafu ujitafute, mbele mbele yao (Journey to unkown). Unawaomba shemeji zako na shangazi kwa kuwa unakaa nao karibu na ukikosa tu chai ya asubuhi ushapiga simu.Ondoka hapo ulipo halafu tupa hiyo sim card, sajili mpya.
Anza kutengeneza cycle mpya ya hustlers.
Move on nigga.
Uko sahihi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom