Haya maisha sio poa kwakweli

Haya maisha sio poa kwakweli

tatizo madogo wa siku hizi mnataka kutoboa ndani ya mda mfupi watu tuli maliza bachelor miaka mi5 mtaani hamna kazi ya maana na hatukuwahi kujiua sembuse ww ulie somea fani za ujuzi
kuliko sie wazee wa colar jobs Pambana mtoto wa kiume na uliende hiyo hazina yako usije ingiwa na tamaa wahuni watakugeuza mwali wao..
 
kweli mkuu.juzi nilienda sehemu kutengeneza gari nikachafuka sana maoli tele fundí nilie msaidia akanipa buki tano tuu haliyakuwa yeyé kachukua milioni na ushee
nilijitukana sana mjini nafanyanini Sasa?
Fundi yoyote junior anapitia hilo hakuna fundi (senior)utakaye fanya nae kazi akupe nusu ya sehemu yake ya malipo. Sasa shukuru sana umepata hiyo knowledge zidisha zaidi nawe uanze kujitegemea, mimi nilisoma hiyo mechanical ila si VETA nimejitolea sana SONGORO MARINE, SAAB SCANIA, TBL acha mzee miaka ya nyuma huko.
Katika ufundi hadi kufika sehemu watu wanakukubali siyo kazi ndogo kabisa fight sana kuna maudhi mno na dharau.

Ila zingatia sana kujua Electrical systems & electronics na matumizi ya computer hapo utawagaragaza mafundi wengi sana homboy huko wengi weupe usiishie kwenye engine na transmission tu au differential kisa ulisoma mechanical dig deep then practical za kutosha haya ma simu sometimes ukiyatumia vizuri yana faida.

God ata bless mwanangu. Pamoja sana usikate tamaa watu wanatumia hadi 15 years kukomaa hadi wanaaminika.
 
Kijana wangu bado mapema sana kukata tamaa 24yrs wewe bado kinda Sana na huo ndio umefika wakat wako wa kustruggle badala ya kukaza wewe ndo unaanza kukata tamaa?why

Jikumbuke umezaliwa wa kiume upambane,usisubiri tu michongo ije..zama posta kapige vibarua vya zege huku unaendelea kuitafutia fani yako pa kuiweka ,usisubiri siku iishe bila kuingiza pesa yoyote.Kuna wenzako Wana matatzo makubwa kuliko wewe..hivi huwaoni walemavu na ombaomba ,tazama wagonjwa na wengine walio na mattzo kuliko wewe.tatiz lako unaangalia walio juu yako Kisha unajikatia tamaa!

Tumepitia mengi kijana hakuna mafanikio kwa kulalamika tu.

Tatiz lako ulikariri ukitoka tu veta utapata kazi ya fani yako kumbe mtaani hapako hivyo! Tafuta kibarua chochote mdogomdogo utatoboa kwa rizki yako bado ipo.

Kaza kijana wangu,asubuhi ikifika amka nenda mjini katafute vibarua hata vya ujenzi.kesho usisubiri chai nyumbani kwa ndugu safar yako ya maisha itaanzia hapo dogo.

Amka,pambana
Usichanganywe na vijaa wenzio wanaovaa pamba Kali na kumiliki mademu wakali.
 
Kijana wangu bado mapema sana kukata tamaa 24yrs wewe bado kinda Sana na huo ndio umefika wakat wako wa kustruggle badala ya kukaza wewe ndo unaanza kukata tamaa?why

Jikumbuke umezaliwa wa kiume upambane,usisubiri tu michongo ije..zama posta kapige vibarua vya zege huku unaendelea kuitafutia fani yako pa kuiweka ,usisubiri siku iishe bila kuingiza pesa yoyote.Kuna wenzako Wana matatzo makubwa kuliko wewe..hivi huwaoni walemavu na ombaomba ,tazama wagonjwa na wengine walio na mattzo kuliko wewe.tatiz lako unaangalia walio juu yako Kisha unajikatia tamaa!

Tumepitia mengi kijana hakuna mafanikio kwa kulalamika tu.

Tatiz lako ulikariri ukitoka tu veta utapata kazi ya fani yako kumbe mtaani hapako hivyo! Tafuta kibarua chochote mdogomdogo utatoboa kwa rizki yako bado ipo.

Kaza kijana wangu,asubuhi ikifika amka nenda mjini katafute vibarua hata vya ujenzi.kesho usisubiri chai nyumbani kwa ndugu safar yako ya maisha itaanzia hapo dogo.

Amka,pambana
Usichanganywe na vijaa wenzio wanaovaa pamba Kali na kumiliki mademu wakali.
Yani ningejua huko unako sema kwakubebea zege mapema tuu ningeenda mana kazi zanguvu naziweza
 
Mimi Mbona nimesoma lakini Sina kitu! Kila mtu kaandikiwa riziki yake tusikate tamaa mkuu.
 
Ndugu yangu maisha hayana formula Yani wewe Muombe Mungu alafu usichoke kupambana na pia usichague kazi ya kufanya piga kazi yoyote hata ukipata buku 2 Kwa siku ..pambana mkuu Mungu ana mipango na maisha Yako ..Hilo la kujiua nakuomba sana Muombe Mungu akusamehe na ukemee hiyo roho ya Mauti ...Mungu Akubariki sana .
 
Yani ningejua huko unako sema kwakubebea zege mapema tuu ningeenda mana kazi zanguvu naziweza
Huwezi kubeba zege wewe, kazi unayoweza ni kushinda mitandaoni kutukana watu basi. Wekeza nguvu katika matusi ya mitandaoni utatoboa dogo.
 
Huwezi kubeba zege wewe, kazi unayoweza ni kushinda mitandaoni kutukana watu basi. Wekeza nguvu katika matusi ya mitandaoni utatoboa dogo.
🤣🤣🤣🤣nielekeze Ile sehemu yakuenda kumenya viazi basi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom