Acha tu ndugu yangu. Yamenikuta. Sijui kama ni stage tu ya maisha nakumbana nayo au kuna mtu anajaribu kunikwamisha. Ila kama ni mtu ananikwamisha siku nitakuja kumgundua ataisoma namba!! Na naomba kama kuna mtaalamu yeyote anaeweza kunisaidia nipo tayari kutoa ushirikiano ila asiwe tapeli
Miaka kama mitatu hivi nilibahatika kupata kazi sehemu flani, kazi ilikuwa na maslahi kweli kweli na ukizingatia mimi nilikuwa bahili kweli kweli. Hela yangu ilikuwa hailiwi kizembe.
Nikawa pia nafanya kilimo, kilimo nacho kikawa kinanilipa kweli kweli. Hela ikanitembelea kweli kweli. Kila nikichungulia kwenye akaunti ikawa inanona vilivyo. Kabla nikiwa naenda likizo akaunti yangu ilikuwa inasoma 57M.
Kufika home kijiji cha kwanza nikamwambia mzee anionyeshe sehemu ya kujenga. Nikaanza chapu maana nilikuwa na likizo ya mwezi m1 tu.
Of course mimi napenda vitu quality. Nikaanza ujenzi wa nyumba ya ndoto zangu ambayo itakuwa ni ya familia yangu pia. Ni nyumba kubwa tu.
Likizo ilivyoisha tu nikarudi zangu mzigoni nyuma nikaacha ujenzi ukiendelea. Nikapaua, nikaweka dirisha na milango ya chuma, nikapiga plasta, wiring na plumbing. Ikawa gumzo pale kijiji. Bwana bwana bwana weee, ghafla mambo yakawa yamebadilika kwa speed ya 5G
Mara vuuup, nikafukuzwa kazi. Lakini akaunti yangu ikawa iko vizuri tu. Nikasema isiwe tabu. Nikasema suburi nifanye biashara pamoja na kuendelea na kilimo kama kawa. Cha kushangaza kila nikitia hela huko inafia huko hairudishi hata mtaji. Nikatia mzigo kwa mara nyingine safari hii nilipigwa hasara mpaka nikikumbuka natetemeka.
Ikawa najikingoja tu hivyo hivyo. Miezi 7 haikuisha 22M sijui zikivyokauka kauka na sasa nipo sina hata mia.
Bado sijakata tamaa, nipo napambana kutafuta chaka lingine maana kama elimu na mavyeti ninayo ya kutosha ila hili nuksi lililonijia sitakaa nilisahau kamwe.
Kimsingi roho hata hainiumi kwa vile kila nikiangalia mjengo wangu natabasamu najisemea kimoyomoyo "Asante Mungu" japokuwa haijaisha ila kwa umri wangu wa 30's nina imani nitapambana nikamilishe nyumba ya ndoto zangu kijijini kwanza ila sijui ni kwa namna gani maana kila nachofanya hakiendi.
Napitia wakati mgumu sana ndugu zangu. Niombeeni. Au nasema uongo ndugu zangu???
KAMA KUNA MTU YUKO NYUMA YA HILI NASEMA AJIANDAE, TENA NASEMA AJIANDAE KWELI KWELI. ONCE NITAKAPOMJUA, hiiiiiiiiiiiiiiii!!!!!!