Hatimaye ZIKA Tanzania ndani ya CCTV

Hatimaye ZIKA Tanzania ndani ya CCTV

Ukweli ni ukweli tu huwezi ficha ukweli kwasababu za uchumi.
Yaani pesa mbele utu nyuma
Yaani kupenda pesa kupita kiasi kwa ajili ya uchumi na kuwasahau watu wako,pesa mbele utu nyuma,hata kama kuna Zika wewe unaangalia uchumi tu,hasa uchumi wa viwanda.
 
  • Thanks
Reactions: bne
Solution ni institutions nyingine za nje na ndani kama ku-replicate study ya NMRI ili kuona kama kile kipimo kipya kinafanya kazi au la ili kuondoa mkanganyiko huu.
 
Mbona vitu vyote vya muhimu serikali inataka viwe hide yaani visijulikane
 
Mi huwa napenda sana kuona mambo kama haya kwa jicho la taswira.

Wazungu wanaovyoona tunabana sana watakuja na story nyingi sana za kutuyumbisha tena kwa kutumia watu wa ndani kama huyu mkurugenzi wa NIMR .

Labda kama mtu hatamuelewa kwa sasa Rais Dr.Magufuli, ila tutaelewa baadaye sana kwa kuona matokeo ya kazi yake.

Ukiangalia mipango ya Tanzania sasa hivi kama ikitekelezeka vizuri bila kikwazo uchumi wetu utapaa sana, mfano. chukulia pana ndege za Tanzania zikaanzisha safari kwenda nchi ambazo hazina safari za mashirika mengine na hapa Tanzania na sehemu zingine ambako hazifiki, tutakamata soko hilo jambo hilo ni kikwazo kwa wazungu katika mipango yao ya akina fastjet.

Pia, viwanda vikakua kwa kasi hapa Tanzania ni wazi kuwa nchi zingine za EAC na SADC zitategemea bidhaa kutoka kwetu, ila sasa wanataka kutuyumbisha ili tupoteze mwelekeo huo wa kiuchumi na kuanza kushughulikia ZIKA.

Pia, mtu yeyote ajue kuwa kuonekana ZIKA nchini kama taarifa ya NIMR ilivyoletwa inaonesha hali ya hatari hivyo utalii na baadhi ya mipango yetu na mataifa ya nje mingi itakwama kutekelezwa hapa nchini kwa hofu hiyo.
Tena, nchi kupitia mamlaka husika wanatakiwa kutangaza hali ya hatari jambo ambalo ni changamoto kwa mipango yetu.

Mfano wa kwanza ni, BRAZIL na ZIKA ; wazungu ni wanafiki sana, kuhusu ZIKA pale Brazil, kwa Brazil jambo halikuwa ZIKA wala Mbu wa ZIKA tatizo lilikuwa Brazil kupata michezo ya olimpiki wote wenye akili walielewa kuwa kuna mataifa makubwa ""wanaojiita nchi za dunia ya Kwanza"" hawakutaka na kupenda kuona Brazil kupata hiyo nafasi ya kuandaa olimpiki, waliitumia zika ili hata kupunguza watakao shiriki ili makadilio ya billioni za mapato zipotee ili Brazil ipate hasara na kufilisika kutokana na maandalizi yale kutumika pesa nyingi na ukumbuke kuwa Brazil iko katika BRICS na wazungu wanona inavyopiga hatua kimaendeleo sasa janga linatengenezwa ; USA, NA Ulaya wako nyuma ya hilo.

Mfano, mwingine ni ugonjwa wa Ebola pale Afrika ya Magharibi, ugonjwa umeua wengi sana na kuwatesa ila tatizo ni dogo sana ni pale walipokuwa na maandalizi ya kuwa na ushirikiano wa sarafu moja (common currency ) na kuzuia matumizi ya dollar, pound na euro katika shughuli zao zote za kiuchumi , sasa ili wawaharibie wakatibua mipango hiyo kwa kuleta ebola ili kila mtu aangalie nchi yake na hilo likafa kabisa hadi leo hakuna anayesema tena kuhusu sarafu. Hapa USA, na Ulaya wamo tena.


Mfano, Rwanda, budget yake wanahitaji wamepiga hatua hii ya kujiwezesha kwa 66% ila 34% tu ni misaada na juzi Rais wao kasema anahitaji kufuta kabisa utegemezi katika budget, sasa hapo utaona povu la wanzugu litakavyowatoka.
Utaona kila kukicha IMF na World Bank [WB] hawaishi kuwashawishi kuchukua mikopo na misaada.
Rwanda moots deadline to end aid dependency

Sasa ukitathimini vizuri ukiangalia mipango yetu kama Tanzania, pia ikitekelezwa hapo pa misaada na utegemezi tutausikia kwa majirani zetu wengine na nchi zingine na hilo ndilo wazungu hawataki kuona likiondoka katika akili zetu na nchi zetu hizi za kiafrika.

Pia unaweza tafuta kitabu hiki usome juu ya mipango ya kujikwamua na papo hapo mwandishi kaonesha mipango inayotumika na wazungu ili kukwamisha nchi za Afrika na Tanzania ikiwemo.

Mwandishi ni A. M. BABU . "AN ECONOMIC STRATEGY FOR THE SECOND LIBERATION OF AFRICA".

Ndani ya kitabu hiki utaelewa ni namna gani Rais Dr. Magufuli yuko makini na kama akiendelea hivi tutafika pazuri sana kama nchi.

Ahsanteni sana.
 
Haya sasa tayari tushaanza kukosa watalii duuuh.....Hili suala ilitakiwa siyo dogo kabisa ilitakiwa nguvu za kitafiti zifanyike kuutambua ukweli kabla ya kuuweka public maana athari zake ni kubwa kwa taifa ila kumbukeni...Lisemwalo lipo kama halipo laja...
Mshakosa watalii, na ndege mshanunua, sijui atapanda nani ndege zenu.

Kuna tatizo la mawasiliano kati ya nimri na wizara ya Afya.
 
Watalii wanaweza wasiulewe Ule msemo/mipasho wa "Hapa Kazi Tu" wanachanganya na "Hapa Zika Tu"
 
Kama ZIKA inashambulia ubongo basi ni kweli ishaingia Tanzania maana kuna watu wanakomenti mpaka unaona kabisa ZIKA washawafanya mazombie yaani hawaekewi kitu kabisa
Zika ni pamoja na kujitoa ufahamu.
 
True beyond all doubts, Dr Kigwangala has decided to be silent because he knows the truth.
Talk because you have something to say, not talk because you have to say something.
 
Wakati serikali ipo kwenye industrial age iliyodumaa, dunia ipo kwenye information age kwa kasi ya jet...!!
Viwanda vya kusindika mbilimbi , pipi, ubuyu, na kufyatua matofali uchwara yenye ratio ya mfuko mmoja kwa matofali 100.
 
Dr Mwele ni Mzalendo wa viwango vyote.

Mungu aendelee kukulinda Dr Mwele...

Matokeo ya utafiti hutolewa na aliefanya utafiti and not otherwise.

Mmeshazoea zile tafiti zenu za kijinga zinazotengenezwa na vile vitengo vyenu TWAWEZA na REDET..!!
Tafiti za twaweze-shwa.
 
Acha kushabikia vyombo vya habari vya nje hujui vina nia gani na nchi yetu.
 
Asee ngoja nianze kufikiria mbele...

Kwahiyo zile ndege za Faru John zitakosa wateja eeeh... [emoji124] [emoji124]
[emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji1] [emoji120] [emoji120] [emoji122]
 
Back
Top Bottom