Hatimaye Mubarak aachia ngazi!

Hatimaye Mubarak aachia ngazi!

unawaza Mugabe wa nini Wakati Mugabe anachapakazi kwa mujibu wa matakwa ya Raia wake Bomu ni huyu wako sio Mugabe
 
unawaza Mugabe wa nini Wakati Mugabe anachapakazi kwa mujibu wa matakwa ya Raia wake Bomu ni huyu wako sio Mugabe
Hapo kwenye bold una maana gani. Mbona unajifanya huyo sio wako vile vile. Acha lugha hizo, hazitufikishi mbali!
 
Kumbukeni kitu kimoja. Wanajeshi hadi leo hawajauwa mtu hata mmoja.

Polisi/usalama wa taifa ndiyo wameuwa watu mitaani wakiwa na/bila bila ya Uniforms.

Jeshi linapendwa sana kwa sasa. Na kama wakijifanya wanaleta kuongeza tarehe ya uchaguzi, watu watarudi mtaani.

USA na mataifa mengine sidhani kama watawaacha wafanye wanavyotaka.

Sidhani kama haya mambo yanatokea USA na EU ukiongeza na Izrael, hawajui nini kinatokea.

Jana alikuwa ajiuzuru ila nafikiri kuna mambo walikuwa hawajayamaliza. Ila kama mnakumbuka, inasemekana mtoto wake alionekana akienda Airport akiwa na msafara mkubwa na baadaye kupanda ndege na kutowekea sijui UK?

Huyu naona atakimbilia German ambako wameshasema watampokea....... Kibaka zee hilooo.

Bado wetu akina Chenge sijui watakimbilia wapi? Mramba na genge lake, hahhahaa....
 
Maandamano yakianza hapa kwetu, ntakwenda na familia yangu hakuna kurudi nyumbani, mpaka kieleweke

Easier said than done...Maji ya kunywa? Kula? Kunya? Kulala? Au unategemea Mohammed Enterprises na Bakhresa watadhamini maandamano?
 
Kumbukeni kitu kimoja. Wanajeshi hadi leo hawajauwa mtu hata mmoja.

Polisi/usalama wa taifa ndiyo wameuwa watu mitaani wakiwa na/bila bila ya Uniforms.

Jeshi linapendwa sana kwa sasa. Na kama wakijifanya wanaleta kuongeza tarehe ya uchaguzi, watatarudi mtaani.
Mkuu i am not buying into this mpaka pale nitakapoona uchaguzi wa haki na uwazi unafanyika kwa sasa wametoa jenerali anayevaa nguo za kiraia na wameweka anayevaa magwanda.
Kuhusu kutokuua well jeshi la misri lina uhusiano mzuri na raia, wananchi hawakuhatarisha usalama wa nchi vile vile labda walikuwa wanataka kuwin trust ya wananchi?
 
Tuone who is the next...............but freedom is coming through river Nile!!!!
 
Natazama Aljazeera asubuhi hii kwa kweli ni furaha isiyo kifani. Kupata uhuru na kujinasua kutoka kwenye minyororo ya ukoloni mamboleo
 
Kilichofanya Rais Mubarak kushindwa ni kutokuwa na watu wa intelligencia kama akina Mwema na Mwamunyange
 
Jamaa zangu sikuingine nishachangia hivi vuguvugu la mabadiliko afrika na namna yanvyofanyika. Kwangu mimi Tunisia sasani unruled state kwa jinsi ilivyoachwa. Kwa upande wa Misri kwa mtazamo wangu Mubark ni heroingawa kuna mtu anamwita pimbi lakini ujue huyu bwa amekua preda for 30 years. Kwanini nasema ni hero? ameweza kujipanga pamoja na Jeshi la Misri ambalo linasifika kuwa ndilo jeshi litiifu na lenye nguvu afrika na kwa baadhi ya nchi za kiarabu. Mubarack ni senior officer wa jeshi makamu wake ni senior officer wa jeshi na pia alikua Mkurugenzi wa intelligence Service (Usalama wa Taifa) na kumbuka toka mwanzo aliagiza mwenyewe kuwa askari na jeshi lisimpige mtu wala kutumia nguvu kubwa kuzuia maandamano maana ni haki yao ila tu atakaye vunja sheria akamatwe na tuliona wakati waliojidai wafuasi wa Mubarak walipokua wakirusha mabom ya petrol walikamatwa, waliokua wanaiba walikua wanakatwa. Kuna mengi ya kumsifia lakini amejipanga na kuhakikisha haiachi nchi katika hali isiyotawalika ameiacha kwa Military Council naye yupo palepale misri kama alivyosema atafia misri naye ni Baba wa Misri. Ikitokea hapa kwetu itakuwa kama tunisia ambapo vyama vya sias vinapigania kutawala nchi. El Baradei siku nilipokutana naye alizuru na kutoa mhadhara UDSM alisema Mubarak ni kichocheo cha umasikini nchini mwake na amejisahau kwa kupumbazwa na Marekani, saudi arabia na izrael maana wanadhani Muslim brotherhood wakichukua nchi wataungana na al Qaeda, Hizbullah na hamas na kuwageuzia waizrael wadhalimu kibao.

Mwisho tusiombee hapa yatokee ya Tunisia bali ya Misri ila yatupasa kuwa makini sana maana mwisho wake ambaye hatumtaki anaweza akawa anaendesha nchi kichinichini yaani akawa na ushawishi mkubwa kama itakavyo kuwa kwa Mubarack.
 
YouTube - Egypt explodes in celebration as Mubarak stepping down

· مبروك لكم ياشباب مصر نصركم العظيم
مبروك لكم يافرسان عودتكم من جديد لساحة الامة العربية
 
Jamaa zangu sikuingine nishachangia hivi vuguvugu la mabadiliko afrika na namna yanvyofanyika. Kwangu mimi Tunisia sasani unruled state kwa jinsi ilivyoachwa. Kwa upande wa Misri kwa mtazamo wangu Mubark ni heroingawa kuna mtu anamwita pimbi lakini ujue huyu bwa amekua preda for 30 years. Kwanini nasema ni hero? ameweza kujipanga pamoja na Jeshi la Misri ambalo linasifika kuwa ndilo jeshi litiifu na lenye nguvu afrika na kwa baadhi ya nchi za kiarabu. Mubarack ni senior officer wa jeshi makamu wake ni senior officer wa jeshi na pia alikua Mkurugenzi wa intelligence Service (Usalama wa Taifa) na kumbuka toka mwanzo aliagiza mwenyewe kuwa askari na jeshi lisimpige mtu wala kutumia nguvu kubwa kuzuia maandamano maana ni haki yao ila tu atakaye vunja sheria akamatwe na tuliona wakati waliojidai wafuasi wa Mubarak walipokua wakirusha mabom ya petrol walikamatwa, waliokua wanaiba walikua wanakatwa. Kuna mengi ya kumsifia lakini amejipanga na kuhakikisha haiachi nchi katika hali isiyotawalika ameiacha kwa Military Council naye yupo palepale misri kama alivyosema atafia misri naye ni Baba wa Misri. Ikitokea hapa kwetu itakuwa kama tunisia ambapo vyama vya sias vinapigania kutawala nchi. El Baradei siku nilipokutana naye alizuru na kutoa mhadhara UDSM alisema Mubarak ni kichocheo cha umasikini nchini mwake na amejisahau kwa kupumbazwa na Marekani, saudi arabia na izrael maana wanadhani Muslim brotherhood wakichukua nchi wataungana na al Qaeda, Hizbullah na hamas na kuwageuzia waizrael wadhalimu kibao.

Mwisho tusiombee hapa yatokee ya Tunisia bali ya Misri ila yatupasa kuwa makini sana maana mwisho wake ambaye hatumtaki anaweza akawa anaendesha nchi kichinichini yaani akawa na ushawishi mkubwa kama itakavyo kuwa kwa Mubarack.

Nakubaliana na wewe na nina amini Mubarak ataendelea kuitawala Misri pasi mtu kujua amefanya jambo la busara sana kutokuwadhuru watu wake na ameondoka nchi ikiwa haijachafuka, Mabruk kwa wale wote waliosimama kidedea ila wajue Mubarak ataendelea kuwa Rais wao na historia haitafutika!
 
Nasikiliza wimbo wa Sarafina apa FREEDOM IS COMMING TOMOROW
 
Kile ambacho dunia nzima tulikua tunakisubiri sasa kimejidhihirisha kua ogopa nguvu ya umma, kwa muda wa siku 18 za wananchi wa Misri kukaa na kukesha usiku na mchana ili Raisi Hosni Mubarak aondoke madarakani kwa kile ambacho wananchi wamechoshwa na utawala wa kibabe na wakidikteta, hii inatufundisha kua viongozi wa Afrika waache ubabe wa kutawala nchi kibabe na kutowasilikiza na kutowatendea wananchi haki kwa ahadi hewa wanazozitoa. Mfano mzuri ni kama huu kwa wananchi wa Misri walishachoshwa na utawala wa kibabe wa Hosni Mubarak na wakaweka woga wao kando kwa kutoogopa nguvu ya dola na wakajitolea kua wacha wafe lakini wacha huyu nduli aondoke na sio kwa manufaa ya wananchi walioko sasa hivi la hata kwa vizazi vitakavyokuja huu ni uzalendo mkubwa wananchi hawa wametuonyesha waafrika wote. sasa hivi na wananchi wa Algeria nao wamezinduka nao wanadai haki yao kwa utawala uliopo madarakani uondoke au utimize matakwa ya wananchi kama Raisi wao alivyoahidi ama sivyo moto utawaka! je sisi watanzania jumejifunza nini? majuzi tumeshaona maandamano ya wanafunzi wa vyuo vikuu wakidai nyongeza ya posho zao nguvu ya dola inatumika! wananchi wanaandamana wakidai haki yao ya kimsingi kudai haki haikutendeka kwenye mchakato wa kudai matokeo ya uchaguzi nguvu ya dola inatumika! Je tunakwenda wapi kama viongozi wa afrika hamtaki kuwasikiliza wananchi na kusikiliza kero zao? Waraka ni wako JK na utawala wako na serikali yako ya CCM zindukeni ama sivyo moto utawaka na muda si mrefu! hali ya maisha ya Watanzani ni mbaya mno kulingana na utawala uliopita! Hizi ni salamu tu kwako JK! Nawasilisha.
 
ni kweli jamaa anamabilioni ya pesa kuzidi hata Bill Gate, anakitita cha pesa kati ya 40-70bln USD:clap2:
Akamatwe arejeshwe Misri na arejeshe mabilioni ya Dola alizowaibia wamisiri na liwe fundisho kwa wengine/
 
Nakubaliana na wewe na nina amini Mubarak ataendelea kuitawala Misri pasi mtu kujua amefanya jambo la busara sana kutokuwadhuru watu wake na ameondoka nchi ikiwa haijachafuka, Mabruk kwa wale wote waliosimama kidedea ila wajue Mubarak ataendelea kuwa Rais wao na historia haitafutika!

mkuu itakuwa hivyo kama atarudisha pesa za wamisri, amekwiba pesa nyingi mno na hilo ndilo litakalo mmaliza.
 
Kwasasa atakuwepo sham ''red sea'' popote pale alipo ni sawa tu na hapa cha kujifunza ni nguvu ya umma na sio umma wote bali ni ''NEW GENERATION POWER OF PEOPLE'' Nguvu hii ni ile niliyoijua katika elimu ya msingi isemayo kwa kizungu tete ''GENERATION IS THE PERIOD OF THIRTY YEARS'' Vijana hawa ni lazima walete mabadiliko kwasababu ndiyo wengi na wana tija ya mabadiliko ya kweli wakisaidiwa na watu wazima wenye kukekerwa na mifumo mibaya....aaahhhhhh kumbe hata hapa tunaweza....pia internet imechangia uhamasishaji ...kwani hapa hatuna net.

TUNASUBIRI MMOJA TU AJITOE MHANGA
 
Back
Top Bottom