Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Hatimaye Mbowe apewa dhamana

Nimetoka kusikiliza redio ya Dochevele ya ujerumani chama cha wanasheria Tanzania kimalani kukamatwa kwa mh mbowe kwa mahakama imekiuka sheria.
 
TLS mbona mnachelewa kutoa maoni? inapendeza kama mnatoa maoni yenu mapema angalau ionekane fulani walisema
 
Katika siasa zinazoongozwa kiukandamizaji ni jambo la kawaida sana kwa viongozi wa upinzani kuwekwa jela kwa kuonewa. Siku moja hadi miaka kadhaa. sasa hivi tumesoma kuwa Geronimo Pratt (RI) alifungwa miaka 28 jela kwa kuonewa, Nelson Mandela alifungwa miaka 26 jela kwa kuonewa; Kenyatta naye alifungwa jela miaka 7 kwa kuonewa, na hata Julius Nyerere naye alinusurika kidogo sana angetupwa jela kwa kuonewa. Kwa hiyo, Mbowe kukaa lumande siku moja kwa kuonewa siyo jambo la ajabu sana chini ya mfumo wetu wa kisiasa wenye kutumia manyanyaso kwa wapinzani.
 
Nimetoka kusikiliza redio ya Dochevele ya ujerumani chama cha wanasheria Tanzania kimalani kukamatwa kwa mh mbowe kwa mahakama imekiuka sheria.
TLS? NGO ya hovyo kabisa ingawa imekuwepo muda mrefu tu. Wanatafuta ni utajiri kwa kila namna. Wamshauri Mh Mbowe nini cha kufanya kwa hatua hii ya mahakama.
 
wanaongoza nchi kwa mazoea ya siasa za chama kimoja, sasa ndiyo matokeo yake haya - kujichanganya changanya kwa mihimili hii mitatu.

sasa hivi chadema ina support kubwa ya wananchi - na hii kamata kamata ndiyo inawamaliza CCM kabisa - "killing themselves softly"
 
Tanganyika Lawless Society(TLS) hawa nao ni mediocre vilevile.It is wastage of space
Baadhi ya wanachama wao wameshirikiana na Chama cha magamba kuihujumu serikali kwa mikataba feki etc.

Umeshasikia hata siku moja(TLS) wamemususpend mmoja wa wanachame wake kwa dubious dealings?
NEVER
 
Strategists wa ccm (kama kweli wapo) ni mufilisi wa kufikiri. Leo tumeamka na headlines mbili kubwa:
Moja ni hii ya Mbowe kukamatwa na nyingine ni Rais Kikwete analalamika viongozi wa dini wanajihusisha na madawa wa kulevya!. Where is ccm in all these? No publicity is bad publicity, CHADEMA nadhani wamelijua hili na ndio maana kila mara ccm wakija na porojo zao basi chadema wanageuza to thier advantage. Sasa Kikwete atarudi dar na kupokelewa na hasira za umma baada ya kumkamata Mbowe, at the same time aanze mkakati wa ku-deal na maaskofu maana kesha-wachefua kwa kuwaita washirki wa biashara ya unga.

Hapo sijaongelea budget, na kwa wale waliosoma wanabidii Dr.Kingwangallah analalamika kamati ya bunge ya afya imeburuzwa kupitisha budget ya wizara ya afya, pia analalamika wabunge wengi wa ccm hawapewi nafasi ya kuongea bungeni!!!. Then tukienda Lumumba tunaambiwa barua za mapacha watatu zimekwama, na mapacha wenyewe wameguka mbogo. Na kwa masikitiko makubwa yule mzee wetu wa 'ramli' hatunaye tena kwa hiyo inabidi kikwete atafute mwenyekiti mwingine wa kamati ya 'ulinzi'.

Niseme hii yote inatokana na nchi kuongozwa kwa 'mazoea' badala ya kufuata sheria sasa chadema wameanza kuwasomea vifungu vya sheria watu wanahamaki. mambo bado- mambo bado-mambo badooo...magoma motomoto ya Nairobi, mambo bado... jamani mnaukumbuka huo wimbo?
 
Chama cha wanasheria Tanzania (Tanganyika Law Socitiety - TLS) kimesema mahakama haikutumia busara kwenye suala la Mh. Freeman Aikael Mbowe. Rais wa Chama hicho Francis Stolla akizungumza na Radio Sauti ya Ujerumani (Deutsche Welle) alisema katika kipindi hiki ambocho bunge la bajeti linakaribia mahakama ingeweza kusubiri mpaka shughuli ya bunge iishe kwani Mbowe ni mtu anayeweza kupatikana.

Aidha amesema hata polisi hawakutumia busara kutomwachia mapema na kumtaka aende mahakamani yeye mwenyewe, kwani ni mtu anayejulikana na si mhalifu sugu.

Mmesema kwa weledi wa kisheria ! na hakuna sehemu mliyosema mahakama imefanya kosa na wala jeshi la polisi limefanya kosa. Well done, mliotoa ni ushauri tu na Mbowe mwambieni hiyo tarehe 24 june afike pale mapemaaaa
 
pole sana Jenifa, upuuzi/ujinga hauna dawa, afadhali ya ngoma kuna dawa za kurefusha maisha lakini si upuuzi/ujinga
 
Haya wacha tuangalie hizi busara za watawala sasa maana Maagesa alikosa busara kabisa na je mbona madai aliyo yataja Slaa jumla yake 4 juu ya kurukwa na kunyimwa haki Mbowe hayaguswi ?
 
Wanafanya kazi kwa kusikiliza maelekezo ya CCM ama kutaka waonekane wanafanya vyema kwa CCM, vyombo vyetu vya dola, polisi na mahakama haviko huru
 
Kama kweli hicho ndicho walichosema TLS basi nadhani kuna mapungufu makubwa ndani ya hicho kikundi. Nilitegemea watoe ni vifungu gani vingeweza kutumika ili kuepesha huu usanii na kuokoa fedha za umma kwa mambo ya kibabe.

TLS wanakuwa na kigugumizi kwenye mambo ya msingi. sikuwasikia wakisema chochote juu ya hoja ya Lissu ya kutoruhusu wanasiasa waingie kwenye mahakama. matoke yake sasa tuna mgongano na 'separation of powers' katika governance system yetu. Walikuwa wapi TLS?
 
Mmesema kwa weledi wa kisheria ! na hakuna sehemu mliyosema mahakama imefanya kosa na wala jeshi la polisi limefanya kosa. Well done, mliotoa ni ushauri tu na Mbowe mwambieni hiyo tarehe 24 june afike pale mapemaaaa

Hiyo tarehe ni siku ya kupitisha budget ya Nishat na madini usitegememee kuwaona mahakamani.
Mnataka mpitishe kimyakimya? Labda Bunge lihairishwe kwa muda hadi warudi.
 
Sasa makeke yote yale ya nini? Yaani wameingia gharama utadhani Mbowe alikuwa anatoroka nchini? Loh! Kweli akili ni nywele kila mtu ana zake! Magamba yanakera jamani! Mh! Basi tu!
 
Ni bora Dk Slaa angeapishwa kuwa rais maana tangu "washinde" uchaguzi mwaka jana JK na administration yake hawajawahi kuiongoza hii nchi wamebakia tu kucheza ngoma za CDM. Mshikemshike mwanza, mauaji arusha, walk out bungeni, katiba mpya, maandamano, kupigwa mawe nyamongo, kukamatwa Lissu, kukamatwa Mbowe. Movie zote hizi good guy - CDM, bad guy - CCM. Ukizingatia ni miezi sita tu....
 
Back
Top Bottom