Hata zikigundulika dhahabu kila mtaa na kila nyumba bado ufukara hautawaondoka Watanzania!

Kiboko ya Jiwe

JF-Expert Member
Apr 7, 2020
12,705
36,154
Habari,

Huu ndio ukweli. Ni wakati sasa Watanzania na viongozi tuache kutwakutwa kujivunia rasilimali za asili badala yake tuwaze maendeleo. Yaani rasilimali zifikiriwe au kutajwa pale tu tunapotaka kufanya jambo.

Tusianze kufikiri na kuzitaja rasilimali kabla ya kufikiri maendeleo (matumizi ya rasilimali). Kutwakutwa kila mtu mara eeh tuna vivutio vingi, mara ukiondoa Brazil sisi tunafuata, Mara oohh tuna rasilimali nyingi kushinda nchi nyingi. So, what?

Hata zikigundulika dhahabu kila kona ya kitanda cha Mtanzania bado ufukara utaendelea kuwaamiza Watanzania. Watanzania wengi wanatafuta asubuhi ili wale mchana, wanatafuta mchana ili wale usiku mmoja tu. Yaani mtu anatafuta akipata anakwenda kumwona mama nitilie.
Anatafuta akipata tu mbio gengeni kuhemea nyanya chungu.

Ndio maana Jiwe alikataa Lock down alijua tu maisha ya Watanzania ni kama ndege, hawana akiba ya miezi 2,3 au 4 mbele. Kama rasilimali hizi zote zilizogundulika na kuanza kutumika hazijamkomboa Mtanzania, basi vivyohivyo hata ardhi yote umbali wa mita moja chini ikijaa Almasi ni bure.

Hapa leo sijagusia malazi, elimu, mavazi na usafiri. Nimegusia msosi tu. Saa sita inakaribia wahangahikaji wanakwenda kugombania msosi wa buku kwa mama nitilie, yaani msosi wa 0.4$, imagine.

Wengine mchana wanatumia jero tu kwa lugha nyingine ni kwamba wanatumia 0.2$ kupata chakula. Wengine wananunua dagaa wa jero, unga nusu 900 nyanya ya mia mbili, maji ya mtoni, kuni. Hapo total 1600 Tshs ambapo ni msosi wa watu 4. Kila mmoja Tsh. 400 ni kama dola 0.1 na ushehe kidogo.
 
Akili fyatu (kwa sauti ya Mzee MwanaKijiji).

Sasa dhahabu ikigundulika kila mahali, si wote tutahamishiwa Kenya? Maana penye madini ni mali ya serikali. Tunaondolewa, analetwa mwekezaji.

Wazaww hawajapewa uwezo wa kuvuna rasilimali zao. Danadana kibao.
 
Akili fyatu (kwa sauti ya Mzee MwanaKijiji).

Sasa dhahabu ikigundulika kila mahali, si wote tutahamishiwa Kenya? Maana penye madini ni mali ya serikali. Tunaondolewa, analetwa mwekezaji.

Wazaww hawajapewa uwezo wa kuvuna rasilimali zao. Danadana kibao.
Hata barabara zote zikijaa rubi bado nyumba za mavi ya ng'ombe zitaendelea
 
Ikigunduliwa dhahabu kila kona dhahabu itashuka thamani yaani itakuwa haina maana tena; hii ilishatokea baada ya Spain kugundua makoloni yenye dhahabu nyingi cha ajabu hawakufanikiwa - Value ilishuka.... Kwahio ni myopic thinking kwetu kuona, kudhani kwamba tunachoambiwa ndio bora ni bora kweli na sio uhalisia wa tunahitaji nini...
 
16884572500841.jpg
 
Hapa leo sijagusia malazi, elimu, mavazi na usafiri. Nimegusia msosi tu. Saa sita inakaribia wahangahikaji wanakwenda kugombania msosi wa buku kwa mama nitilie, yaani msosi wa 0.4$, imagine.

Wengine mchana wanatumia jero tu kwa lugha nyingine ni kwamba wanatumia 0.2$ kupata chakula. Wengine wananunua dagaa wa jero, unga nusu 900 nyanya ya mia mbili, maji ya mtoni, kuni. Hapo total 1600 Tshs ambapo ni msosi wa watu 4. Kila mmoja Tsh. 400 ni kama dola 0.1 na ushehe kidogo.
Ku-equate umasikini na wellness kwa dollar amount ni kupotoka..., Nina mdau bush maisha yake yote hakugusi hata Jero na akipata sana sana consumption ni ulabu / konyagi ambayo nayo ni jero kwahio kwa elfu ishirini anakula bata mwezi mzima..., huyu jamaa amezungukwa na chakula ambacho anakula kila anapotaka..., nyumba yake ya CLAY ni natural Air Condition kwenye joto kuna baridi na kwenye baridi inaleta Joto... Sasa niambie kati ya huyo na mdau aliyepo New York kwenye One Flat Apartment na anavuta hewa ya Exhaust Fumes nani ni tajiri fukara hapo....

We need to rethink our strategies kulingana na mazingira na community / society development yake lazima iangalie Environmental, Economical na Social Factors
 
Ku-equate umasikini na wellness kwa dollar amount ni kupotoka..., Nina mdau bush maisha yake yote hakugusi hata Jero na akipata sana sana consumption ni ulabu / konyagi ambayo nayo ni jero kwahio kwa elfu ishirini anakula bata mwezi mzima..., huyu jamaa amezungukwa na chakula ambacho anakula kila anapotaka..., nyumba yake ya CLAY ni natural Air Condition kwenye joto kuna baridi na kwenye baridi inaleta Joto... Sasa niambie kati ya huyo na mdau aliyepo New York kwenye One Flat Apartment na anavuta hewa ya Exhaust Fumes nani ni tajiri fukara hapo....

We need to rethink our strategies kulingana na mazingira na community / society development yake lazima iangalie Environmental, Economical na Social Factors
Na Hawa wanaotumia 500 kwa msosi wa mchana unawaweka kundi gani?
Wanaolala chumba kimoja vijana 4 na godoro lilulochoka vipi?
 
Na Hawa wanaotumia 500 kwa msosi wa mchana unawaweka kundi gani?
Usiseme wanatumia kiasi gani bali hicho wanachokula ni kitu gani kama kina afya ?!! unaweza ukatumia elfu hamsini ukala junk food zilizokaa kwenye freezer miezi minne; Ulizia watu wa huko Ughaibuni wengine wakija huku wakila chakula wanafurahia taste sababu huko kuna vitu ukila hakuna tofauti na kula makapi...

Alafu unaongelea watu wanakula 500/= msosi wa mchana kwamba ndio kipimo cha masikini Bongo ? (Hivi unajua wangapi mchana wanapiga pasi ndefu) yaani badala ya milo mitatu ni mlo mmoja ? (Hence huenda hata hujui the extent ya tatizo lililopo - Middle Income is Shrinking Wenye nazo wachache na masikini wa kutupwa ndio wengi....
Wanaolala chumba kimoja vijana 4 na godoro lilulochoka vipi?
Tatizo sio vijana au hao wanaolala tatizo ni ecosystem nzima haina balance - Makazi bila Ajira / Ujira wa ku-maintain hayo makazi ni kutengeneza ghettos na ajira bila makazi au sehemu za kutosha kuweka hao watu ni kutengeneza slums - no matter kipato cha hao watu; By the way sijasema Bongo hakuna mafukara; ila inabidi tu-redifine ufukara huenda wewe unawaona wapo vizuri Bongo wote ni mafukara sababu Basic Needs za Chakula, Malazi na Mavazi hawana uhakika nazo - Majority hata milo mitatu hawapati na ni accident waiting to happen siku wakiugua huko Hospitali kutoka lazima ipite donation.....
 
Habari,

Huu ndio ukweli. Ni wakati sasa Watanzania na viongozi tuache kutwakutwa kujivunia rasilimali za asili badala yake tuwaze maendeleo. Yaani rasilimali zifikiriwe au kutajwa pale tu tunapotaka kufanya jambo.

Tusianze kufikiri na kuzitaja rasilimali kabla ya kufikiri maendeleo (matumizi ya rasilimali). Kutwakutwa kila mtu mara eeh tuna vivutio vingi, mara ukiondoa Brazil sisi tunafuata, Mara oohh tuna rasilimali nyingi kushinda nchi nyingi. So, what?

Hata zikigundulika dhahabu kila kona ya kitanda cha Mtanzania bado ufukara utaendelea kuwaamiza Watanzania. Watanzania wengi wanatafuta asubuhi ili wale mchana, wanatafuta mchana ili wale usiku mmoja tu. Yaani mtu anatafuta akipata anakwenda kumwona mama nitilie.
Anatafuta akipata tu mbio gengeni kuhemea nyanya chungu.

Ndio maana Jiwe alikataa Lock down alijua tu maisha ya Watanzania ni kama ndege, hawana akiba ya miezi 2,3 au 4 mbele. Kama rasilimali hizi zote zilizogundulika na kuanza kutumika hazijamkomboa Mtanzania, basi vivyohivyo hata ardhi yote umbali wa mita moja chini ikijaa Almasi ni bure.

Hapa leo sijagusia malazi, elimu, mavazi na usafiri. Nimegusia msosi tu. Saa sita inakaribia wahangahikaji wanakwenda kugombania msosi wa buku kwa mama nitilie, yaani msosi wa 0.4$, imagine.

Wengine mchana wanatumia jero tu kwa lugha nyingine ni kwamba wanatumia 0.2$ kupata chakula. Wengine wananunua dagaa wa jero, unga nusu 900 nyanya ya mia mbili, maji ya mtoni, kuni. Hapo total 1600 Tshs ambapo ni msosi wa watu 4. Kila mmoja Tsh. 400 ni kama dola 0.1 na ushehe kidogo.
UPO SAHIHI TANGANYIKA NI NCHI TAJIRI LAKINI WANANCHI WAKE NDIO MASIKINI ILA VIONGOZI WAKE WANAISHI KITAJIRI
 
Back
Top Bottom