Papa Mopao
JF-Expert Member
- Oct 7, 2009
- 4,107
- 2,506
- Thread starter
- #21
Basi zitapendeza km zikiandikwa kwa mkono
Tena kwa maandishi ya kiufundi kabisa kabisa, cover page itawekwa mchoro wa harusi wa kuchorwa kabisa!
Basi zitapendeza km zikiandikwa kwa mkono
Safi sana!
Hata mumeo mtarajiwa anaweza kukubaliana na hili, nina shaka kama wifi zako wataafiki.
Njoo Mwanza kwenye 'Bukombe' uone, simpo sana, na hakuna kadi, na wanakuja kweli unaona wanakupenda.
Hizi harusi za michango unafki mtupu.
Hilo halina shida, unatoa tu sababu ya kwanini nimechagua hivyo...!
Papaa mukulukulu huyo ni wewe sasa hujui ya wanandugu na wapambe utajuta!
Mawifi wa kizaramo huwajui wewe, bila rusha roho hawamwelewi kaka yao... Na hiyo nyumba ungehama.
Usije ukahangaika kununua vinywaji vya viwandani, andaa togwa, mbege, ulanzi nk
Bila shaka kama zikipatikana na hata ya cake ya ndizi!
kwenye menu ya chakula umesahau mabumunda na mikate ya kumimina! nimeipenda!
wahudumu wavae kama wale mabinti wanaoenda kuchaguliwa kuwa mke wa mfalme mswati!itanoga kichizi
usisahau mwenye mbwa wake aje nae,mwenye nyani haya...kama bush party vile
kuleta utofauti mc akitangaza atumie Megaphone!wireless microphone kila mtu anatumia bana!
All the best papamopao...