Harusi ni mipango yako binafsi, kwanini uninunie?

Harusi ni mipango yako binafsi, kwanini uninunie?

Utamaduni wa mtanzania ni kuishi ktk jamii pamoja...so kama ulichangiwa lazima uchange au ushiriki kwenye maandalizi kikamilifu...pia hata kama hukuchangiwa ww wanao watakuja kuchangisha.....unless uende kuishi kenya...
 
Binafsi nadhani mambo ya kuchangiana harusi yaishie kwa ndugu tu...jamaa na marafiki wachangie wakipenda
 
Big up@ Mtanzanika : tena muowaji ajipange ku cover 60% ya budget otherwise ana kuwa kero hata kwa kamati . ndipo hapo kununiana kunapoanza...kamati inahaha kusaka michango utadhani Loan Recovery team inasaka defaulter!!!! Arafa miezi 6 ndoa imevunjika....
 
Tatizo kwenye kamati wanalaz8misha single iwe 50. Ukitoa 25-30 watakujadili kabisa kama vile umefanya kosa kubwa. Wakikustahi watakupigia uongeze.
Tena wengine watakuhesabia gharama kuwa 30 haitoshi hata mapambo.

Kumbuka usipotoa hawakuelewi......na ukiwaambia hiyo ya kujazia jazia sina kitu siwezi kuja wataona unawadharau

Suala la kuwa mwana kamati hilo ni lingine, muoaji huwa anaangalia ndugu, jamaa na marafiki zake ambao ni wanafanyakazi/wanaojiweza ambao anaamini kabisa hawa watamsaidia ktk shughuli yake, ndio hivyo, ingawa inategemea, mimi ni mwana kamati harusi nyingi na kila siku natoa 50,000 tu, kadi ya double nimemaliza huwa sizidi hapo na harusi ni nzuri sana.
 
Kuna jamaa yangu ni noma ye alivyomaliza harusi yake akatunza daftali lenye orodha ya wote waliomchangia sasa ukienda kuomba mchango anafungua daftari kama haumo imekula kwako
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Uko sahihi mkuu
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Ni kweli kabisa alafu unakuta jitu zima linataka kuoa linatembeza bakuli sasa ulilazimishwa kuoa mimi mtu akinisumbua na michango ya harusi kama ni mwanaume namwambia nikikuchangia na mimi siku nikiwa na kiu nakuja kwa shemeji kukata kiu ndiyoo kwa sababu si nimemchangia na mimi na haki naye.Badala ya kuhangaika na harambee za maendeleo kama vile elimu na afya sisi wa tz wa leo tunahangaika na masherehe ya siyokuwa na tija.
 
Usipochangia harusi,wabongo hawachangii msiba wako.

Mtaenda sawa tu,nae atakwambia ana mipango binafsi.

Potelea mbali hata kwani city na manispaa si wako watazika tu,kwani wao wakushiriki kwenye mazishi ndiyo watasababisha mtu kwenda heaven?
 
Kuna jamaa yangu ni noma ye alivyomaliza harusi yake akatunza daftali lenye orodha ya wote waliomchangia sasa ukienda kuomba mchango anafungua daftari kama haumo imekula kwako

Hahahaha jino kwa jino
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Yaani ndugu yangu wewe ni km mimi,kuna jamaa aliniganda kipindi anafunga harusi sasa kwa bahati mbaya mimi nilikuwa ktk wakati mgumu sana kimaisha,hivyo nilishindwa kumchangia yaani unaambiwa jamaa kaamua kukata mawasiliano na mimi kabisa,Maisha haya!!!!,kazi kwelikweli.
 
Ni kweli kabisa alafu unakuta jitu zima linataka kuoa linatembeza bakuli sasa ulilazimishwa kuoa mimi mtu akinisumbua na michango ya harusi kama ni mwanaume namwambia nikikuchangia na mimi siku nikiwa na kiu nakuja kwa shemeji kukata kiu ndiyoo kwa sababu si nimemchangia na mimi na haki naye.Badala ya kuhangaika na harambee za maendeleo kama vile elimu na afya sisi wa tz wa leo tunahangaika na masherehe ya siyokuwa na tija.

Teh!teh!teh!,huwa wanadai hao km deni vile.
 
Mimi wakati ninafunga harusi sikupenda kuwadai sana watu michango ya harusi mwenyewe nilijipanga,halafu wale jamaa zangu wa karibu tu!,ndo niliwahusisha lkn hata hivyo sikuwabana kwakuwa nilijua Maisha tunatofautiana,aidha wale ambao hawa kunichangia sikuwalipizia kisasi,km nina mchango wakati huo ninautoa tu pasipokujali km alichangia au lah???,lkn sipendi mtu kunilazimisha kutoa mchango wakati ambào mimi sipo vizuri kimaisha,na akininunia kimpango wake.
 
Kwa nini kusiwe na michango ya kujengeana nyumba?
 
Kwa nini kusiwe na michango ya kujengeana nyumba?
Kukiwa na hiki kitu mbona Watanzania tutasonga! Fikiria ile nyomi ya kwenye vikao wangekuwa wanajadili kukomboana kimaisha.Hii haina tofauti na mkulima aliyevuna mazao yake vizuri halafu anaandaa sherehe ngoma chakula chote kinatumika halafu anabaki kutumbua macho!!!
 
Kukiwa na hiki kitu mbona Watanzania tutasonga! Fikiria ile nyomi ya kwenye vikao wangekuwa wanajadili kukomboana kimaisha.Hii haina tofauti na mkulima aliyevuna mazao yake vizuri halafu anaandaa sherehe ngoma chakula chote kinatumika halafu anabaki kutumbua macho!!!

Binadamu sisi hatuna mapenzi ya ukweli.
 
Huu utaratibu unawatesa sana Watanzania,Ni vyema ukaanza kuomba michango kwa watu at least miezi 4-6 kabla ya harusi uchangiwe kidogo kidogo.Utakuta mtu harusi mwezi mmoja au miwili ndio anakwambia umchangie
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Afadhali yako wewe mie shangazi yangu alikuwa anaoza mtoto wa kakaake mwezi ambao nilikuwa napeleka wanangu shule na wala nilikuwa sijajipanga kaninunia hadi leo wala hakuuliza watoto wameendaje shule ila nikishundwa kuwahudumia atakuwa wa kwanza kunilaani!
 
Back
Top Bottom