Harusi ni mipango yako binafsi, kwanini uninunie?

Harusi ni mipango yako binafsi, kwanini uninunie?

Mi kuna watu ninaofanya nao kazi ofisi moja ambao walinichunia makusudi kwenye harusi yangu, hawakutoa mchango wala hata kusema neno lolote lile lakini leo miaka 4 sasa wanashindwa kunipa hata taarifa za mambo yao mbalimbali ya kijamii ikiwemo harusi.
Chamsingi kama huna mueleze ukweli mtu kama mstarabu atakuelewa kwani yeye ndiye aliyepanga siku ya harusi, sio unakaa kimya had shughuri yake inapita hiyo huwa inakera labda kama unauhakika kwamba hautahitaji msaada wa kibinadamu kutoka kwake!
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Ujiandae Na Wewe Kususiwaa Kwenye Sherehe Zakoo...

Waswahili Ndio Tulivo
 
Ujiandae Na Wewe Kususiwaa Kwenye Sherehe Zakoo...

Waswahili Ndio Tulivo
Mie kama kipimo cha ushiriki kwenye shughuli za kijamii ni "mchango wa harusi" bora kususiwa.Tatizo linakuwa kama huchangii harusi na vile vile hushiriki shughuli nyingine misiba n.k. hapo sasa hiyo "NONGWA"
 
Mie kama kipimo cha ushiriki kwenye shughuli za kijamii ni "mchango wa harusi" bora kususiwa.Tatizo linakuwa kama huchangii harusi na vile vile hushiriki shughuli nyingine misiba n.k. hapo sasa hiyo "NONGWA"

Mimi Dada mmoja hata salami amekataa kisa sijalipa 50,000/ alizokuwa ameniandikia kwenye kadi yake.
 
Binafsi ukinipa kadi ukinipangia kiwango cha kutoa sahau..bora uninunie...
 
Watu wanaopanga kuoana kwa mikakati ya kuchangiwa harusi yao basi watachangiwa mpaka unyumba wao.
 
Watu wanaopanga kuoana kwa mikakati ya kuchangiwa harusi yao basi watachangiwa mpaka unyumba wao.

Kwa zile harusi zenu za disco vumbi na sheikh kuweka ubani wala huitaji michango laki tano ni nyingi sana kumaliza yote.
 
Kwa zile harusi zenu za disco vumbi na sheikh kuweka ubani wala huitaji michango laki tano ni nyingi sana kumaliza yote.

Nyingi sana.

Mahari, halwa na ukiweza walima. Kwisha.

Mwanamme anaomba msaada wa kuchangiwa ili aoe? Khaa!

Kwetu hiyo hatukubali kabisa.

Wanangu wameoa na kuolewa bila kuomba msaada kwa yeyote, na mmoja kanipigia simu tu, ananambia "mama nimepata mchumba wiki ijayo tunaoana, naomba wewe na mzee mje kuhudhuria, na tiketi zenu nimeshawatumia na booking ya hoteli nimewafanyia reservation na nimewatumia tayari tazameni email zenu" na schedule ya harusi nimewatumia, msikasirike hiyo schedule wame arrange upande wa mke".

Hicho ndiyo kidume na sikumshangaa, kafata nyayo zetu.
 
Nyingi sana.

Mahari, halwa na ukiweza walima. Kwisha.

Mwanamme anaomba msaada wa kuchangiwa ili aoe? Khaa!

Kwetu hiyo hatukubali kabisa.

Wanangu wameoa na kuolewa bila kuomba msaada kwa yeyote, na mmoja kanipigia simu tu, ananambia "mama nimepata mchumba wiki ijayo tunaoana, naomba wewe na mzee mje kuhudhuria, na tiketi zenu nimeshawatumia na booking ya hoteli nimewafanyia reseration na nimewatumia tayari tazameni email zenu" na schedule ya harusi nimewatumia, msikasirike hiyo schedule wame arrange upande wa mke".

Hicho ndiyo kidume na sikumshangaa, kafata nyayo zetu.

Aka ka bibi kanajifanyaga kanajua sana "reseration ""ndo nn
 
Back
Top Bottom