Harusi ni mipango yako binafsi, kwanini uninunie?

Harusi ni mipango yako binafsi, kwanini uninunie?

Mimi nachanga tena kwa ka furaha ila nachanga kwa mtu mwenye impact kwangu namaanisha uzito wa huyo mtu kwangu...mfano nyie mnaobisha hamchangi je kama ni harusi let say ya mtoto wa mama yako mdogo ambae mmecheza na kukua pamoja kama na ndugu na kama marafiki hutochanga???Au mi mwenzenu sijui maana ya mchango??Coz mimi hata kama sina hela naudhuria kwenye maandalizi,namsaidia kazi za mikono inapobidi uo pia ni mchango..
Marafiki wa karibu mi nawachangia kabisa tena bila kuwa na huzuni......
To me kuchanga ni just kuboresha mahusiano na pia kuonyesha ushirikiano kwa mwenzangu anaepata mke/mume
Vitu ambavyo sichangii ni birthday na graduation
 
One day utaelewa.

Kwa upande mwingine: Si vizuri kumchukia mtu ambaye hakukupa mchango!
 
Single 25- 30?
Itakuwa hujachabgia muda mrefu sana wewe


Single 50!!!!!

Sio lazima uchangie kiasi kikubwa changia kwa uwezo wako, kama ni single hata 30,000 au 25,000 elfu inatosha, pia hakuna mtu anayekupa kadi ya mchango na kukutaka utoe hela siku hiyohiyo au baada ya siku ya 3.

Harusi ni maandalizi ya muda mrefu kuanzia miezi 4 au hadi 6, mtu anaweza anza vikao june na kuoa December so y? elfu sh 25 ndani ya miezi 6, sio vizuri wachangieni wenzenu.Na kama wewe hupendi mambo ya harusi basi ni wewe ikifika zamu yako usifanye, acha wengine tufanye na kufurahia kwa raha zetu.
 
Single 25- 30?
Itakuwa hujachabgia muda mrefu sana wewe


Single 50!!!!!

Sijasema kiasi cha single ni 25 - 30, mtu anaweza toa hadi 200,000 as single, na mwingine anaweza toa 10,000 kama single, pia sidhani kama kuna viwango rasmi vimewekwa kwamba ni lazima uchangie elfu 50, no ni just utaratibu tu na ukiwa nayo unatoa huna basi, kwani lazima ukale kuku ktk sherehe, si unanunua unalia home kwako tu. Kwahiyo kama wewe unatoaga 50,000 as single sio mbaya, ni uwezo wako tu, wengine wanatoa hadi 20,000 single na wengine 50,000 double na kadi wanapewa.
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Heee....heee....heee ! hupendi kuchangia mpaka umejiita sinafungu !
 
Last edited by a moderator:
Usiseme sana ukweli watakuchukia wahusika
 
nina kadi nne za michango mpaka kichwa kinauma... Killa mtu anataka 30000 sasa huon kama ni shida hiyooo.. Watanisamehe sichangii hata 100
 
Ukiangalia vipaumbele vyetu inakupa picha kwa nini hata viongozi wetu kama hawaoni kuwa madawa hamna hospitali, vitabu vya kutosha hakuna mashuleni, maji shida n.k. Kama wananchi wenyewe ndiyo sie wa kukaa tunajadili tupate wapi 30ML tuponde raha kwa siku moja.
 
Michango ya harusi inaumiza kwa kweli, nna kadi sita hapa za kuniomba michango!! Ukiendekeza hizi mambo utaumia!!
 
Kuchangia ni suala la hiari, una nipa taarifa/kadi lkn uamuzi wa kuchangia ama kutochangia upo kwangu na usiniwekee kiwango.
 
michango ya harusi ni upotevu wa rasilimali ni bora hiyo hela uka invest sehemu nyingine
 
Harusi inategemea sana na msimamo wa bwana harusi kwa kukubaliana na bibi harusi. Watu wengine wanafuata namna ambayo nyie mtafurahi zaidi.
Binafsi ndugu wa pande zote mbili walitaka sherehe kuubwa mimi nilikataa na baadae walikuja kunielewa na imekuwa precedent ya harusi simple ninayoimudu mimi na ndoa imedumu. Inahitaji independent mind na msimamo thabiti.
Umesema kweli bwana harusi ukiwa huna msimamo utapelekeshwa.Mie pia niliwaambia sitaki kuhangaishana na watu kama mimi pia nisivyopenda kuhangaishwa hivyo harusi yangu niliwaambia kinapikwa chakula watu wale then kila mtu asepe ndugu walikuwa wabishi Kisa nao wanadai wamechangiwa harusi nyingi nilikomaa mbona walinyoosha mikono funga ndoa newnda kale Bata na mkeo kokote si ndoa tayari.
sio unaanza kusumbuana na watu "ooh! Nimetoa 50,000 wamenipa kijoti kimoja... "
 
Tatizo kwenye kamati wanalaz8misha single iwe 50. Ukitoa 25-30 watakujadili kabisa kama vile umefanya kosa kubwa. Wakikustahi watakupigia uongeze.
Tena wengine watakuhesabia gharama kuwa 30 haitoshi hata mapambo.

Kumbuka usipotoa hawakuelewi......na ukiwaambia hiyo ya kujazia jazia sina kitu siwezi kuja wataona unawadharau


Sijasema kiasi cha single ni 25 - 30, mtu anaweza toa hadi 200,000 as single, na mwingine anaweza toa 10,000 kama single, pia sidhani kama kuna viwango rasmi vimewekwa kwamba ni lazima uchangie elfu 50, no ni just utaratibu tu na ukiwa nayo unatoa huna basi, kwani lazima ukale kuku ktk sherehe, si unanunua unalia home kwako tu. Kwahiyo kama wewe unatoaga 50,000 as single sio mbaya, ni uwezo wako tu, wengine wanatoa hadi 20,000 single na wengine 50,000 double na kadi wanapewa.
 
Tatizo sio tu kutoa mchango, tatizo kuna ndoa nyingine mtu anachangia zinakaa miezi 6 watu wanagawana vyombo, inakeraaaaaa.
 
Hii michango isiyokuwa na tija ndio inachangia umasikini,starehe zako zinataka kuwasumbua wengine.
 
Nashangaa mtu anapanga kuoa, wakati huo hajui wewe umepanga nini? Sasa ukimwambia mimi sina hela kwa sasa kutokana na hali ilivyo, ananuna! Waswahili sisi tuna taabu.

Wanapokutana kwenye hivyo vikao vya harusi agenda ni mimi.

Jamani kila mtu ana majaaliwa yake katika kuzipata fedha, sasa mfuko wangu usiupangie matumizi.

Michango ya harusi ni upuuzi na umasikini wa kujitakia kwa watanzania
 
Hii ni culture ambayo inatutesa sana wabongo na hatuwezi imaliza mana imekua ni kama part ya maisha yetu"

Umenena vyema sana mkuu!
Swala la kuchangia harusi ni la utamaduni zaidi wa sehemu husika...., ambao kwa namna moja au nyingine inakuwa ngumu kuuepuka kwa sababu tunaishi kwenye jamii inayofuata mfumo huo. Hivyo kulingana na utamaduni huo inapofikia wakati mtu anataka kuoa lazima apitishe bakuli la mchango. Na kinachofurahisha zaidi usipochangisha watu (rare cases) ukiwaalika waje kula tu watu wengi huwa hawaudhurii harusi na pengine kuchukulia kama hukuona umuhimu wao kwenye kuchanga why kuuwalika kwenye harusi...??!!

Fikiria katika baadhi ya nchi (mf. Japan) ambazo mwanaume ndio anabeba jukumu zima la maandalizi na kugharamia harusi, kijana huwa anaanza kujiandaa mapema sana. Na huu ndio utamaduni wao, hivyo kama na huku kwetu gharama za harusi zingekuwa ni swala la muoaji pekee tusingesumbuliwa kutoa michango!

Nafikiria kwa wale wanaosema hawachangii harusi yeyote, je hata mdogo, au kaka, dada yako wa damu anapooa/kuolewa je bado hamuwachangii (sizungumzii watu baki au marafiki)...?

Kibongobongo wengi kuoa bila kuchangiwa ni ngumu hata kama atafanya ka-party ka kawaida sana!!
 
Back
Top Bottom