Harrier T...BXL hii sio crash ni karashi!

Harrier T...BXL hii sio crash ni karashi!

Tupo shosti,ukisikia gari kama si dala dala basi lift.
Asante mamii mana bana nimechoka mie kusikia stori hizi..mie gari, mara jana wakati nadrive hakuna asemae jana nilitumbukia kwenye tope wakati natoka shamba..
 
Ok. Tumeshajua kuwa una kigari cha mkopo na unakiendesha kwa mawazo ili kisipigwe pass barabarani. Usingeanza na promo za kukwepa mashimo tungejuaje una kigari cha mkopo? Halafu wewe utakuwa Mhaya misifa kibao!
 
Jamani leo nimekutana na huyu mtu wa Harrier si kuwa nime crash nae ni kuwa ameniletea msala barabarani.

Ilikuwa hivi niko mandela road alfajiri leo kuna mahali nilikuwa nawahi sasa kufika eneo la mwananchi pale kwenye kiungio cha reli kuna mashimo na leo nilikuwa na ka baby walker so nikapinda kulia kukwepa mashimo kisha nikarudi main road ili niendelee maana kuna siku nilipota hapo kwa speed nikayavaa mashimo tairi ikatoka kwenye rim.

Sasa nyuma yangu ndo kulikuwa na hii harrier ilikuwa inakuja ikataka kunipita wakati mie nakwepa shimo ile narudi barabarani akawa kama kaniblock kwa mbele.

Tukatupiana maneno hapo kisha nikamwambia nenda basi muda unaisha maana ningekuwa nakata kona ningewasha indicator.

Aliniboa baada ya kuondoka akakaa site ya kulia mie nikapita ya kushoto akawa anaendesha kawaida, kwa vile nilikuwa na haraka nikakanyaga mafuta baby walker yangu nimpite nae akakanyaga wese baada ya kuona nampita nusura amgonge mtu wa bodaboda yaani aliniboa mnoo na ndo ilikuwa alfajiri.

Yaaani wewe harrier T...BXL popote ulipo ulichonifanyia leo sijakipenda hata.


Sasa Kasinde, mimi nimekusoma zaidi ya mara moja lakini kusema kweli sijakuelewa, naomba nifafanulie kidogo, "crash" ulimaanisha mmegongana gari zenu? na ndivyo nilidhani kwanza kuwa mmegongana (ajali), lakini baada ya kukusoma naona hamja "crash" au ulimaanisha "crush"? (umemzimikia) au ulimaanisha mli "clash" kwa maneno.

Unajuwa hizi lugha za watu kuchanganya na Kiswahili saa nyingine sisi wenye uelewa mdogo inakuwa shida kukuelewa ulimaanisha nini, naomba nisaidie ufafanuzi, was it "crash", crush or clash?
 
Last edited by a moderator:
Huwa nashangaa sana mambo mengine ya humu jf.
 
Dada Faiza kwenye zile mbili za kwanza nilimaanisha kugongana mioyo au kudondokeana kati yangu na hao watu niliokutana nao barabarani kila mtu akiwa kwenye gari lake kwenye foleni. Hii ya tatu hatukugongana mioyo wala magari yaani hakuna ajali ila ilinusurika kuwa ajali na tulitupiana maneno tuu maana aliniblock kwa mbele mie nikashindwa kwenda, baada ya kumwambia unanipotezea muda mie nina haraka nawahi mahali ndo akaondosha gari kwa speed nami nikakanyagia mafuta yangu, ila all the way ni kama alikuwa hataki nimpite akiona nataka kumpita anaongez speed na nusura apate ajali na pikipiki kwa kutokubali mie nimpite, Ni hivo hizo clash, crash crush ni lugha tuu ya kujielezea.

Sasa Kasinde, mimi nimekusoma zaidi ya mara moja lakini kusema kweli sijakuelewa, naomba nifafanulie kidogo, "crash" ulimaanisha mmegongana gari zenu? na ndivyo nilidhani kwanza kuwa mmegongana (ajali), lakini baada ya kukusoma naona hamja "crash" au ulimaanisha "crush"? (umemzimikia) au ulimaanisha mli "clash" kwa maneno.

Unajuwa hizi lugha za watu kuchanganya na Kiswahili saa nyingine sisi wenye uelewa mdogo inakuwa shida kukuelewa ulimaanisha nini, naomba nisaidie ufafanuzi, was it "crash", crush or clash?
 
Ulikuwa unawahi mchepuo!

Mkutano na nilikuwa nina paper ya kupresent saa mbili asubuhi sasa kuna vitu nilikuwa sijakamilisha hivo nikawa nawahi eneo la mkutano mapema ili niweke mambo yangu sawa pamoja na kuizoea venue, si unajua kupresent paper mbele ya wakubwa... tension sasa huyu jamaa akaniharibia pozi, kifupi aliniboa nilitamani nimkate mtama na hiyo harrier yake.
 
Ni wewe tena?

hata sielewi ila safari hii hakukuwa na kudondokeana mioyo ni kutupishiana maneno na kushindana kukanyaga pedeli maana mie nlikuwa na haraka zangu sijui yeye ila aliniboa sana yaani alinikera.
Nikikutana na wengine sitawaleta hapa tatizo sina pa kusimulia ntapata shida...
 
Asante mamii mana bana nimechoka mie kusikia stori hizi..mie gari, mara jana wakati nadrive hakuna asemae jana nilitumbukia kwenye tope wakati natoka shamba..

hahahaahhaa hapo kwenye rangi nyekundu pana muhusu babu Dark City, samahani lakini babu sijamaanisha nilichosema heheheheheheeee
 
Last edited by a moderator:
kuna mtu amewahi kuulizia mguu wa kuku sababu ya mambo kama haya barabarani
 
okay Kasinde again....pole sana kwa crash hii

asantee ila jamaa alinikera sana yaani ngethubutu tuu kushuka kwenye gari yake kunifata maana aliniblock kwa mbele ningefungua kioo nikampiga kwenzi kisha nikafunga vioo na kujilockia milango.
 
We Kasinde we hebu tafuta wa kuzipunguza...

ngoja nimuige babu Asprin alichomuandikia Karucee, nanukuu... ''Hahahah keimamae walah''..........
halafu ntafutie wapi, mi huwa zoezi la kutafuta silifaulu hat iwe kijiko jikoni, utasikia sikioni, sjui kikwapii...
 
Last edited by a moderator:
ngoja nimuige babu Asprin alichomuandikia Karucee, nanukuu... ''Hahahah keimamae walah''..........
halafu ntafutie wapi, mi huwa zoezi la kutafuta silifaulu hat iwe kijiko jikoni, utasikia sikioni, sjui kikwapii...

Ukishindwa kutafuta basi weka hata bandiko hapa kule lavu konekti
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom