Kiukweli kama watanzania ni wazalendo na nchi yao. basi kauli za uongo zinapaswa kupigwa vita. Leo nashangaa kusikia kuwa nchi yetu haikuwahi kuwa na mshikamano, umoja, upendo na amani mpaka hapo ambapo CDM wamekuwa chama cha kwanza kuleta mshikamano hapa Tanzania, ninaweza kuita ni kauli dhaifu kwa kiongozi mkubwa kama yeye (Dr. slaa) unapo utangazia umma kuwa CHADEMA ndo chama cha kwanza kuleta mshikamano Tanzania, naomba tujiulize
1. Tanzania ilipataje uhuru wake bila mshikamano
2. Tanzania iliondoaje ukabila bila mshikamano
3. Tanzania ilishindaje vita vya Idd Amini bila ya mshikamano
... 4. Tanzania imeingiaje kwenye mfumo wa vyama vingi na uhuru wa kuongea(kuropoka, maana wengine wanaropoka tuu kisa yupo huru) bila mshikamano
5. Tanzania imetunzaje amani ya nchi yake bila mshikamano
Je kwa kipindi chote hicho mpaka leo watanzania wanaishije bila ya mshikamano
Je CDM imefanya kipi au imechukua lini madaraka mpaka imeleta huo mshikamano ambao nchi haukuwa nao????????????????
kwa hoja na sio ushabiki naomba kusaidiwa
najua waropokaji watakuja na kuanza kudai oh katumwa. Mimi ni msomi najitambua hivyo sin jinsi ya ya kumfanyia kazi mtu mwingine. but nahitaji kuyajua haya tu.