Hamis Kingwangala amjibu Lowassa

Hamis Kingwangala amjibu Lowassa

Existentialist

JF-Expert Member
Joined
Jan 8, 2013
Posts
554
Reaction score
377
Kazi imeanza na EL najua hutashinda hii vita kwani si ndogo unavyodhani na jina lako litakatwa bora ungekaa kimya!! Huwa nasema kila siku huna washauri wazuri wa campaign!!
ImageUploadedByJamiiForums1432569575.823387.jpg

attachment.php
 
Nilishamaluza kumsikitikia huyu jamaa.....sitafanya hivyo sasa, wala kesho
 
Ha ha ha.. Mwaka huu tutaona kila rangi ndani ya ccm..
 
kutoka Wama ya Mama Salma pale nyuma ya Ikulu hadi ubunge Nzega tena akiwa sio chaguo la kwanza wala la pili unategemea ataacha kuwatumikia nyumba kuu??!!

Kampuni ya MSK ilichotewa mabillioni ya shilling kama stimulus package ya mdororo wa uchumi kuelekea uchaguzi 2010 kutoka BoT,ni bahati tu??!! kwa mdororo upi??!!

Kigwa ni mwenyekiti wa kamati fulani bungeni kwa sasa ja ubunge alipewa baada ya Bashe kufungwa kamba ya usomali na Kikwete,Kigwa ataachaje kuwa kibaraka??!!
 
Ndo maama Hamisi Kigwangala kaomba mdahalo na Lowasa. Ana maswali mengi ya kumuuliza. Mie nina maswali mengi pia. Kwa kuanzia naweka haya maswali ambayo wadau wengi wameyauliza humu jf
Mh Edward Ngoyai Lowassa uko kwenye Safari yako ya matumaini. Nina maswali haya kumi naomba majibu ili iamue kuunga bogi kwenye hiyo safari au nikutose:

1. Je MH. LOWASSA utatumia JIKI ya aina gani kujisafisha na tuhuma ya UFISADI iliyokuganda kama ruba ?


2. Je kwanini BABA WA TAIFA 1995 alisema hufai kabisa kuwa Kiongozi?


3.Je ni kwanini unautaka Urais kwa udi na uvumba, je ukiukosa utajinyonga au utaingia mstuni?


4. Je "FRIENDS OF LOWASSA" ni akina nani? Je unaweza kututajia majina yao? Je huwa wanalipa kodi?Je mabilioni yao hayatokani na MONEY LAUNDERING?


5. Je ukiukosa Urais utaendelea kugawa hayo mamilioni kwa watu na vikundi mbambali au ndo utakula kona?


6. Je wenzako wa CCM waliokwambia wewe ni fisadi na UJIVUE GAMBA ukitwaa Urais utawatia adabu au utakula jiwe na kuwaachia wale nchi ndani ya CCM??


7. Je ni kweli afya yako ni mgogoro na kuwa huwezi kushika kikombe cha chai kwa dakika 3??


8. Je ni kweli huwa unazuka UJERUMANI kutibiwa mara kw mara? Kama ni kweli nchi si itakuwa inaongozwa na Makamu wa Rais muda mwingi?


9. Je washindani wako wa kinyanganyiro cha URAIS utawashikisha adabu au utawaweka kwenye Serikali yako?


10. Je unautaka URAIS ili kujinufaisha wewe binafsi na marafiki zako au una nia njema na madhubuti ya kawaondolea waanchi umasini mkubwa unaoongezeka kila siku?


=======
Feb 2015:
By Kilaza
Wakuu heshima kwenuhaya ni maswali yangu kumi kwa Mheshimiwa Edward Lowassa na Vibaraka wake


1 . Gazeti la Raia Mwema la Novemba 2010 ,liliripoti na kuonyesha picha ya nyumbaambayo familia yako inamiliki Uingereza .Ukasema ni ya mwanao . Je, kwa nchimaskini kama ya kwetu , ni sahihi kwakiongozi mkubwa kumiliki nyumba kubwa naya kifahari nje ya nchi ?


2 . Mkapa alipounda Baraza la Mawazirijipya mwaka 1995 alikuacha . Wengiwanasema kwamba Mwalimu alimwambiaasikupe hata Uwaziri je Kwanini mwalimu Alikukataa???


3 . Tangu mwaka 1994 , yaani miaka 20sasa, Afrika ya Kusini imekuwa inakodishanyumba yako Masaki kama Ubalozi wake .Kuna tetesi kwamba huko nyumba walitakakuhama lakini wakaogopa kuihama nyumbainayomilikiwa na kiongozi mkuu na kunatetesi kwamba sasa wanataka kuhamalakini wanatishiwa kwamba hamuwezikuhama nyumba ya Rais ajaye . Ni kiasigani cha fedha umepata kwa miaka 20 yakukodisha nyumba hiyo ? Je kiasi hichokimeripotiwa kwenye fomu ya maadili?


4 . Kuna maelezo kwamba nyumba hiyo yaMasaki ambayo Mzee Mandela alikujamwaka 1994 kuufungua ubalozi mpya waAfrika ya Kusini ndicho chanzo kikuu chaMwalimu kusema kwamba inakuwaje kijanawa miaka 41 , akiwa mtumishi ya ummamaisha yake yote na mshahara wakeunajulikana , anamiliki hekalu kama lile natena kulikodisha kwa Serikali ya kigeni . Je,unasemaje kuhusu hili ?


5 . Pia unamiliki ranchi kubwa sana kuleMzeri Handeni . Ranchi hiyo ilikuwa ranchiya taifa lakini ukajimegea na sasaumeipanua kwa kumega maeneo zaidi .Ranchi hiyo uliipata ukiwa bado kiongozi waumma. Je, mtu aliyewahi kuwa Waziri waMifugo na Waziri Mkuu kujiuzia ranchiiliyokuwa ya Serikali inaendana na dhanaya uongozi safi na uliotukuka? Tukikupamadaraka makubwa zaidi hautajiuzia kilakitu? Vilevile, katika nchi ambayo wananchiwengi hawamiliki ardhi , kwa kiongozianayetaka kuwa Rais wetu , kuhodhi eneokubwa la ardhi , inatuma picha gani kwawananchi hao ?


6 . Kwenye sakata la Richmond , ujasiri nikusema ukweli au kubwaga manyanga?Kama ungesema ukweli na usingejiuzulukwenye Richmond , Chama kingeathirika vipiwakati unasema hakuna kosa lililofanyika???


7 . Kwanini kwenye kila tukio la kitaifaukisimama tu karibu na Kikweteunahangaika kutuma picha kwenyemagazeti na mitandao yote ???


8 . Katika miaka yako 40 ya utumishi waumma, kuna jipi jipya ambalo umelisahauna sasa utalifanya kwenye Urais???


9 . Umekuwa Waziri wa Ardhi , mbonamatatizo ya ardhi bado tele nchini ?Umekuwa Waziri wa Maji , mbona matatizoya maji bado tele ? Umekuwa Waziri waMazingira, mbona kuna matatizo yauchafuzi wa mazingira ? Umekuwa Waziriwa Mifugo, mbona wafugaji bado maskinina wanahangaika ?? huo urais unautaka wa nini kama uwaziri umekushinda???


10 . Kwenye sikukuu hii , kila MNEC kapatamilioni 1 , hizo ni milioni 370 na kilamjumbe 500 , 000 hizo ni bilioni 2 . Hizi pesazinatoka wapi na zitarudishwa vipi? Je,kuna zoezi la usafishaji wa pesa chafulinalofanywa kupitia kampeni yako???Professor kilaza
 
Anasema kweli mlinda wezi hawezi kupewa ofisi, walijua sakata lote la richmund na mpk akalazimika kujiuzuru. Leo usafi apate wapi kama hakuwa yeye angejiuzuru mapema unafiki. Leo ameitaje wahariri fisi mwamgeuza mbuzi?
 
kigwangwala wewe ni kinda katika medani za siasa za ccm. hujulikani ccm na ni mgeni katika fitina za kiccm. sasa ujue ndio unapotea kabisa katika ccm. mimi niko ccm muda mrefu nazijua fitna za ccm. umekwisha kigangwala nakuonea huruma
Kazi imeanza na EL najua hutashinda hii vita kwani si ndogo unavyodhani na jina lako litakatwa bora ungekaa kimya!! Huwa nasema kila siku huna washauri wazuri wa campaign!!
View attachment 254564
 
Masikini HK!, kumbe hajui hata "what is the name of the game?!.

P.
Hapa dawa ni mtu wetu amwage vyote,ugali,mboga na maji ya kunawa! Hili fukuto lisipokuwa handled vema,basi Ukawa ni mwaka wa mavuno,mapeeemaaa!
Kuna wakubwa fulani wamejiandaa kumchinjia bahari EL,Including JK. Komesha yao ni EL kutema cheche...Watanywea,,otherwise...
 
Back
Top Bottom