Hali ya wanachuo mtaani

Hali ya wanachuo mtaani

Tatizo lenu mnadharau biashara.
Kuna wadau hapo juu wanawashangaa graduates mmoja anauza kande, mwingine vitumbua.

Cha ajabu hapo ni kipi hasa?? Ndivyo biashara inavyoanza kiugumu, siku mtaji ukikua akafanya makubwa mnaanza kusema anadanga. Akili mgando kabisa hizi
Shida wanadharau kazi ngoja jua liwapige ndio watatia akili
 
Nyumba Hadi za ghorofa tunajenga na mafundi darasa la Saba ..
Halafu wenye vyeti civil engineering... Wana hangaika kutafuta kazi

Tunafanya hivyo. Sababu hata tukiwachukua wenye vyeti vya Civil engineering huwa hawajengi.. wanafanya udalali tu wa kupokea kazi ya kujenga kisha wanawauzia mafundi darasa 7 wawajengee.. wao wenye vyeti wanakaa pembeni wanachat na kunywa bia tu ama kubishana simba na yanga
 
Kuna dada mmoja alikuwa pini sana chuoni..kamaliza mwaka jana..nilimfukuzia sana lkn wapi alikuwa anaweka ngumu sana( nadhani alikuwa na mshkaji wake) sasa mwaka huu nipo kwenye mishemishe zangu si nikakutana nae sehemu anauza vitumbua...ameisha...ule uzur wake umepungua haswaaaaa...yani alishtuka kuniona akawa anavunga tu...nikamuungisha nikasepa zangu

Sikutaka kufanya lolote kwan nilijua tu huyu safar hii hachomoi..na zigo lote litaniangukia mm(gharama za kumtunza)
 

Attachments

  • _20230130_200043_1.JPG
    _20230130_200043_1.JPG
    19.1 KB · Views: 16
Sambazeni maombi ya kazi msichoke vijana
Tatizo lenu mnadharau biashara.
Kuna wadau hapo juu wanawashangaa graduates mmoja anauza kande, mwingine vitumbua.

Cha ajabu hapo ni kipi hasa?? Ndivyo biashara inavyoanza kiugumu, siku mtaji ukikua akafanya makubwa mnaanza kusema anadanga. Akili mgando kabisa hizi
Mimi mwenyewe nimeshangaa. Sijui walitaka hao gradutes wawe wadangaji🤔
 
wengine sie hata ajira ziwe wazi wazi, kuna vigezo vinatutoa nje ya mfumo.

Na tusharidhikaaa, polee zao wenye matarajio ya ajira, wanabaki kufurahishwaa km sio kushangazwaa,

Jamaa wa Petroleum anaendesha bajaji, GPA 3.8

Namuangalia nasemaa hiiii,
Kiukwel kuna wengine hata kama ajira zipo lakin hawez kupata

Kuna watu wana maGPA makubwa lakin kwenye interview ni madomo zege
 
Back
Top Bottom