Hakuna Taifa au Kabila lenye Watu Bora kuzidi jingine, mataifa au Makabila yote ni Sawa Ila hayalingani

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,341
51,907
Anaandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Wapo wenzetu wenye mitazamo Duni linapokuja suala la ukabila u utaifa. Wapo wanaojiona ni Bora kuliko wengine lakini ukifuatilia Kwa umaskini ubora wanaojivunia ndio udhaifu wao. Na wapo ambao wanaojiona Duni lakini ukifuatilia uduni wao ndio ubora wao.

Kwa hapa nchini yapo makabila ambayo Watu Kutoka makabila hayo hujiona wao ni Bora kuliko wengine. Ingawaje sio wote lakini kasumba hiyo Ipo. Bila kumung'unya maneno naweza kutaja baadhi ya makabila hayo au maeneo ambayo wanatoka Watu hao, mathalani Wachaga, Wahaya, Wazanzibar, wanyakyusa miongoni mwa wengine. Zingatia sio wote.

Taikon Master nikasema embu ngoja nifuatilie na kuona huo ubora wanaojiona Bora kushinda wengine lakini nikagundua na Kiburi na majivuno ya wapumbavu tuu.

Niligundua Watu wa mataifa wote ni Sawa siku moja nilipokutana na Wayahudi Wakati Fulani nilipokuwa Rwanda. Tangu nikiwa mdogo nilikuwa nasikia Wayahudi ni Watu Bora na wenye Akili lakini siku nilipokutana nao haikunichukua siku Saba kugundua kuwa kuna Wayahudi wajinga, wapumbavu, na wenye Sifa dhaifu kama Watu wa mataifa mengine.

Wachaga nimeishi nao Kwa kitambo kirefu, wengine ni ndugu zangu, wengine na Baba zangu na sasa ni Wakwe zangu. Hivyo tangu utoto ninawajua. Hakuna maajabu yoyote ambayo yatawafanya wajione Bora kuliko wengine.
Wajinga wapo, walevi kupindukia wapo, wakatili wapo, Wasiojua kutafuta Pesa wapo, yaani kila Sifa dhaifu ambazo kwingine zipo nao wanazo.

Wazungu ni wateja wangu, ninachangamana nao Sana kwenye kazi zangu. Sikuona tofauti Ile kubwa ya kuonekana Bora kuliko wengine. Wapo Wazungu wenye Roho Mbaya, wapo Wazungu wanyanyasaji na wabaguzi, wapo Wazungu wenye tabia chafu ambazo zingine kuzisema sio Maadili. Hawana ule ubora ambao Watu wasiowajua huwaona.

Ninachotaka kusema, hakuna mtu Bora kuliko mwingine. Na hakuna taifa Bora kuliko taifa jingine. Na wala hakuna kabila Bora kuliko kabila jingine.

Ubora wa Watu hupimwa Kwa uadilifu, maadili, Haki, Wema, Upendo, Ukweli miongoni mwa mambo mengine.

Wakati tukiwa wadogo wale wote(wengi wao) waliokuwa wanajiona Bora kuliko wengine, wale wote wenye Kiburi na majivuno Kwa sababu yoyote Ile Kwa sasa ni Watu ambao wanatia huruma, Watu wakuhurumiwa tuu.

Usihangaike kuwa Bora dhidi ya wengine. Bali tafuta kuwa Bora juu yako mwenyewe na sio juu ya wengine. Jitahidi uwaone wengine Bora kuliko wewe hiyo itakupa nafasi ya kuona umuhimu wa wengine na umuhimu wako kuonwa na wengine.
Usipoona ubora wa wengine jua hata wewe ubora wako hauonekani.

Pumzika sasa Taikon wa Fasihi

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Sawa ila kuna makabila yasio kua na maendeleo bila sabab za msingi, wame kumbatia umasikini wa naona ni sifa, ukioa katika hilo kabila sahau utajiri.
 
Sawa ila kuna makabila yasio kua na maendeleo bila sabab za msingi, wame kumbatia umasikini wa naona ni sifa, ukioa katika hilo kabila sahau utajiri.
Maendeleo ya vitu hayamfanyi MTU kuwa Bora. Hayo makabila au mataifa yenye Maendeleo yangetumia Maendeleo hayo kusaidia mataifa au makabila ambayo hayajaendelea angalau kidogo tungeona faida ya hayo Maendeleo.
 
Nayasoma maandishi haya nikiwa kwakoko hill nikiomba msamaha mizimu ya kipare baada ya kumchezea binti yao
 
Watu wengine ndio wanaona makabila hayo kuwa bora zaidi. Hata kati ya watu wapo wanaojiona bora kuliko wengine. Nafikiri kati ya watu wanaojiona bora sana ni mtu mmoja anaitwa Robert Heriel. Pia amefanikiwa kuwafanya watu wamwone bora sana kumbe ni mtu wa kawaida sana.
 
Watu wengine ndio wanaona makabila hayo kuwa bora zaidi. Hata kati ya watu wapo wanaojiona bora kuliko wengine. Nafikiri kati ya watu wanaojiona bora sana ni mtu mmoja anaitwa Robert Heriel. Pia amefanikiwa kuwafanya watu wamwone bora sana kumbe ni mtu wa kawaida sana.

Ubora wa mtu utaonekana pale anapowaona wengine ni Bora zaidi yake.
Kila mtu ni muhimu na Bora Kwa nafasi yake. Kuingilia nafasi za Wengine ndio Kiburi Chenyewe
 
Haiitajiki rocket science kujua kabisa kuwa Wazungu na South Asians wakifuatiwa na Waarabu ni bora watu weusi tupo huko mwisho kabisa tunaburuza mkia.
 
Mwanangu ni ngumu kuutetea Uafrika kwa namna yoyote ile dhidi ya ubora wa races zengine tupo hovyo kwenye angles nyingi sana zinazo onekana kirahisi tu ni ngumu kuficha ubovu wetu dhidi ya hao wengine
 
Heriel, napenda sana uchambuzi wako. Lakini kwenye ili suala la ubora wa kabila fulani umekumbwa na mapokeo ya jamii.

Sifa za makabila uliyoyataja nyingi wamepewa na jamii. Chanzo kikiwa ni mapokeo. Nao wakaikumbatia.

Sifa hii uwagharimu watu wa makabila haya wakashindwa kunufaika na fursa mbalimbalibkwa sababu tu ni kabila fulani. Wengine wakaenda mbalimbali na kukataa kujitambulisha kwa kabila lao.

Sababu nyingine ni dhana ya uzalendo waliopandikizwa kwenye kabila lao. Zamani kabila lilikuwa kama taifa ambalo wenye kabila lao walipaswa kujitambua na kutetea mila zao, maeneo/ardhi yao n.k. Hivyo nyimbo na taratibu nyingine zililenga huko. Haya mambo hayaishi siku moja utembea kizazi hadi kizazi.

Sasa kusema kuwa .makabila fulani ujiona bora na kuendelea kuyataja Heriel nawe umekumbwa na mapokeo ambayo nimeyasema mwanzo.
 
Back
Top Bottom