Kila kabila lilitakiwa kuwa na nchi yake

Lycaon pictus

JF-Expert Member
Jan 31, 2021
7,221
12,726
Ukisoma historia ya dunia toka mwanzo utaona kuwa kila kabila la watu lilikuwa na nchi yake. Habari ya makabila mengi kuwa nchi moja ilitokea pale kabila moja kuteka jingine na kulifanya kuwa chini yao. Na hilo lilileta unyonyaji na ubaguzi. Hata wazungu ambao tunaona wamestaarabika wana ubaguzi wa kikabila hadi leo. Waflemish na Wafaransa huko Ubelgiji haviivi. Wabritish na wascottish na wairish nao haviivi. Wacanada wanaoongea Kiingereza na wale wanaaongea Kifaransa hawako bado sawa.

Wazungu walipounda mataifa ya Afrika lengo halikuwa kuunganisha makabila mbalimbali. Lengo lilikuwa kujimegea maeneo makubwamakubwa ya kutawala. Hata wakati wa ukoloni, makabila haya hayakujiona kuwa ni nchi moja. Ndiyo maana walijitambulisha kama Nchi ya Ugogo, Nchi ya Unyamwezi, Uchagga nk nk. tulipopata uhuru ndipo walilazimika kujitambua kama nchi yenye makabila mengi.

Tokea nchi za kiafrika zianze kupata uhuru, miaka 60+ iliyopita, zoezi la kuunda nchi za makabila mengi limekuwa gumu kupita kiasi. Naweza sema ni Tanzania pekee walau imepiga hatua kidogo katika hilo. Nchi zingine imeshindikana kabisa. Rwanda walichinjana kikatili sababu hiyo. Ethiopia bado wapo vitani, Darfur watu walichinjwa kama wanyama. Nigeria haieleweki hata kidogo. Angalia karibu kila taifa la Afrika utaona kuwa zoezi la kuunda nchi ya watu wa makabila tofauti limeshindikana kabisa.

Ukiangalia hali halisi utaona kuwa Nchi ya makabila mengi haiwezi kuwa sawa, na kuwa kila kabila lilipaswa kuwa nchi, kama ilivyokuwa kwa maelfu ya miaka.
 
Ukisoma historia ya dunia toka mwanzo utaona kuwa kila kabila la watu lilikuwa na nchi yake. Habari ya makabila mengi kuwa nchi moja ilitokea pale kabila moja kuteka jingine na kulifanya kuwa chini yao. Na hilo lilileta unyonyaji na ubaguzi. Hata kabila mengi haiwezi kuwa sawa, na kuwa kila kabila lilipaswa kuwa nchi, kama ilivyokuwa kwa maelfu ya miaka.
Ndio maana ya kingdom, Nyerere alipofuta machifu aliogopa hilo kila Chief ndio mtawala halisi wa Kabila lake na ndiye anayeheshimika na jamii yake.
 
Ubaguzi sio lazima uwe WA kikabila ,upo WA kidini,rangi n.k
Hizi tamaduni za kikabila zitafikia ukomo kadri watu watakavyozidi kutangamana.
Tatizo la WA Africa ni kutojitambua kama race inayotakiwa kujismamia kama walivyo chines na European au indians.
 
Bila shaka huyu atakua msukuma, ameona jins walivyo wengi kwao ila tambua kama nimchaga ujue yale nimakabila mengi yameungana ila ukingia ndani mmeru nammarangu niwatu tofauti, na mkibosho na mmachame nao tofauti yan mpaka lugha... Ukienda huko mara mkoa mmoja unamakabila zaid ya 30
 
Ubaguzi sio lazima uwe WA kikabila ,upo WA kidini,rangi n.k
Hizi tamaduni za kikabila zitafikia ukomo kadri watu watakavyozidi kutangamana.
Tatizo la WA Africa ni kutojitambua kama race inayotakiwa kujismamia kama walivyo chines na European au

Wahindi hawajamaliza kabisa tatizo la ukabila. Ni kubwa kuliko nchi nyingi za Afrika. Hao watu wa Ulaya, Uingereza bado inakabili hii shida. Yugoslavia ilivunjika na watu kuuana sababu ya ukabila. Si rahisi kuuondoa. Zaidi ni huwa unakomaa.
 
Bukoba ingekuwa Nchi ingekuwa noma sana wako na misosi na ya kutosha na Ziwa na Mandhari nilifika kule nilipapenda sema kilugha ndo mtihani.
 
Ukisoma historia ya dunia toka mwanzo utaona kuwa kila kabila la watu lilikuwa na nchi yake. Habari ya makabila mengi kuwa nchi moja ilitokea pale kabila moja kuteka jingine na kulifanya kuwa chini yao. Na hilo lilileta unyonyaji na ubaguzi. Hata wazungu ambao tunaona wamestaarabika wana ubaguzi wa kikabila hadi leo. Waflemish na Wafaransa huko Ubelgiji haviivi. Wabritish na wascottish na wairish nao haviivi. Wacanada wanaoongea Kiingereza na wale wanaaongea Kifaransa hawako bado sawa.

Wazungu walipounda mataifa ya Afrika lengo halikuwa kuunganisha makabila mbalimbali. Lengo lilikuwa kujimegea maeneo makubwamakubwa ya kutawala. Hata wakati wa ukoloni, makabila haya hayakujiona kuwa ni nchi moja. Ndiyo maana walijitambulisha kama Nchi ya Ugogo, Nchi ya Unyamwezi, Uchagga nk nk. tulipopata uhuru ndipo walilazimika kujitambua kama nchi yenye makabila mengi.

Tokea nchi za kiafrika zianze kupata uhuru, miaka 60+ iliyopita, zoezi la kuunda nchi za makabila mengi limekuwa gumu kupita kiasi. Naweza sema ni Tanzania pekee walau imepiga hatua kidogo katika hilo. Nchi zingine imeshindikana kabisa. Rwanda walichinjana kikatili sababu hiyo. Ethiopia bado wapo vitani, Darfur watu walichinjwa kama wanyama. Nigeria haieleweki hata kidogo. Angalia karibu kila taifa la Afrika utaona kuwa zoezi la kuunda nchi ya watu wa makabila tofauti limeshindikana kabisa.

Ukiangalia hali halisi utaona kuwa Nchi ya makabila mengi haiwezi kuwa sawa, na kuwa kila kabila lilipaswa kuwa nchi, kama ilivyokuwa kwa maelfu ya miaka.
Ungekuwa Rais wa nchi ipi.
Inaonekana unapenda kuwa Rais, unapotaja wafaransa una maanisha mkusanyiko wa makabila ndani ya nchi ya ufaransa. Sijaizunguka sana Dunia hii ila ulikuta wapi nchi yenye kabila Moja?
 
Back
Top Bottom