Hakuna sababu ya msingi ya Diaspora wa Kenya kuwa na haki tofauti na wa Tanzania!

Kamundu

Platinum Member
Nov 22, 2006
6,609
8,753
Tukiacha ushabiki na kulishwa maneno kama majibu ya maswali yote mawili kwako ni "Ndiyo" basi unatakiwa kuunga mkono dual citizenship kwa wazawa wa Tanzania

1. Je unataka Watanzania wazawa ambao wako nje (Disapora) wapate haki sawa kwenye jumuia ya Africa mashariki kama wenzao wa Kenya na nchi nyingine? Kwa sheria za sasa diaspora wa kenya ana haki nyingi Tanzania kuliko diaspora ambaye ni mzawa wa Tanzania kwasababu diaspora wa Kenya anakuja kama Raia wa Kenya na huyu wa Tanzania anakuja kama mgeni/tourist.

2. Je unataka Watanzania Dispora huko walipo wawe ha haki sawa kama diaspora wa nchi nyingine?.

Hakuna Mtanzania namjua mimi amewahi kukana Uraia. Kukana Uraia ni utaratibu ambao una kuwa na barua ha hati ya kukana au kiapo cha kukana. Sifahamu mtu ambaye amekana Uraia wa Tanzania. Sheria ya Tanzania ndiyo inalazimisha neno Kukana na hii ndiyo kesi iliyopo mahakamani.

Uraia wa huko wanapoishi utawasaidia mambo ya msingi kama
(1) Kupata kazi nzuri
(2) Kupata bima za maisha
(3) Kuweza kusomesha watoto
(4) Kuhakikisha uwekezaji wao unalindwa kisheria.

Ngoja niwape mfano mdogo mimi binafsi mke wangu ambaye hakuwa na Uraia wa USA alikuwa na kuumwa sawa baada ya kumleta kutoka Tanzania. Tulipoenda Hospitali wakasema ni lazima afanyiwe operesheni haraka sana Vipimo tu vilikuwa $30,000 lakini operesheni ilikuwa $235,000. Mimi kwasababu ya bima yangu ambayo nisingeweza kuipata kama nisingekuwa Raia nililipia $3,000 tu na sio $265,000 ambazo ni gharama halisi. Hata Watanzania wenzangu wasingeweza kunisaidia.

Hizi ndiyo sababu kubwa za diaspora kuchukuwa Uraia wa nchi nyingine. Huwezi kukaa sehemu unafanya kazi usaidie familia nyumbani halafu tena kuna haki huna wakati wenzako wa kenya ambao mnashindana kwenye kazi hizo hizo wana haki zote. Hivyo badala ya kulishwa maneno tuwaulize kwanza diaspora ni kwanini wamechukuwa Uraia wa nchi wanazokaa na majibu kwa wanaojua sio ya kibinafsi bali ni ya kifamilia.

Hii ndiyo sababu umeona mabalozi wengi wa Tanzania wanaunga mkono kwasababu wanaelewa maisha halisi ya huku.
 
Tukiacha ushabiki na kulishwa maneno kama majibu ya maswali yote mawili kwako ni "Ndiyo" basi unatakiwa kuunga mkono dual citizenship kwa wazawa wa tanzania
Kama kuna mtu atakupa jibu sahihi kwenye maswali yako ya msingi unipigie simu +1 000-123-7654

Watanzania wengi sana wanaamini kuwa mtanzania anayefanya kazi nje ya nchi ama ana hela nyingi sana au ni mtu fulani ...................; kuna neno la kiswahili nimeshindwa kulipata lakini linafanana na Betrayer wa nchi.

Wanasahau kuwa mtu huyo ana ndugu zake na hata wazazi wake huko huko Tanzania ambao huenda wanamtegema yeye kwa kiasi kikubwa sana. Mtanzania huyo hataweza kupata haki huko Kenya kama Mtanzania tofauti na ambavyo Mkenya mwenye hadhi kama yeye huko ughaibuni waliko akiingia Tanzania atapewa hadhi kama Mkenya.
 
Tuwe na Diaspora kama Lema, Lissu Wenje ambao wanaweza kulikoroga hapa Bongo kisha wakakimbilia UK kuishi, sio?
 
Kama kuna mtu atakupa jibu sahihi kwenye maswali yako ya msingi unipigie simu +1 000-123-7654

Watanzania wengi sana wanaamini kuwa mtanzania anayefanya kazi nje ya nchi ama ana hela nyingi sana au ni mtu fulani ...................; kuna neno la kiswahili nimeshindwa kulipata lakini linafanana na Betrayer wa nchi.

Wanasahau kuwa mtu huyo ana ndugu zake na hata wazazi wake huko huko Tanzania ambao huenda wanamtegema yeye kwa kiasi kikubwa sana. Mtanzania huyo hataweza kupata haki huko Kenya kama Mtanzania tofauti na ambavyo Mkenya mwenye hadhi kama yeye huko ughaibuni waliko akiingia Tanzania atapewa hadhi kama Mkenya.
Ngugu yangu, tatizo la watz wengi walilishwa siasa za zamanu za ujamaa,kutaka wanancgi wake wasiende nje kutafuta riziki, kama ambavyo wengine waliobaki wanatafuta. Sasa kulipelekea wale wanaotaka kwenda nje kutafuta fursa fursa na riziki wanaonekana ni kama ' wasaliti' fulani' hivi na labda wanafaidi sana wakati bado walitegemea kutaka kuwasaidia Kwa ukamilifu nduu na jamii waliyoiacha nyumbani Tz...taswira hiyo ya wanaopinga uraia pacha bado Iko kwenye mawazo hayo ya nchi za kijamaa bila kujaribu kuona Kwa uzito faida zake zaidi ya hasara itakayopatikana Kwa kuruhusu uraia pacha....tatizo ninaloiona kubwa Kwa Tz bado Kuna ' hangover ya siasa za ujamaa' zinakuwa zinakwamisha mambo mengi ya kupiga hatua mbele za maendeleo..
 
Ngugu yangu, tatizo la watz wengi walilishwa siasa za zamanu za ujamaa,kutaka wanancgi wake wasiende nje kutafuta riziki, kama ambavyo wengine waliobaki wanatafuta. Sasa kulipelekea wale wanaotaka kwenda nje kutafuta fursa fursa na riziki wanaonekana ni kama ' wasaliti' fulani' hivi na labda wanafaidi sana wakati bado walitegemea kutaka kuwasaidia Kwa ukamilifu nduu na jamii waliyoiacha nyumbani Tz...taswira hiyo ya wanaopinga uraia pacha bado Iko kwenye mawazo hayo ya nchi za kijamaa bila kujaribu kuona Kwa uzito faida zake zaidi ya hasara itakayopatikana Kwa kuruhusu uraia pacha....
Ujamaa ulikufa Tanzania mwaka 1987 nikiwa mwanafunzi wa chuo kikuu. Leo ni zaidi ya miaka 35 na watanzania wengi hawakuishi ndani ya ujamaa. Tatizo ni la viongozi tu.
 
Tukiacha ushabiki na kulishwa maneno kama majibu ya maswali yote mawili kwako ni "Ndiyo" basi unatakiwa kuunga mkono dual citizenship kwa wazawa wa Tanzania

1. Je unataka Watanzania wazawa ambao wako nje (Disapora) wapate haki sawa kwenye jumuia ya Africa mashariki kama wenzao wa Kenya na nchi nyingine? Kwa sheria za sasa diaspora wa kenya ana haki nyingi Tanzania kuliko diaspora ambaye ni mzawa wa Tanzania kwasababu diaspora wa Kenya anakuja kama Raia wa Kenya na huyu wa Tanzania anakuja kama mgeni/tourist.

2. Je unataka Watanzania Dispora huko walipo wawe ha haki sawa kama diaspora wa nchi nyingine?.

Hakuna Mtanzania namjua mimi amewahi kukana Uraia. Kukana Uraia ni utaratibu ambao una kuwa na barua ha hati ya kukana au kiapo cha kukana. Sifahamu mtu ambaye amekana Uraia wa Tanzania. Sheria ya Tanzania ndiyo inalazimisha neno Kukana na hii ndiyo kesi iliyopo mahakamani.

Uraia wa huko wanapoishi utawasaidia mambo ya msingi kama
(1) Kupata kazi nzuri
(2) Kupata bima za maisha
(3) Kuweza kusomesha watoto
(4) Kuhakikisha uwekezaji wao unalindwa kisheria.

Ngoja niwape mfano mdogo mimi binafsi mke wangu ambaye hakuwa na Uraia wa USA alikuwa na kuumwa sawa baada ya kumleta kutoka Tanzania. Tulipoenda Hospitali wakasema ni lazima afanyiwe operesheni haraka sana Vipimo tu vilikuwa $30,000 lakini operesheni ilikuwa $235,000. Mimi kwasababu ya bima yangu ambayo nisingeweza kuipata kama nisingekuwa Raia nililipia $3,000 tu na sio $265,000 ambazo ni gharama halisi. Hata Watanzania wenzangu wasingeweza kunisaidia.

Hizi ndiyo sababu kubwa za diaspora kuchukuwa Uraia wa nchi nyingine. Huwezi kukaa sehemu unafanya kazi usaidie familia nyumbani halafu tena kuna haki huna wakati wenzako wa kenya ambao mnashindana kwenye kazi hizo hizo wana haki zote. Hivyo badala ya kulishwa maneno tuwaulize kwanza diaspora ni kwanini wamechukuwa Uraia wa nchi wanazokaa na majibu kwa wanaojua sio ya kibinafsi bali ni ya kifamilia.

Hii ndiyo sababu umeona mabalozi wengi wa Tanzania wanaunga mkono kwasababu wanaelewa maisha halisi ya huku.


1. Umefanya kosa kubwa sana kuingiza Kenya kwa haya maneno. Ni uchungu kuona ukieneza chuki na uhasama kwa Wakenya ambapo hawahusiki. Naona kama wewe ni wale wenye chuki kwa Wakenya zisizo na misingi Kenya haihusiki kamwe kwa haya maneno.

2. Kuna kitu cha mzingi sana naomba nikuelimishe. Kenya tuna dual citizenship kwa katiba. Hivyo mtu akienda ulaya achukue uraiya wa, tusema Marekani, bado atabaki na uraiya wa Kenya.
TZ hamna sheria kama hii. Ukichukua uraiya wa U.S. unapoteza wa TZ. Wewe sio raiya wa TZ tena kisheria, japo umezaliwa TZ. Marekani haiko ndani ya EAC. Hivyo kama una ulichukua uraiya wa Marekani hauko entitled kupata haki/privileges kama raiya wa EAC! Nadhani umeelewa sasa.

3. TZ, UG, KE, RW, Congo & Burundi zote ni wanachama wa jumuiya ya EAC. Na raiya wote wa member states wana haki/privileges zinazoambatana na makubaliano ya member states. Kwa hivyo privileges na haki anazopata Mkenya ndizo anapata Mrwanda, Mganda, na Mkongo akija TZ. Pia Mtz akienda nchi za EAC ata-enjoy haki/privilaged hizo hizo. Hakuna special treatment ya Wakenya pekee. Hizo ni haki walopewa raia wote wa EAC.

4. Ndio maana nasema umefanya kosa kuingiza Kenya kwenye huu uzi maana shida ipo kwenye katiba yeni ya Tanzania. Mnastaili kuwa na dual citizenship.
 
Tukiacha ushabiki na kulishwa maneno kama majibu ya maswali yote mawili kwako ni "Ndiyo" basi unatakiwa kuunga mkono dual citizenship kwa wazawa wa Tanzania

1. Je unataka Watanzania wazawa ambao wako nje (Disapora) wapate haki sawa kwenye jumuia ya Africa mashariki kama wenzao wa Kenya na nchi nyingine? Kwa sheria za sasa diaspora wa kenya ana haki nyingi Tanzania kuliko diaspora ambaye ni mzawa wa Tanzania kwasababu diaspora wa Kenya anakuja kama Raia wa Kenya na huyu wa Tanzania anakuja kama mgeni/tourist.

2. Je unataka Watanzania Dispora huko walipo wawe ha haki sawa kama diaspora wa nchi nyingine?.

Hakuna Mtanzania namjua mimi amewahi kukana Uraia. Kukana Uraia ni utaratibu ambao una kuwa na barua ha hati ya kukana au kiapo cha kukana. Sifahamu mtu ambaye amekana Uraia wa Tanzania. Sheria ya Tanzania ndiyo inalazimisha neno Kukana na hii ndiyo kesi iliyopo mahakamani.

Uraia wa huko wanapoishi utawasaidia mambo ya msingi kama
(1) Kupata kazi nzuri
(2) Kupata bima za maisha
(3) Kuweza kusomesha watoto
(4) Kuhakikisha uwekezaji wao unalindwa kisheria.

Ngoja niwape mfano mdogo mimi binafsi mke wangu ambaye hakuwa na Uraia wa USA alikuwa na kuumwa sawa baada ya kumleta kutoka Tanzania. Tulipoenda Hospitali wakasema ni lazima afanyiwe operesheni haraka sana Vipimo tu vilikuwa $30,000 lakini operesheni ilikuwa $235,000. Mimi kwasababu ya bima yangu ambayo nisingeweza kuipata kama nisingekuwa Raia nililipia $3,000 tu na sio $265,000 ambazo ni gharama halisi. Hata Watanzania wenzangu wasingeweza kunisaidia.

Hizi ndiyo sababu kubwa za diaspora kuchukuwa Uraia wa nchi nyingine. Huwezi kukaa sehemu unafanya kazi usaidie familia nyumbani halafu tena kuna haki huna wakati wenzako wa kenya ambao mnashindana kwenye kazi hizo hizo wana haki zote. Hivyo badala ya kulishwa maneno tuwaulize kwanza diaspora ni kwanini wamechukuwa Uraia wa nchi wanazokaa na majibu kwa wanaojua sio ya kibinafsi bali ni ya kifamilia.

Hii ndiyo sababu umeona mabalozi wengi wa Tanzania wanaunga mkono kwasababu wanaelewa maisha halisi ya huku.
Kwanza, ya Kenya ni ya Kenya, ya kwetu ni ya kwetu, kama ni rahisi na kumbe ni vizuri kuwa raia wa Kenya, nenda huko.

Kuhusu benefits za kuwa raia wa US, unazipataje? Ni lazima uwe raia wao. Ni rahisi kuchukua uraia wao just like that? Basi chukua. Kama wana masharti, ni masharti gani hayo? Kamani rahisi, yatimize. Kama siyo rahisi, mathalani kwanza uikane Tanzania, basi jipime kipi kimojawapo.

Kama unaipenda Tanzania, una baba yako, njoo umsaidie ni baba yako hakuna atakayekuzuia. Ukimaliza rudi zako USA au tuna hela "remittance" titazipokea hamna kodi.

Masharti ya USA ni haya:

What does it mean? The Oath asks you to let go of loyalty to the government of your home country. This is important because the U.S. wants its citizens to be loyal to the United States. The Oath also asks you to support the Constitution and to defend its values. It says:
SO HELP ME GOD.

Yaani hata Mungu unamtaka alkane Tanzania.
 
Sema Bado natafakari hiyo Operation ya $235,000.
Unaweza kuwa sawa kwa sababu watu nimatajiri wanaweza kuilipa, yaani ikibidi wachague kimoja wapo kati ya kufa au kuzilipa, wanaona rahisi kuzilipa kwa vile ema wanazo mfukoni au Serkali yao iko tayari kuzilipa. Serkali inazitoa wapi? Kwenye kodi za raia wake. Wewe siyoraia wake hujachangia kwa nini ikulipie?
 
Ngugu yangu, tatizo la watz wengi walilishwa siasa za zamanu za ujamaa,kutaka wanancgi wake wasiende nje kutafuta riziki, kama ambavyo wengine waliobaki wanatafuta. Sasa kulipelekea wale wanaotaka kwenda nje kutafuta fursa fursa na riziki wanaonekana ni kama ' wasaliti' fulani' hivi na labda wanafaidi sana wakati bado walitegemea kutaka kuwasaidia Kwa ukamilifu nduu na jamii waliyoiacha nyumbani Tz...taswira hiyo ya wanaopinga uraia pacha bado Iko kwenye mawazo hayo ya nchi za kijamaa bila kujaribu kuona Kwa uzito faida zake zaidi ya hasara itakayopatikana Kwa kuruhusu uraia pacha....tatizo ninaloiona kubwa Kwa Tz bado Kuna ' hangover ya siasa za ujamaa' zinakuwa zinakwamisha mambo mengi ya kupiga hatua mbele za maendeleo..
Wapi Ujamaa unasema mtu asiende nje? Mbona walienda nje wengi tu - Nyerere, Jussa, Kabudi, Baregu, Pengo, Lipumba, baadaye wakarudi kwao kusaidia ndugu zao. Ni sawa kabisa kwenda kokote kule au hapa kujitafutia maisha bora, laki fuata masharti YA NCHI HIZO. Wakisema uukane Uraia wa nchi yako, chagua. Wakisema hakuna ulazima kuwa raia wao watapata mafao hivi hivi tu basi uraia wao hauna lazima endelea kula huku na huku.
 
Kama kuna mtu atakupa jibu sahihi kwenye maswali yako ya msingi unipigie simu +1 000-123-7654

Watanzania wengi sana wanaamini kuwa mtanzania anayefanya kazi nje ya nchi ama ana hela nyingi sana au ni mtu fulani ...................; kuna neno la kiswahili nimeshindwa kulipata lakini linafanana na Betrayer wa nchi.

Wanasahau kuwa mtu huyo ana ndugu zake na hata wazazi wake huko huko Tanzania ambao huenda wanamtegema yeye kwa kiasi kikubwa sana. Mtanzania huyo hataweza kupata haki huko Kenya kama Mtanzania tofauti na ambavyo Mkenya mwenye hadhi kama yeye huko ughaibuni waliko akiingia Tanzania atapewa hadhi kama Mkenya.
JIBU SAHIHI NI MOJA TU, HILI HAPA SOMA MWENYEWE. AU NENDA UBALOZINI USA PALE DRIVE-IN KESHO THEN UKASOME MWENYEWE:

**************************************************
It says: “I hereby declare, on oath, that I absolutely and entirely renounce and abjure all allegiance and fidelity to any foreign prince, potentate, state, or sovereignty, of whom or which I have heretofore been a subject or citizen; that I will support and defend the Constitution and laws of the United States of America against all enemies, foreign and domestic; that I will bear true faith and allegiance to the same; that I will bear arms on behalf of the United States when required by the law; that I will perform noncombatant service in the Armed Forces of the United States when required by the law; that I will perform work of national importance under civilian direction when required by the law; and that I take this obligation freely, without any mental reservation or purpose of evasion; so help me God.”
**************************************************
 
Kwanza, ya Kenya ni ya Kenya, ya kwetu ni ya kwetu, kama ni rahisi na kumbe ni vizuri kuwa raia wa Kenya, nenda huko.

Kuhusu benefits za kuwa raia wa US, unazipataje? Ni lazima uwe raia wao. Ni rahisi kuchukua uraia wao just like that? Basi chukua. Kama wana masharti, ni masharti gani hayo? Kamani rahisi, yatimize. Kama siyo rahisi, mathalani kwanza uikane Tanzania, basi jipime kipi kimojawapo.

Kama unaipenda Tanzania, una baba yako, njoo umsaidie ni baba yako hakuna atakayekuzuia. Ukimaliza rudi zako USA au tuna hela "remittance" titazipokea hamna kodi.

Masharti ya USA ni haya:

What does it mean? The Oath asks you to let go of loyalty to the government of your home country. This is important because the U.S. wants its citizens to be loyal to the United States. The Oath also asks you to support the Constitution and to defend its values. It says:
SO HELP ME GOD.

Yaani hata Mungu unamtaka alkane Tanzania.
Kama kawaida vipuuzi lazima vichomekee ujinga wao na kumwaga sumu ili mradi navyo vionekane vipo, vitu kama huelewi au havikuhusu ni bora kusikiliza na kuuliza maswali kuliko hizi sumu
 
Kwanza, ya Kenya ni ya Kenya, ya kwetu ni ya kwetu, kama ni rahisi na kumbe ni vizuri kuwa raia wa Kenya, nenda huko.

Kuhusu benefits za kuwa raia wa US, unazipataje? Ni lazima uwe raia wao. Ni rahisi kuchukua uraia wao just like that? Basi chukua. Kama wana masharti, ni masharti gani hayo? Kamani rahisi, yatimize. Kama siyo rahisi, mathalani kwanza uikane Tanzania, basi jipime kipi kimojawapo.

Kama unaipenda Tanzania, una baba yako, njoo umsaidie ni baba yako hakuna atakayekuzuia. Ukimaliza rudi zako USA au tuna hela "remittance" titazipokea hamna kodi.

Masharti ya USA ni haya:

What does it mean? The Oath asks you to let go of loyalty to the government of your home country. This is important because the U.S. wants its citizens to be loyal to the United States. The Oath also asks you to support the Constitution and to defend its values. It says:
SO HELP ME GOD.

Yaani hata Mungu unamtaka alkane Tanzania.


Unaongea kama ugomvi sisi tunaongelea maendeo ya nchi na watu sio mambo na fikra za chuki binafsi na vikundi bila sababu ya maana. Ukisema " Ya Kenya ni ya Kenya" umejibu hoja gani hapo au swali gani hasa umejibu. Na jibu lako linasaidia vipi jamii yetu. Faida ya sheria za diaspora za kenya zipo wazi kuliko Tanzania. Hakuna yeyote mwenye data za kiuchumi zinazo onyesha matatizo kwa taifa hilo kwasababu ya uraia pacha au sheria za namna hiyo badala yake ni faida tu. Kuhusu kuchagua hakuna mtu kachagua kuzaliwa Tanzania ni Mungu ndiye anachagua wewe ni nani sio binadamu. Kumnyima mtu passport haina maana sio Mtanzania. Utanzania sio kibali ni DNA ya mtu na haibadilishiki. Hapa tunaongelea vibali tu.
 
1. Umefanya kosa kubwa sana kuingiza Kenya kwa haya maneno. Ni uchungu kuona ukieneza chuki na uhasama kwa Wakenya ambapo hawahusiki. Naona kama wewe ni wale wenye chuki kwa Wakenya zisizo na misingi Kenya haihusiki kamwe kwa haya maneno.

2. Kuna kitu cha mzingi sana naomba nikuelimishe. Kenya tuna dual citizenship kwa katiba. Hivyo mtu akienda ulaya achukue uraiya wa, tusema Marekani, bado atabaki na uraiya wa Kenya.
TZ hamna sheria kama hii. Ukichukua uraiya wa U.S. unapoteza wa TZ. Wewe sio raiya wa TZ tena kisheria, japo umezaliwa TZ. Marekani haiko ndani ya EAC. Hivyo kama una ulichukua uraiya wa Marekani hauko entitled kupata haki/privileges kama raiya wa EAC! Nadhani umeelewa sasa.

3. TZ, UG, KE, RW, Congo & Burundi zote ni wanachama wa jumuiya ya EAC. Na raiya wote wa member states wana haki/privileges zinazoambatana na makubaliano ya member states. Kwa hivyo privileges na haki anazopata Mkenya ndizo anapata Mrwanda, Mganda, na Mkongo akija TZ. Pia Mtz akienda nchi za EAC ata-enjoy haki/privilaged hizo hizo. Hakuna special treatment ya Wakenya pekee. Hizo ni haki walopewa raia wote wa EAC.

4. Ndio maana nasema umefanya kosa kuingiza Kenya kwenye huu uzi maana shida ipo kwenye katiba yeni ya Tanzania. Mnastaili kuwa na dual citizenship.

Naona unakubaliana na mimi kwamba katiba ya Tanzania inatakiwa iwe na kifungu kama cha kenya. Nakubaliana na wewe na umenisaidia kuelewesha watu Lakini kikubwa haujasema hata baya moja la Dual Citizenship ! yakushukuru sana
 
JIBU SAHIHI NI MOJA TU, HILI HAPA SOMA MWENYEWE. AU NENDA UBALOZINI USA PALE DRIVE-IN KESHO THEN UKASOME MWENYEWE:

**************************************************
It says: “I hereby declare, on oath, that I absolutely and entirely renounce and abjure all allegiance and fidelity to any foreign prince, potentate, state, or sovereignty, of whom or which I have heretofore been a subject or citizen; that I will support and defend the Constitution and laws of the United States of America against all enemies, foreign and domestic; that I will bear true faith and allegiance to the same; that I will bear arms on behalf of the United States when required by the law; that I will perform noncombatant service in the Armed Forces of the United States when required by the law; that I will perform work of national importance under civilian direction when required by the law; and that I take this obligation freely, without any mental reservation or purpose of evasion; so help me God.”
**************************************************

Mjinga mjinga sasa unasemaje kuhusu Kenya na nchi zenye Dual na uraia wa Marekani. Yaani unaonyesha kama vile ukiwa na USA citizenship huwezi kuwa na Uraia mwingine na hii sio kweli. Hujui chochote hapa inaelekea. Useme tu ukweli unachukia tu hapa na utatafuta chochote hata vya uongo kuongesha hili.

Pili hata haujui USA.

Mambo ya Uraia yapo kwenye Homeland security na balozi zao haziko kwenye wizara hii zipo foreign affairs !
 
Wewe mtu huchoki kulilia nyumbani, si rudi tu huko, kwani ni nani anayekushikilia kuwa mTanzania?

Usitegemee hata siku moja Tanzania kuwa Kenya. Tanzania ni Tanzania, usiwe unapenda kuleta mambo ya Kenya yawe ya Tanzania.
Sidhani kama umeilewa hoja yake.
 
Sidhani kama umeilewa hoja yake.
Mkuu 'jmushi', huwa sibahatishi wala kusema nisichokielewa. Ninaposoma habari yoyote kutoka kwa mchangiaji yeyote humu JF, sikurupuki, kuna historia inayohusika.

Kwa hiyo usidhani nilivyoandika hapo sikijui nilichoandika, kuna historia ndefu nyuma yake na huyo niliyemjibu anaifahamu vyema historia hiyo.
Kwako mtu wa pembeni utaona kama ulivyoona wewe, kwa hiyo sikulaumu.
 
Back
Top Bottom