Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

Muuaji ni Hans, sikujua kama uzi huu una utamu kiasi hiki.wee mizambwa weeeee niletee wakili wa moyo wangu.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu siku hizi kuna li pepo la maringo limekuingia huku la ubishi na kutosikiliza maneno ya kubwa zako likianza kukunyemelea ...lol.... sasa nakemea ya shindwe na ya rudi yalipotoka. Ili urudi kuwa mtu mwema kama ulivyoanza kurusha hii hadithi.
 
Wakili wa Moyo-31



ILIPOISHIA:
"Tutawarudishia fedha zao."
"Wee mwana tutazipata wapi?"
"Mi najua pa kuzipata."
SASA ENDELEA...


"Hebu mwanangu nieleza tatizo nini, kama Colin amekukosea bado tuna nafasi ya kuzungumza tukalimaliza."

"Mama Colin hajawahi kunikosea toka tujuane, ila mimi ndiye nimekuwa nikimkosea muda wote. Najua ananipenda sana na uamuzi wangu utamchanganya, lakini ukweli utabakia palepale si chaguo la moyo wangu. Nimejilazimisha kumpenda lakini moyo umekataa hivyo sina budi kuusikiliza moyo wangu unachotaka.

"Siku zote moyo wa mtu huwa ndiyo muamuzi kwa jambo lolote kwa vile wenyewe ndiyo unaopokea furaha kwa jambo zuri au la huzuni kwa jambo baya."

"Kwa hiyo unasema hujakosana na Colin?"

"Walaa, najua Colin ananipenda sana na ataumizwa na uamuzi wangu lakini sina jinsi kila ndege hutua mti aupendao."

"Mage upo sawa mwanangu?"

"Nipo sawa mama."

Kauli ile ilimfanya mama yake akae kwenye kitanda baada ya miguu kukosa nguvu.

"Mage mwanangu mbona sikuelewi, kipi kimekusibu mama?"

"Mama najua itakuwa vigumu kunielewa lakini utanielewa tu."

Mara simu ya Mage iliita, aliichukua na kuitazama na kuirudisha bila kuipokea kitu kilichomfanya mama yake kuuliza.

"Mbona hupokei kwani inatoka wapi?"

"Kwa Colin."

"Sasa kwa nini hupokei?"

"Sasa nitazungumza naye nini?"

"Pokea mwambie leo huwezi kwenda, hujisikii vizuri."

"Siwezi kuzungumza naye kwa leo, nitajisikia vibaya."

Simu iliita tena lakini haikupokelewa mpaka ikakatika, baada ya muda msichana wa kazi alimwita mama Mage kuwa kuna simu yake inaita.
Alitoka na kuichukua, ilikuwa inatoka kwa mama Colin, akaipokea mara moja.

"Haloo dada."

"Eeh! Kuna usalama huko?"

"Kiasi."

"Kulikoni?"

"Mage kichwa kilimshika ghafla."

"Jamani mkwe wangu! Vipi hali yake?"

"Kidogo hajambo amelala kwa sasa."

"Basi tunakuja kumuona."

"Usisumbuke, hayupo serious sana."

"Basi augue pole maana mwenzake alikuwa na wasiwasi baada ya kupiga simu bila kupokelewa."
"Mwambie asiwe na wasiwasi ni kichwa tu lakini anaendelea vizuri kesho atakuwa hajambo."

"Basi niwatakie usiku mwema."

"Na ninyi pia."

Mama Colin baada ya kumaliza kuzungumza, alimgekia mwanaye aliyekuwa pembeni yake akifuatilia mazungumzo yale.

"Vipi mama?"

"Kumbe kichwa kilimshika ghafla amekunywa dawa kimetulia, alitaka kuja lakini mama yake kamwambia alale kwa leo atakuja kesho."

"Duh! Afadhali, nilikuwa na wasiwasi sana."

"Kapumzike, kesho mchumba wako atakuja."

"Sawa mama."

Colin alikwenda chumbani kwake, kabla ya kulala alichukua simu yake na kuangalia picha zote alizopiga na Mage na nyingine iliyopigwa siku ile mchana aliyotumiwa na Mage alipokuwa na shoga yake Brenda Mlimani City- Samakisamaki.
Aliibusu picha kubwa ya mpenzi wake iliyokuwa katika tabasamu la kufa mtu na kusema kwa sauti ya chini.

"Mage wewe ndiye mke wa maisha yangu," aliikumbatia na kujilaza.

***

Mama Mage usingizi uligoma kabisa na kukiona kichwa kikitaka kupasuka kutokana na kuchanganywa na kauli ya mwanaye, alijiuliza kama mwanaye atasimamia uamuzi ule angeuweka wapi uso wake, wasiwasi wake huenda amemfumania Colin na mwanamke mwingine na kuamua kuvunja uchumba.

Bado aliona kama ni hivyo linazungumzika kwa vile wote wamejuana wakiwa tayari wanayajua mapenzi. Alinyanyuka kitandani na kutoka kwenda kwa mwanaye kupata ukweli kwani alikuwa amechanganyikiwa sana.

Alitoka taratibu, taa ya sebuleni ilikuwa imezimwa. Kulikuwa na hali ya ukimya kutokana na watu wote kuwa wamelala.

Hakutaka kuwasha taa ya sebuleni, alitembea taratibu hadi chumba cha Mage. Alipotaka kuushika mlango, alimsikia mwanaye akizungumza na simu, alitulia ili asikilize anazungumza nini na nani. Alimsikia mwanaye akisema:

"Kama hivyo nimeisha tibua yote kwa ajili ya mapenzi yangu mazito kwako, kama umejitoa muhanga kwa ajili yangu nami sina budi kujitoa kwa ajili yako. Najua uamuzi wangu utamchanganya mama na yule mchovu lakini wewe ni zaidi yao wote, nakupenda sana zaidi ya kukupenda. Nipo radhi vyote duniani viondoke ubakie peke yako.

"Please mpenzi usinitende, kosa lako ni mauti yangu, nashukuru kwa kujali mapenzi yangu kwako. Asante mpenzi wangu naomba ulale usingizi


ITAENDELEA..................
 
Wakili wa Moyo-31



ILIPOISHIA:
“Tutawarudishia fedha zao.”
“Wee mwana tutazipata wapi?”
“Mi najua pa kuzipata.”
SASA ENDELEA...


“Hebu mwanangu nieleza tatizo nini, kama Colin amekukosea bado tuna nafasi ya kuzungumza tukalimaliza.”

“Mama Colin hajawahi kunikosea toka tujuane, ila mimi ndiye nimekuwa nikimkosea muda wote. Najua ananipenda sana na uamuzi wangu utamchanganya, lakini ukweli utabakia palepale si chaguo la moyo wangu. Nimejilazimisha kumpenda lakini moyo umekataa hivyo sina budi kuusikiliza moyo wangu unachotaka.

“Siku zote moyo wa mtu huwa ndiyo muamuzi kwa jambo lolote kwa vile wenyewe ndiyo unaopokea furaha kwa jambo zuri au la huzuni kwa jambo baya.”

“Kwa hiyo unasema hujakosana na Colin?”

“Walaa, najua Colin ananipenda sana na ataumizwa na uamuzi wangu lakini sina jinsi kila ndege hutua mti aupendao.”

“Mage upo sawa mwanangu?”

“Nipo sawa mama.”

Kauli ile ilimfanya mama yake akae kwenye kitanda baada ya miguu kukosa nguvu.

“Mage mwanangu mbona sikuelewi, kipi kimekusibu mama?”

“Mama najua itakuwa vigumu kunielewa lakini utanielewa tu.”

Mara simu ya Mage iliita, aliichukua na kuitazama na kuirudisha bila kuipokea kitu kilichomfanya mama yake kuuliza.

“Mbona hupokei kwani inatoka wapi?”

“Kwa Colin.”

“Sasa kwa nini hupokei?”

“Sasa nitazungumza naye nini?”

“Pokea mwambie leo huwezi kwenda, hujisikii vizuri.”

“Siwezi kuzungumza naye kwa leo, nitajisikia vibaya.”

Simu iliita tena lakini haikupokelewa mpaka ikakatika, baada ya muda msichana wa kazi alimwita mama Mage kuwa kuna simu yake inaita.
Alitoka na kuichukua, ilikuwa inatoka kwa mama Colin, akaipokea mara moja.

“Haloo dada.”

“Eeh! Kuna usalama huko?”

“Kiasi.”

“Kulikoni?”

“Mage kichwa kilimshika ghafla.”

“Jamani mkwe wangu! Vipi hali yake?”

“Kidogo hajambo amelala kwa sasa.”

“Basi tunakuja kumuona.”

“Usisumbuke, hayupo serious sana.”

“Basi augue pole maana mwenzake alikuwa na wasiwasi baada ya kupiga simu bila kupokelewa.”
“Mwambie asiwe na wasiwasi ni kichwa tu lakini anaendelea vizuri kesho atakuwa hajambo.”

“Basi niwatakie usiku mwema.”

“Na ninyi pia.”

Mama Colin baada ya kumaliza kuzungumza, alimgekia mwanaye aliyekuwa pembeni yake akifuatilia mazungumzo yale.

“Vipi mama?”

“Kumbe kichwa kilimshika ghafla amekunywa dawa kimetulia, alitaka kuja lakini mama yake kamwambia alale kwa leo atakuja kesho.”

“Duh! Afadhali, nilikuwa na wasiwasi sana.”

“Kapumzike, kesho mchumba wako atakuja.”

“Sawa mama.”

Colin alikwenda chumbani kwake, kabla ya kulala alichukua simu yake na kuangalia picha zote alizopiga na Mage na nyingine iliyopigwa siku ile mchana aliyotumiwa na Mage alipokuwa na shoga yake Brenda Mlimani City- Samakisamaki.
Aliibusu picha kubwa ya mpenzi wake iliyokuwa katika tabasamu la kufa mtu na kusema kwa sauti ya chini.

“Mage wewe ndiye mke wa maisha yangu,” aliikumbatia na kujilaza.

***

Mama Mage usingizi uligoma kabisa na kukiona kichwa kikitaka kupasuka kutokana na kuchanganywa na kauli ya mwanaye, alijiuliza kama mwanaye atasimamia uamuzi ule angeuweka wapi uso wake, wasiwasi wake huenda amemfumania Colin na mwanamke mwingine na kuamua kuvunja uchumba.

Bado aliona kama ni hivyo linazungumzika kwa vile wote wamejuana wakiwa tayari wanayajua mapenzi. Alinyanyuka kitandani na kutoka kwenda kwa mwanaye kupata ukweli kwani alikuwa amechanganyikiwa sana.

Alitoka taratibu, taa ya sebuleni ilikuwa imezimwa. Kulikuwa na hali ya ukimya kutokana na watu wote kuwa wamelala.

Hakutaka kuwasha taa ya sebuleni, alitembea taratibu hadi chumba cha Mage. Alipotaka kuushika mlango, alimsikia mwanaye akizungumza na simu, alitulia ili asikilize anazungumza nini na nani. Alimsikia mwanaye akisema:

“Kama hivyo nimeisha tibua yote kwa ajili ya mapenzi yangu mazito kwako, kama umejitoa muhanga kwa ajili yangu nami sina budi kujitoa kwa ajili yako. Najua uamuzi wangu utamchanganya mama na yule mchovu lakini wewe ni zaidi yao wote, nakupenda sana zaidi ya kukupenda. Nipo radhi vyote duniani viondoke ubakie peke yako.

“Please mpenzi usinitende, kosa lako ni mauti yangu, nashukuru kwa kujali mapenzi yangu kwako. Asante mpenzi wangu naomba ulale usingizi


Mkuu mbona umeruka sehemu ya 30? ITAENDELEA..................




Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 
Wakili wa Moyo-32


ILIPOISHIA:
Please mpenzi usinitende kosa lako ni mauti yangu, nashukuru kwa kujali mapenzi yangu kwako.
SASA ENDELEA...

Asante mpenzi wangu naomba ulale usingizi mororo huku ukiniota. I love you and i need you in all my life, mmmmwa."

Mama Mage alijiuliza mwanaye anazungumza na nani, wazo lake lilimpeleka labda ni Hans, lakini hakukubaliana nalo kutokana na maumivu aliyoyapata mwanaye kutoka kwa Hans na familia yake. Wazo lilielekea huenda kapata mpenzi mwingine ambaye kamzidi kete Colin.

Alishangaa mabadiliko yake ya ghafla kwani mpaka saa tatu kasoro usiku mwanaye alikuwa na kimuhemuhe cha kwenda kwa mchumba wake Colin na kumhimiza kuwahi.

Lakini aliporudi alikuta mambo yamebadilika ghafla kama saa sita mchana igeuke kiza totoro na watu wasionane.

Alipata wazo la kwenda chumbani kwa Sofia msichana wa kazi kumuuliza kuna kitu gani kilitokea kabla ya kurudi na kusababisha hali ile. Alikwenda kugonga chumba cha msichana wa kazi aliyeamka.

"Abee mama."

Mama Mage aliingia chumbani bila kusema kitu kisha alirudisha mlango na kumuuliza kwa sauti ya chini.

"Sofi."

"Abee mama."

"Eti nilipotoka, Mage alitoka?"

"Hapana hajatoka," Sofi alikataa huku akitikisa kichwa.

"Colin alikuja?"

"Hapana."

"Nani alikuja."

"Mmh! Da' Brenda."

"Brenda si alikuja mchana na kuondoka na Mage?"

"Hata usiku alikuja na kwenda chumbani kwa dada Mage kisha walitoka nje, baadaye nilimuona dada Mage akirudi peke yake huku ameshikilia kitambaa mkononi kama anafuta machozi lakini sikumtilia maanani."
"Mmh! Sasa nimeelewa," mama Mage alisema huku akishika mikono kiunoni.

"Kuna nini mama?" Sofi alishtushwa na kauli ya mama Colin.

"Kawaida, ila nimeelewa," alisema huku akitoka chumbani kwa Sofi na kurudi chumbani kwake.
Alipoingia chumbani alichukua simu na kumpigia Brenda ili amwambie alimpeleka wapi mwanaye mpaka kugeuka ghafla na kumtia gharama na fedheha kubwa.

Baada ya kupiga simu ya Brenda, ilipokelewa upande wa pili.

"Haloo mama."

"Brenda za sa hizi?"

"Nzuri mama."

"Eti Brenda kumetokea nini mama?"

"Kuhusu nini?"

"Ulimpekeka wapi Mage?"

"Sijampeleka popote, nilitoka naye nje mara moja akarudi ndani kujiandaa kwenda kwa shemeji Colin."

"Unajua wewe ndiye umevunja ndoa ya Mage?"

"Kivipi mama?" Brenda alishtuka.

"Umemwambia nini Mage mpaka akakataa kuolewa, gharama za harusi utazilipa wewe?"

"Mama kwa nini unasema hivyo?" Brenda alishtuka.

"Haiwezekani kuja wewe ghafla na Mage abadili uamuzi wa kuolewa."

"Mamaa! Hebu subiri," Brenda alikata simu na kumpigia Mage.

Baada ya kuita kwa muda, simu ilipokelewa.

"Haloo Brenda afadhali umenipigia."

"Mage kuna nini?"

"Nimevunja uchumba na Colin."

"Mungu wangu! Kwa nini tena?"

"Nimepata tiba ya moyo wangu."

"Mage unajua lawama zote nabebeshwa mimi?"

"Brenda walaa hilo halikuhusu, kila kitu kitaeleweka, nitazungumza na mama muda si mrefu."

"Mage ndugu yangu naomba usivunje ndoa yako utaniweka mahali pabaya," Brenda alimbembeleza Mage.

"Nitaolewaje na mtu nisiyempenda?"

"Mage leo yamekuwa hayo? Si ni wewe ndiye ulinihakikishia Colin ndiye tiba ya moyo wako."

"Hakuwa tiba bali dawa ya kupunguza maumivu lakini Hans ndiye tiba kamili, kama alijitoa kwa ajili yangu nami sina budi kujitoa kwa ajili yake."

"Colin anajua?"

"Hajajua ila sitaki mtu yeyote amwambie, nitamwambia mwenyewe nina imani tutaelewana tu."

"Mmh! Mbona najuta kiherehere cha kumleta Hans!" Brenda alijua yeye ndiye chanzo cha yote yaliyotokea.
Alijiuliza Hans alimweleza Mage kitu gani kilichomfanya abadili ghafla uamuzi wa kuolewa.

Aliamua kumpigia simu Hans kutaka kujua aliwambia nini Mage mpaka kuamua kuvunja uchumba wakati kila kitu kilikuwa kipo katika hatua za mwisho lakini simu ya Hans haikuwa hewani.

Alijikuta akijiuliza atamwambia nini mama Mage mpaka amuelewe. Usiku ulikuwa mrefu kwa Brenda na kujuta kwa nini alimkubalia Hans kwenda kuonana na Mage.


***

Siku ya pili, Mage aliamka asubuhi, akaoga na kujipamba kisha alitoka, alimkuta mama yake amekaa sebuleni ameshika tama.

"Mama vipi mbona hivyo?" alimuuliza huku akijilazimisha kujenga tabasamu.



Itaendelea................
 
Mwandishi unatuzungushaaa...hutaki kutuambia Hans alimwaga sumu gani....haya bwana
 
Back
Top Bottom