Hadithi: Wakili wa moyo

Hadithi: Wakili wa moyo

Wakili wa Moyo-26



ILIPOISHIA:
Mkuu wa Polisi, Mr. Clarence alimchukua Mage na kumrudisha nyumbani.
Mama yake alifurahi kumuona mwanaye akiwa na Mr. Clarence Mulisa.
"Asante shemeji."
"Kawaida, nina imani Hans akipata nafuu kila kitu kitakuwa wazi."

SASA ENDELEA...

"Tena Mungu ampe afya ili kuwaumbua wenye roho mbaya wanaotaka kuiharibu harusi ya mwanangu."

"Usiwe na wasiwasi, kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa na aliyetenda unyama ule atajulikana kwani mkono wa dola ni mrefu."

Mkuu wa polisi aliaga na kumuacha Mage na mama yake, baada ya kuondoka Mage aliangua kilio.

"Mama kosa langu nini? Mbona familia ya akina Hans wameniandama namna hii?, Mimi nimuue mke wa Hans pamoja na mwanaye ili iweje?"

"Ndiyo dunia ilivyo mwanangu, kwa vile baba yako yupo atakusimamia."

"Unajua mama mimi nilikuwa na wasiwasi labda aliyefanya vile ni Colin."

"Wee! Temea chini tena usirudie kusema kitu kama hicho, Hans na Colin wapi na wapi?" Mama yake alijibu kwa ukali.

"Basi mama nisamehe ni mawazo tu."

"Tena umeniudhi sana, wee kidogo ufe na presha kwa kusingiziwa unataka kumpaka shombo mtoto wa watu."

"Basi mama nisamehe, ulikuwa wasiwasi wangu."

"Nataka uoge ubadili nguo uende kwa mwenzio ukamtoe hofu usimueleze ya kupelekwa polisi."

"Sawa mama."

Mage alikwenda kuoga na kubadili nguo ambapo alichukua gari na kwenda kwa Colin, akiwa njiani alijawa na mawazo juu ya familia ya Hans.

Alijiuliza kipi hasa kilichofanya wamfikirie yeye kwanza. Aliona jinsi gani familia ile ilivyokuwa ikimchukia na kuamini kauli ya mama yake kuwa hata kama angeolewa asingedumu kwenye ndoa yake kwa vile hakuwa chaguo la familia.

Alijikuta taratibu mapenzi yake yote akiyahamishia kwa Colin na kuuapia moyo wake kumpenda kwa nguvu na akili zake zote. Alipofika nyumbani kwao Colin baada ya kuteremka kwenye gari aliingia ndani huku akikimbia kama mtu aliyepagawa. Sebuleni alimkuta mama Colin, alishtuka kumuona katika hali ile.

"Vipi Mage?"

"Mama, mume wangu yupo wapi?" aliuliza akionesha kuchanganyikiwa.

Wakati huo Colin alikuwa akitokea chumbani kwake kuja sebuleni, alipomuona alimkimbilia na kumkumbatia.
"Jamani mume wanguu!"

"Vipi mbona hivyo?" Colin alishtuka uchangamfu wa Mage uliopitiliza.

"Najua nimekuudhi nisamehe sana, mama nimemuudhi sana mume wangu," Mage alisema huku akilia.
"Hujamuudhi chochote," mama Colin alisema.

"Najua nimemuudhi, Colin naomba twende chumbani."

Walishikana mikono na kuelekea chumbani na kumuacha mama Colin akiwatazama na kuchekelea moyoni na kusema kwa sauti ya chini. "Kweli wanapendana." Aliwatazama mpaka walipopotea machoni kwake.
Colin na Mage walikwenda hadi chumbani, alipofika ndani Mage alijitupa kifuani kwa mpenzi wake na kuanza kulia kitu kilichomshtua Colin na kuhoji.

"Vipi mpenzi?"

"Colin nisamehe sana mpenzi wangu."

"Kwa lipi?"

"Najua leo nimekukosea kwa kuondoka bila kukuaga kitu kilichokufanya usumbuke kunitafuta, kibaya zaidi sijapokea simu zako na kukataa kuzungumza na wewe uliponifuata nyumbani."

"Kumbe ni hayo? Achana nayo."

"Hapana najua umenikubalia ili yaishe lakini umejenga picha mbaya juu yangu."

"Walaa."

"Colin nihukumu hukumu yoyote lakini elewa nakupenda sana mpenzi wangu, nilitaka kufanya surprise lakini ikaenda ndivyo sivyo. Nilishindwa nikueleze nini kwa vile sikuwa na la kukueleza kwa wakati ule hasa baada ya Brenda kunichanganya."

"Yote mama alinieleza ndiyo maana nilikuelewa toka asubuhi."

"Colin lakini si unajua nakupenda?" Mage alimuuliza kwa sauti ya kudeka.

"Najua, ndiyo maana upo hapa."

"Nashukuru kulifahamu hilo."

Siku ile Mage alishinda pale na kufanya kazi zote za nyumbani ikiwa ni pamoja na kupika chakula cha jioni. Colin alijikuta akisahau yote na kujiona kama tayari ameshamuoa Mage.
Siku ile muda wote walikuwa pamoja kama kumbikumbi kwa kufanya kazi kwa kusaidiana.
Mama Colin muda wote alikuwa mtu wa tabasamu na kuona ndoa ya mwanaye jinsi itakavyojaa furaha na upendo.

Aliwaangalia walivyopendeza kwa kusaidiana kazi zote za jikoni mtu na mchumba wake. Alifumbata mikono yake na kuomba kwa sauti ya chini.

"Eeh! Mwenyezi Mungu baba ijalie ndoa ya wanangu iwe yenye matunda," baada ya dua alipiga njia ya msalaba kumshukuru Mungu.

Siku ile ilikuwa ya furaha kwa wapenzi wawili kwa Mage ambaye alihamishia mapenzi yake yote kwa Colin baada ya kujua hata kama angempenda vipi Hans asingekuwa na nafasi ndani ya familia yake. Aliona jinsi gani isivyompenda mpaka kumzushia shutuma nzito za mauaji ya shambulio la kuua.

Kingine kilichomuweka njia panda kama Mungu atamsaidia Hans kupona atamchukuliaje, lazima naye angeamini muhusika ni yeye. Lakini kwa upande wa Hans alijua ni vigumu kumshuku yeye kutokana na ukaribu wao ulivyokuwa.

Angekuwa na wasiwasi kama angekuwa akilipigania penzi la Hans. Kama tatizo lile lingemtokea baada ya kuoa lazima Hans angejua ni yeye, lakini baada ya mkewe kupata ujauzito na kujifungua penzi lake alilizika rasmi.

Aliamini ule ndiyo muda wa kulionesha penzi lake halisi kwa Colin, siku ile alilala tena na kuondoka siku ya pili huku kila mmoja akifurahia penzi la mwenzake.

Ukaribu wa Mage na Colin kwa kufuatana muda wote kama kumbikumbi, ulifanya Colin ashindwe kutekeleza ahadi yake kwa kina Cecy. Baada ya kusubiri kwa wiki bila kuonekana dalili zozote za kutekelezwa ahadi. Cecy aliyekuwa amejilaza kitandani na kukosa usingizi.


Itaendelea............
 
Mkuu kwema? Hatuendelei tena? ??





Wakili wa Moyo-26



ILIPOISHIA:
Mkuu wa Polisi, Mr. Clarence alimchukua Mage na kumrudisha nyumbani.
Mama yake alifurahi kumuona mwanaye akiwa na Mr. Clarence Mulisa.
“Asante shemeji.”
“Kawaida, nina imani Hans akipata nafuu kila kitu kitakuwa wazi.”

SASA ENDELEA...

“Tena Mungu ampe afya ili kuwaumbua wenye roho mbaya wanaotaka kuiharibu harusi ya mwanangu.”

“Usiwe na wasiwasi, kila kitu kitakwenda kama kilivyopangwa na aliyetenda unyama ule atajulikana kwani mkono wa dola ni mrefu.”

Mkuu wa polisi aliaga na kumuacha Mage na mama yake, baada ya kuondoka Mage aliangua kilio.

“Mama kosa langu nini? Mbona familia ya akina Hans wameniandama namna hii?, Mimi nimuue mke wa Hans pamoja na mwanaye ili iweje?”

“Ndiyo dunia ilivyo mwanangu, kwa vile baba yako yupo atakusimamia.”

“Unajua mama mimi nilikuwa na wasiwasi labda aliyefanya vile ni Colin.”

“Wee! Temea chini tena usirudie kusema kitu kama hicho, Hans na Colin wapi na wapi?” Mama yake alijibu kwa ukali.

“Basi mama nisamehe ni mawazo tu.”

“Tena umeniudhi sana, wee kidogo ufe na presha kwa kusingiziwa unataka kumpaka shombo mtoto wa watu.”

“Basi mama nisamehe, ulikuwa wasiwasi wangu.”

“Nataka uoge ubadili nguo uende kwa mwenzio ukamtoe hofu usimueleze ya kupelekwa polisi.”

“Sawa mama.”

Mage alikwenda kuoga na kubadili nguo ambapo alichukua gari na kwenda kwa Colin, akiwa njiani alijawa na mawazo juu ya familia ya Hans.

Alijiuliza kipi hasa kilichofanya wamfikirie yeye kwanza. Aliona jinsi gani familia ile ilivyokuwa ikimchukia na kuamini kauli ya mama yake kuwa hata kama angeolewa asingedumu kwenye ndoa yake kwa vile hakuwa chaguo la familia.

Alijikuta taratibu mapenzi yake yote akiyahamishia kwa Colin na kuuapia moyo wake kumpenda kwa nguvu na akili zake zote. Alipofika nyumbani kwao Colin baada ya kuteremka kwenye gari aliingia ndani huku akikimbia kama mtu aliyepagawa. Sebuleni alimkuta mama Colin, alishtuka kumuona katika hali ile.

“Vipi Mage?”

“Mama, mume wangu yupo wapi?” aliuliza akionesha kuchanganyikiwa.

Wakati huo Colin alikuwa akitokea chumbani kwake kuja sebuleni, alipomuona alimkimbilia na kumkumbatia.
“Jamani mume wanguu!”

“Vipi mbona hivyo?” Colin alishtuka uchangamfu wa Mage uliopitiliza.

“Najua nimekuudhi nisamehe sana, mama nimemuudhi sana mume wangu,” Mage alisema huku akilia.
“Hujamuudhi chochote,” mama Colin alisema.

“Najua nimemuudhi, Colin naomba twende chumbani.”

Walishikana mikono na kuelekea chumbani na kumuacha mama Colin akiwatazama na kuchekelea moyoni na kusema kwa sauti ya chini. “Kweli wanapendana.” Aliwatazama mpaka walipopotea machoni kwake.
Colin na Mage walikwenda hadi chumbani, alipofika ndani Mage alijitupa kifuani kwa mpenzi wake na kuanza kulia kitu kilichomshtua Colin na kuhoji.

“Vipi mpenzi?”

“Colin nisamehe sana mpenzi wangu.”

“Kwa lipi?”

“Najua leo nimekukosea kwa kuondoka bila kukuaga kitu kilichokufanya usumbuke kunitafuta, kibaya zaidi sijapokea simu zako na kukataa kuzungumza na wewe uliponifuata nyumbani.”

“Kumbe ni hayo? Achana nayo.”

“Hapana najua umenikubalia ili yaishe lakini umejenga picha mbaya juu yangu.”

“Walaa.”

“Colin nihukumu hukumu yoyote lakini elewa nakupenda sana mpenzi wangu, nilitaka kufanya surprise lakini ikaenda ndivyo sivyo. Nilishindwa nikueleze nini kwa vile sikuwa na la kukueleza kwa wakati ule hasa baada ya Brenda kunichanganya.”

“Yote mama alinieleza ndiyo maana nilikuelewa toka asubuhi.”

“Colin lakini si unajua nakupenda?” Mage alimuuliza kwa sauti ya kudeka.

“Najua, ndiyo maana upo hapa.”

“Nashukuru kulifahamu hilo.”

Siku ile Mage alishinda pale na kufanya kazi zote za nyumbani ikiwa ni pamoja na kupika chakula cha jioni. Colin alijikuta akisahau yote na kujiona kama tayari ameshamuoa Mage.
Siku ile muda wote walikuwa pamoja kama kumbikumbi kwa kufanya kazi kwa kusaidiana.
Mama Colin muda wote alikuwa mtu wa tabasamu na kuona ndoa ya mwanaye jinsi itakavyojaa furaha na upendo.

Aliwaangalia walivyopendeza kwa kusaidiana kazi zote za jikoni mtu na mchumba wake. Alifumbata mikono yake na kuomba kwa sauti ya chini.

“Eeh! Mwenyezi Mungu baba ijalie ndoa ya wanangu iwe yenye matunda,” baada ya dua alipiga njia ya msalaba kumshukuru Mungu.

Siku ile ilikuwa ya furaha kwa wapenzi wawili kwa Mage ambaye alihamishia mapenzi yake yote kwa Colin baada ya kujua hata kama angempenda vipi Hans asingekuwa na nafasi ndani ya familia yake. Aliona jinsi gani isivyompenda mpaka kumzushia shutuma nzito za mauaji ya shambulio la kuua.

Kingine kilichomuweka njia panda kama Mungu atamsaidia Hans kupona atamchukuliaje, lazima naye angeamini muhusika ni yeye. Lakini kwa upande wa Hans alijua ni vigumu kumshuku yeye kutokana na ukaribu wao ulivyokuwa.

Angekuwa na wasiwasi kama angekuwa akilipigania penzi la Hans. Kama tatizo lile lingemtokea baada ya kuoa lazima Hans angejua ni yeye, lakini baada ya mkewe kupata ujauzito na kujifungua penzi lake alilizika rasmi.

Aliamini ule ndiyo muda wa kulionesha penzi lake halisi kwa Colin, siku ile alilala tena na kuondoka siku ya pili huku kila mmoja akifurahia penzi la mwenzake.

Ukaribu wa Mage na Colin kwa kufuatana muda wote kama kumbikumbi, ulifanya Colin ashindwe kutekeleza ahadi yake kwa kina Cecy. Baada ya kusubiri kwa wiki bila kuonekana dalili zozote za kutekelezwa ahadi. Cecy aliyekuwa amejilaza kitandani na kukosa usingizi.


Itaendelea............
 
Wakili wa Moyo-27



ILIPOISHIA:
Ukaribu wa Mage na Colin kwa kufuatana muda wote kama kumbikumbi, Ulifanya Colin ashindwe kutekeleza ahadi yake kwa kina Cecy. Baada ya kusubiri kwa wiki bila kuonekana dalili zozote za kutekelezwa ahadi. Cecy aliyekuwa amejilaza kitandani na kukosa usingizi.
SASA ENDELEA...


Alijikuta akinyanyuka kitandani na kumfuata mama yake aliyeamini ameshapitiwa na usingizi ambaye alikuwa na matumaini ya kuyakimbia maisha ya kulala nyumba ya kuvuja na taa ya kibatari.
Alitoka chumbani kwake na kwenda hadi kwenye mlango wa mama yake na kugonga.

"Mama..mama."

"Unasemaje Cecy," alimuuliza bila kuamka kwa vile tayari alikuwa amepitiwa na usingizi.

"Kuna jambo nataka tushauriane."

"Jambo gani, kwani lazima tuzungumze usiku?"

"Ndiyo, asubuhi nikiamka nijue cha kufanya."

"Mmh! Nakuja."

Mama yake aliamka na kutoka sebuleni, alimkuta Cecy amesimama, mama yake aliketi kwenye kigoda na kumtazama mwanaye aliyekuwa bado amesimama.

"Unasemaje mama?"

"Mama siku zote huwa nayaamini mawazo yangu japokuwa sina elimu kubwa, lakini busara haina elimu bali kipawa toka kwa Mungu."

"Ni kweli."

"Hivi mama tulipokuwa tukifanya biashara zetu tulipungukiwa nini?"

"Hatukupungukiwa kitu, kwani maisha ya mwanadamu Mungu ndiye anayetuongoza."

"Kwa hiyo hatuwezi kumtegemea mtu?"

"Ndiyo, kwani amelaaniwa kila amtegemeaye mwanadamu."

"Nimefurahi sana kulifahamu hilo."

"Ulikuwa unamaanisha nini?"

"Huoni kama tunamkosea Mungu kumtegemea mtu."

"Tunamtegemea nani?"

"Tumeacha kufanya biashara zetu kwa ajili ya Colin aliyetugeuza watoto kutuahidi pipi, leo ni siku ya ngapi hatufanyi biashara kwa ajili ya kusubiri ahadi yake. Wiki inakatika hakuna cha tofali wala mchanga."

"Cecy mwanangu, Colin naye binadamu huenda amepatwa na matatizo. Hivyo tulitakiwa kuvuta subira."
"Mama niliyajua haya mapema, sikutaka kukukata kauli kwa vile wewe ni mtu mzima. Lakini nilijua hakuna kitu, Colin atujengee nyumba kwa kipi cha maana tulichompa?"

"Kwa hiyo ulikuwa unasemaje?"

"Kesho asubuhi nakwenda Mabibo kununua ndizi na kuendelea na kazi yangu inayoniweka mjini."
"Mmh! Si wazo baya."

Walikubaliana siku ya pili Cecy aendelee na biashara yake ya ndizi kama kawaida. Kila mmoja alirudi chumbani kwake na kupanda kitandani. Cecy alichelewa kulala huku moyo ukimuuma kwa kitendo cha Colin kuwadhalilisha kwa kuwaahidi kitu kisichowezekana.

Alijikuta akimchukia Colin na kuapa hatazungumza naye siku zote za maisha yake. Kutokana na hasira alijikuta akichelewa kulala.

Siku ya pili, Cecy aliamka mapema na kuwahi kununua ndizi, baadaye alirudi nyumbani na kuoga kisha aliingia chumbani na kuchagua nguo za kuiingia nazo mtaani. Alitafuta gauni lililochoka na upande wa khanga uliopauka na kuvaa.

Alitoka kuelekea nje, alipofika mlangoni alisita kidogo na kujiuliza swali.

"Hivi maisha yangu namtegemea nani? Jibu Mungu, kwa nini niishi maisha kwa ajili ya mtu fulani? Ina maana bila Colin sina maisha? Hapana..hapana," Cecy alisema huku akirudi chumbani na kuvua nguo chakavu na kufungua sanduku lake na kutoa nguo nzuri na kuzivaa kisha alitoka na kuchukua beseni lake la ndizi na kumuaga mama yake akaingia mtaani kuuza ndizi.

Alishangaa siku ile, alimaliza ndizi mapema tofauti na alivyobadili mfumo wa maisha baada ya kuumizwa na penzi la Colin na kuamua kuishi kwa kutojijali. Toka alipoamua kuishi maisha yale, biashara yake haikuwa kama awali, alijikuta akimaliza biashara zake kwa kutembea umbali mrefu pia kutumia muda mwingi.

Alijikuta akijilaumu kwa kupoteza muda wake mwingi kumuwaza Colin, mwanaume asiye na mapenzi naye ambaye tayari alikuwa na mpenzi wake.

Moyo wake aliutoa kifungoni na kuwa tayari kupokea penzi jipya ila la mtu atakayempenda naye ampende ambaye atakuwa sahihi kwa moyo wake. Hakuwa tayari kumkubali mwanaume anayetumia umaskini wake kufanya naye ngono.

Siku zote aliamini mwenye mapenzi ya kweli hawezi kutanguliza ngono mbele zaidi ya upendo kwanza.
Lakini kwa Colin alikuwa radhi kuupoteza usichana wake hata bila ndoa kwani aliamini penzi la Colin lilizidi furaha ya maisha yake. Baada ya matukio yote aliamini muda wa uvumilivu ulikuwa umepita hivyo alitakiwa kitengeneza mawazo mapya na kuwaza kitu kingine kabisa kigeni katika ubongo wake.

Kila usiku ulipoingia alitumia muda mwingi kuwaza maisha wanayoishi ya kuuza ndizi, mwisho wake ni nini? Aliamini muda ule bado ana nguvu, alitakiwa atafute njia mbadala itakayomsaidia kukabiliana na ukali wa maisha aweze kumsaidia mama yake.

Wazo lilikuwa kila jioni baada ya kutoka kwenye biashara zake ambazo zilikuwa zikifanya vizuri japokuwa changamoto za wanaume zilikuwa kubwa ambazo alikabiliana nazo.

Wazo kubwa lilikuwa aanze kusoma masomo ya jioni kujifunza lugha ya kingereza ambayo ingemsaidia kufafuta kazi ya kuajiliwa na kuachana na kazi ya kuzurula huku akila vumbi la barabarani.

Wazo hilo alimwambia mama yake ambaye naye aliliafiki, jioni ilipofika alikwenda sehemu moja iliyokuwa ikifundisha twisheni na kuomba kusoma kingereza ambacho aliahidiwa kukijua baada ya miezi mitatu.

Alilipa ada na kuanza kusoma siku ileile huku akiwa na ndoto za siku moja naye kuzungumza kingereza.


Itaendelea..................
 
Mkuu kwema ni siku nyingine tdna. Tafadhali njoo tuendelee
 
Back
Top Bottom